0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Mar 15, 2016

Machale na utendaji wake (Intuition)



Wengi wetu tunadhani kwamba machale ni kitu cha kufikirika na hayafanyi kazi kama inavyosemwa. Ukweli ni kwamba machale yapo  na yanafanya kazi sema tu wengi hatufuati maelekezo ya machale yetu kila kitu tunabahatisha na mwisho wa siku ni sisi tunaoumia.

Leo nitaelezea namna kutumia machale yako ili yakusaidie kukuongoza katika shughuli zako na maisha yako ya kawaida.

Machale yako kwenye akili yetu ya kina (subconscious mind) na kama ilivyo kwa akili yako inavyokuunganisha na ulimwengu au jamii inayokuzunguka kutegemea na namna masafa yako yanavyotikisika na machale nayo yanakuunganisha na ulimwengu wa nje. kwa kukuongoza katika safari yako ya kutafuta mafanikio

Kwa hiyo wakati unapofikiria kufanya jambo lolote au kama unataka mafanikio kupitia kitu chochote machale yako yatakuwa yanakuongoza na kukuweka katika mazingira yatakayofanikisha safari yako ya mafanikio. Machale yatakuongoza katika kufanya maamuzi sahihi.

Kwa mfano kila mtu anahitaji awe na pesa au utajiri, kwa kuwa ni lazima uwe na kitu cha kubadilishana ili upate pesa unafanya upembuzi na kuona kwamba ukifanya biashara fulani au ukipata kazi fulani utaweza kuimarisha kipato chako na kupata mafanikio.

Hapa ndipo mtego ulipo, wakati unafanya jitihada za kutafuta mtaji ili kuanzisha hiyo biashara unajikuta unakwama lakini inatokea fursa nyingine ambayo unaweza kuifanya lakini unaiona kama isiyo na kipato unachokitarajia, hapo machale yamekuunganisha na bishara ambayo ndiyo itakayokuletea mafanikio ingawa siyo ile uliyokuwa unaitaka. Lakini pia kwa upande mwingine unaomba kazi fulani katika kampuni halafu unapangiwa kazi tofauti na ile uliyokuwa unaitaka, hapo machale yanakuongoza kupata kazi sahihi itakayotimiza ndoto zako.

Lakini wengine kwa kutojua namna machale yanavyofanya kazi hupuuza kila milango ya fursa inapofunguka kwa sababu fursa hiyo iko kinyume na malengo yao. Haya ni makosa yanayofanywa na watu wengi kwa kutofuata machale yanapowaongoza.

Kwa wale wanaojua utandaji wa nguvu ya mvuto ambao niliwahi kuileleza wakati fulani hapa  nilisema kwamba Mawazo yetu ya kina yanatengeneza mawimbi na yanavuta kila tunachokiwaza na kuwa ndio maisha yetu halisi. Sasa basi katika kuvuta tunachotaka machale kazi yake ni kukuongoza katika safari yako ya kupata unachohitaji. Kwa hiyo unaweza kushangaa kila unachoomba kinakuja kinyume na matarajio yako na hivyo  unapuuza na kuendelea kuhangaika ili ufanikiwe kwenye jambo hilo lakini juhudi zako hazielekei kuzaa matunda unayoyakusudia.

Kama utapuuza na kushindwa kufuata machale yako yanavyokuongoza utaishi kufanya maamuzi mabaya na kupoteza kile ulichokuwa unakitaka.

Hebu tuangalie mfano ufuatao:

Utendaji kazi wa machale…..

Labda tuseme unatafuta kazi, kwa hiyo unatuma maombi kwenye  kampuni fulani, hiyo ni baadaya kufanya uchunguzi kwa kuongea na watu wanaofanya kazi katika kampuni hiyo wakakuambia mambo mazuri wanayofanyiwa katika hiyo kampuni hususan mishahara na marupurupu mengi sana. Unavutiwa na hiyo kampuni na kutuma maombi huku ukiendelea kuelekeza nguvu zako za mvuto katika kampuni hiyo ili upate kazi lakini pamoja na kuitwa kwenye usaili na kufanya vizuri inatokea unapigwa dana dana katika kuipata hiyo kazi kwa ahadi za njoo kesho au subiri tutakuita.

Lakini siku moja unakutana na rafiki yako wa siku nyingi anakupa taarifa kuhusu nafasi ya kazi katika kampuni anayofanya kazi lakini nafasi hiyo iko kinyume na kazi unayotaka kuifanya, lakini pia hata hiyo kampuni huipendi na unaiona ni ndogo ukilinganisha na ndoto zako za kutaka kufanya kazi katika kampuni kubwa.

Hata hivyo kwa shingo upande unaomba na kufanya usaili na ndani ya muda mfupi unapata hiyo kazi ambayo baadaye inakuletea mafanikio makubwa na ndoto zako nyingi zinatimia.

Hapo machale yanakuongoza kupata kazi sahihi kwa ustawi wa maisha yako na si kazi uliyokuwa unaitaka. Ukweli ni kwamba machale na akili ya kina vinafanya kazi kwa pamoja.

Kwa hiyo kila tunachofanya au tunachotaka kukifanya, kama vile kupata kazi nzuri, kuanzisha biashara, kununua gari, kujenga nyumba au kujiendeleza kielimu vyote hivyo machale yatakuongoza lakini kama nilivyosema kuwa iwapo hutayasikiliza machale yako hakuna utakachofanikiwa kwani unaweza ukapata unachohitaji lakini kisikupe amani na matokeo yake ni vurugu tupu, na hapo ndipo unapoweza kumsikia mtu akisema, ‘machale yalinicheza wakati nilipotaka kufanya jambo fulani lakini nikapuuza sasa nimekwama.’

Kwa hiyo ni vyema sasa tukaanza kufuata machale yetu, tunatakiwa kuyapa umuhimu na kuyaelewa ili yaweze kutuongoza kwa kushirikiana na akili ya kina, na hapo ndipo utakapokuwa unafanya uchaguzi mzuri na kupata unachokihitaji.

Machale yanaweza kukupa taarifa kwa njia mbali mbali……

Ni zipi hizo?

Machale yanaweza kukupa taarifa kupitia njia zifuatazo:

1; Rafiki

2; Mpenzi wako au mwenzi wako, hapa kidogo kwa wanaume kuna ugumu kusikiliza machale yao kama taarifa itapitia kwa mke au mpenzi wake; kwani kutokana na mfumo dume wapo wanaume wengi tena kiasi cha kutosha hawawaamini wake zao au wapenzi wao, kwa hiyo machale yanapopitisha taarifa kupitia kwa watu hao, kuna ugumu kama taarifa hiyo itasikilizwa na kufuatwa.

3; Ndugu, jamaa na marafiki

4; mtoto njia hii nayo inaweza isiaminiwe kwa sababu siyo watu wote wanaoweza kuwaamini watoto, lakini ukweli ni kwamba watoto ndiyo njia inayotumiwa na machale katika kutoa taarifa kuliko njia nyingine yoyote

5; Radio na Magazeti kupitia taarifa mbalimbali zinazotanganzwa kupitia Radio au katika magazeti kwa mfano unataka kununua kiwanja au shamba, wakati umeshapata shamba na ukawa unataka kulipa halafu siku moja kabla ya malipo unasikia taarifa kupitia radio au magazetini kwamba eneo unalotaka kununua lipo kwenye mipango miji kwa hiyo wale waliojenge bila kufuata taratibu nyumba zao zitabomolewa na kama ni viwanja vitachukuliwa kwa matumizi yaliyokusudiwa. Hiyo ni taarifa ambayo imeletwa na machale.

6; Wapita njia au watu usiowafahamu wanaweza kukupa taarifa muhimu wakiwa kwenye mazungumzo yao yasiyokuhusu.

Labda unataka kuacha kazi baada ya kupata kazi mahali pengine ambapo walikuahidi kukupa mshahara mkubwa na marupurupu mengi sana, mara unakutana na watu wako kwenye mazungumzo yao lakini wanazungumzia matatizo ya kampuni inayotaka kukuajiri kwamba imefilisika na watafunga muda si mrefu au wanazungumzia ubaya wa mkurugenzi wa kampuni hiyo jinsi anayoajiri na kufukuza wafanya kazi hovyo kwa uonevu. Hii nitaarifa kupitia machale yako.

Niliposema machale yanakuunganisha na ulimwengu wa nje nilikuwa na maana hiyo kwamba kazi yake kubwa ni kukulinda kwa kukuongoza upite njia sahihi, kinachotakiwa ni sisi kuwa tayari muda wote kupokea taarifa ya machale yetu.

Watu waliofanikiwa na ambao wanaijua siri hii ya kutumia machale yao vizuri ndiyo hao tunaosema wana kismati, Bahati au kuwasingizia wana kizizi. Watu hawa ni ngumu kutapeliwa au kuingizwa chaka.

No comments:
Andika Maoni Maoni

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi