0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Mar 14, 2016

Kile kinachoitwa mwanamke kuzaa nje ya ndoa…..


 
Hivi sasa katika jamii yetu kuna kundi la wanawake ambao wana watoto lakini hawajaolewa lakini pia lipo kundi kubwa la wanawake ambao wako kwenye ndoa au mahusiano kwa muda mrefu lakini hawana watoto, hawa wamekuwa ni wahanga wa kubwa wa makanisa na hizi kliniki za tiba mbadala zilizosheheni hapa nchini zikidai kwamba zinasaidia wanawake kupata watoto.
Kundi hili la wanawake ambao hawajajaaliwa kupata watoto kwenye ndoa zao  wamejikuta wakipoteza fedha nyingi sana ili kupata watoto.

Dunia yetu imebadilika, mitindo ya maisha nayo imebadiliaka, mila desturi zetu nazo zimebadilika pia. Zamani vijana walikuwa wanalazimishwa na wazazi kuoa mapema na kama kijana akifikisha umri fulani hajaoa alikuwa anaonekana mtu wa ajabu tofauti na siku hizi shinikizo la vijana kuoa halipo tena kama zamani vijana wanawajibika kuamua wenyewe ni wakati gani waoe kwa sababu hata hivyo huduma ya ngono inapatikana hovyo.
Kwa upande wa wanawake nao shinikizo limebaki kwao, kwa kadiri umri unavyosonga ndivyo wazazi, jamii iliyomzunguka inavyozidi kumpa shinikizo la kuhoji kwa nini haolewi huku wanaume wakizidi kubaki huru na maamuzi yao.

Kwa wale ambao waliamua kuzaa kabla ya ndoa iwe ni kwa bahati mbaya au kwa kukusudia ambao wamebaki kuwa na watoto kabla ya ndoa wanao mtihani mwingine wa kupata wenza. Wanaume wengi wanashikwa na kigugumizi cha kuoa wanawake waliokwisha kuzaa.
Lakini wanaume hao hao unaweza kukuta nao wana watoto waliowazaa nje ya ndoa wakawatelekeza kwa mama zao. Hapo ndipo ilipo hadithi ya kuku na kifaranga haijulikani kipi ni kipi.

Bila shaka wengi wetu tumeshakutana na wanawake wenye kutafuta watoto wakiwa tayari umri umeshawatupa mkono. Ukweli ni kwamba, umri wa kupata watoto kwa wanawake umepungua sana tofauti na zamani.
Hivi sasa kutokana na mtindo wa maisha na vyakula tunavyokula watoto wa kike wanavunja ungo mapema hivyo wanaanza kushiriki ngono mapema, na hivyo kutokana na utoaji wa mimba holela au kutumia vidonge vya kuzuia mimba mapema wengi wamejikuta wakikosa uzazi pale wanapokata shauri ya kutafuta watoto. Lakini pia maradhi ya ngono yaliyoachwa kwa muda mrefu kabla ya kutibiwa yameathiri via vya uzazi vya wasichana wengi na hivyo kupoteza uwezo wa kuzaa.

Lakini pia vyakula tunavyokula na madawa tunayotumia yanayotibu maradhi mbalimbali nayo yana mchango katika tatizo hilo.
Sasa basi labda changamoto tuliyo nayo kwa sasa ni je kuna haja kweli kwa wanawake kuwa na ulazima wa kusubiri mpaka kufunga ndoa ndipo wapate watoto au wanaweza kupata watoto kabla ya ndoa kutokana na kuepuka umri kuwatupa mkono na kupoteza kabisa uwezo wa kuzaa.

Je jamii inawachukuliaje wanawake wenye watoto kabla ya ndao? Je hawastahili kuolewa?

No comments:
Andika Maoni Maoni

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi