Nov 22, 2009

NI MAMA! SEHEMU YA MWISHO

Ø Amtazama mtoto na kusema bila mabadiliko atakufa mtu
Ø Awabadilikia mume na binamu zake dakika chache baada ya ndoa
Ø Atangaza kwa mtoto kwamba yeye ni mama aliyekufa zamani amerudi

Mwaka ukakatika na wenzangu wa lifunga na kufungua shule wakaingia darasa jipya, mwaka 1973. Nilitakiwa niwe darasa la tano, lakini badala yake nilishaanza kuzoea maisha ya mitaani. Mwaka huo huo, Februari ndipo ambapo baba aliamua kuoa. Nilisikia akiwaambia wale ndugu zake habari hizo. Mmoja kati yao, yule ndugu wa binamu yake aliyekuwaq akiitwa Hamadi ambaye alikuwa akinichukia sana, alimwambia baba kwamba, ningemsumbua sana huyo mkewe. Baba alisema kwamba, kama ninataka kufa, hapo ndipo palikuwa pahala pazuri pa kufia. Aliongeza kuwambia kwamba, angemtahadharisha sana huyo mke wake mpya kuhusu mimi.

Kweli alioa kwa sherehe ndogo ambayo ilifanyika pale pale nyumbani. Baba alikuwa amepanga nyumba nzima ya vyumba vitatu, tulimokuwa tukiishi. Nilikwambia nilikuwa nikilala sebuleni, unaweza kuhisi kwamba, labda ninajaribu kuongopa. Nitakwambia ni kwa nini baba yangu alikuwa akinichukia.

Baada ya sherehe ile ya ndoa, ambayo ilihusisha ndugu zake yule mama wanne na wale binamu wa baba na mimi ambaye pale nilikuwa kama kijana wa kutumwa, ulifika muda wa mke wa baba kutambulishwa kwa familia. Baba aliwatambulisha wale ndugu zake wawili kwa yule mama mpya. Halafu alimwambia yule mkewe ambaye nilishamchukia hata kabla hajaolewa, ‘huyu ndiye yule mtoto niliyekwambia. Kama akikukera muda wowote naomba nipate taarifaharaka ili nimfunze adabu. Na vitu vyako uviweke vizuri, maana……’

Yule mama yangu mpya wa kamboa aliingilia kati. ‘Sawa nimekuelewa, lakini kwa nini usiniache mwenyewe nikaona kama kweli ni morofi?’ Huyu mama ambye naye alikuwa mtu mzima kidogo, akiwa ni mwalimu aliyewahi kufundisha na baba wakati baba anaanza kazi, alisema huku nikiona wazi kwamba, kauli za baba hazikumshawishi.

Wale ndugu zake baba walicheka na kusema, ‘kwani shemeji tangu uje hujaona kwamba huyu ni mtoto wa mtaani huj….’ Yule mama mpya alimwambia binamu yangu. ‘Nikiwa humu ndani, nisikusikie tena unasema hayo maneno. Nimesema mniache nione mwenyewe, mnanifundisha nini sasa!’ Mama alionekana wazi kwamba alikuwa amekasirika.

Nilihisi kama vile nataka kucheka au kuruka kwa furaha au kulia au sijui kufanyaje, sikujua tu. Hajawahi kuja mgeni pale nyumbani na kuambiwa mambo yangu na kuacha kuwaunga mkono baba na ndugu zake. Yule alikuwa ni mtu wa kwanza. Halafu kumbuka alikuwa ni mama wa kambo ambaye nilitegemea angekuwa katili kuliko baba. Lakini kumbe bado nilikuwa sijagundua jambo kubwa zaidi.

Jioni ile baba na ndugu zake na mkewe ilikuwa watoke kwenda kutembea mjini kukamilisha ile sherehe ya ndoa. Baba alitoka kwenda kwanza dukani na ndugu zake walitoka nao sijui kwenda wapi. Tulibaki mimi na mama yule mgeni.

Kwenye saa 10.30 jioni yule mama alipokuwa ametoka kuswalialiniita na kuingia nami chumbani kwa baba. Nilisita kuingia kwa sababu nilikuwa nimepigwa marufuku hata kusogelea mlango wa chumba hicho, Ingawa binamu zake binamu zake baba walikuwa wakiiba fedha za baba na kudai ni mimi. Ingia Almasi, usiogope mimi ni mama.'

Niliingia na mama aliniambia nikae kitandani. 'Unasikia mwanangu, usikubali kuwa wewe ni mtundu.' Yule mama alianza kusema akiwa amnishika mkono. 'Wewe ni mtoto mzuri, mwenye akili na huruma. Nimekuona ile asubuhi nilipokuja, kwamba, huna tatizo hata kidogo.'

Alinyamaza na kuendelea kusema, 'najua unafahamu kwamba, mama yako alikwishafariki, lakini akina mama wanpofariki, hurudi kwa njia nyingine, kuja kuwapenda tena watoto wao. Nimerudi kuja kukupenda ili usome na kufika mbali sana. Lakini usimwambie mtu. Mimi ni mama yako, nataka nikuone ukiwa shujaa kama wakati ule ulipokuwa mdogo….’ Alitulia kidogo, alikuwa akilia.

Unajua ulipokuwa mdogo ulitambaa na kutembea haraka sana kuliko watoto wengine pale mtaani, hadi watu wakashangaa. Nataka uendelee kuwa mtoto mzuri na mwenye bidii kama wakati ule. Kumbuka kwamba, mimi ni mama nimekuja kukulea.’

Akiwa anafuta machozi aliniambia. ‘Tafuta zile nguo zako nzuri, nikiandalie, jioni tutaenda wote na baba na baba kutembea mjini.’ Nilihisi kitu ambacho hadi leo wala sikijui kilikuwa ni nini. Nilijiona kama siko duniani au sijijui. Nilibubujikwa na machozi na nilisema kwa kunong’ona, ‘sina nguo nzuri.’

Yule mama alisimama na kusema, usijali mwanangu.’ Alikwenda kwenye sanduku lake na alilokuwa amekuja naloasubuhi ile na kulifungua. Alitoa suruali, shati na viatu, vyote vipya. Aliniambia nikaoge, halafu nivae nguo zile.

Nikiwa na kichwa chepesi hadi kufikia kuyumba, bila kujua sababu, nilikwenda kuoga. Nilimwacha mama huku nyuma akiwa bado anafuta machozi yake. Nilirudi bafuni na kuvaa nguo zile. IliIlikuwani mara ya kwanza kwangu kuvaa nguo mpya nikiwa na akili ya kukumbuka, ukiacha sare za shule. Mama alinisifia sana na nilihisi ile hali ambayo sikuwa ninaijua. Hali ngeni kabisa.

Saa 11.30, baba na wale ndugu zake walirudi na awali hakuna aliyenitambua. Waliponitambua, binamu binamu yake baba alisema, ‘umeiba wapi nguo hizo?’Nilimtazama mama ambaye nilikuwa naye pale sebuleni, naye kama kuonyesha kunilinda kam alivyoahidi alisema. ‘Ni mimi nimeiba, Unasemaje?’ Palizuka kimya. Halafu mama alisema maneno ambayo siwezi kuyasahau.

‘Huyu ni mwanangu. Hana tabia mbaya na wala sio mjinga kama mnavyotaka aamini. Huyu ni mtoto mjanja na mwenye uwezo mkubwa wa ufahamu. Nataka niseme hivi. Huyu ndiye atakayeniweka au kuniondoa katika nyumba hii. Akionewa tu, nafunga kilicho changu, naondoka na sioni aibu kusema kwamba nitaondoka naye. Nimemaliza.’ Hakuna aliyejibu labda kwa sababu hakuna aliyeamini.

Alinyamaza na kuendelea kusema, 'najua unafahamu kwamba, mama yako alikwishafariki, lakini akina mama wanapofariki, hurudi kwa njia nyingine, kuja kuwapenda tena watoto wao. Nimerudi kuja kukupenda ili usome na kufika mbali sana. Lakini usimwambie mtu. Mimi ni mama yako, nataka nikuone ukiwa shujaa kama wakati ule ulipokuwa mdogo….’ Alitulia kidogo, alikuwa akilia.

‘Unajua ulipokuwa mdogo ulitambaa na kutembea haraka sana kuliko watoto wengine pale mtaani, hadi watu wakashangaa. Nataka uendelee kuwa mtoto mzuri na mwenye bidii kama wakati ule. Kumbuka kwamba, mimi ni mama nimekuja kukulea.’

Ni kweli hakuna aliyesema neno na sikusikia neno kwa siku ile wala zilizofuata. Wiki ile ile nilianza masomo na wale ndugu zake baba waliondoka miezi miwili tu baadae baada ya kushindwa kuishi na mama ambaye alikuwa ni mtu mnyoofu, anayesema kile ambacho kipo na kinachopaswa kusemwa. Hata baba aliwachukia sana.

Huyu mama ndiye ambaye alimbadili kabisa baba na kumfanya kuwa mtu tofauti kwangu. Nikiwa na umri wa miaka 13 ndipo nilipoanza kujua upendo wa baba na mama.

KWA NINI BABA ALIKUWA ANANICHUKIA? Niligundua kwamba baba katika kuhangaika kwake kwa waganga, aliambiwa kwamba mimi nilizaliwa na mkosi, hivyo kifo cha mama kilikuwa kimepitishwa mikononi mwangu na wachawi na kwamba kama ningekuwa mtu mzima nikiwa kwake, ningesababisha mikosi kwa familia yake. Kwa hiyo baba hakutaka niwe mtu mzima nikiwa kwake.

Mama yangu wa kambo ambaye ndiye mama yangu mzazi kwa ninavyoamini kutokana na upendo wake, ndiye aliyebadili mawazo ya baba ya kishirikina na kumfanya kuanza kufikiri vizuri zaidi kuhusu mimi na maisha kwa ujumla.

Leo hii baba yangu amefariki, lakini mama yangu ninaye, nikiwa na mdogo wangu wa kike ambaye ameolewa na ana shughuli zake, anaitwa Shamim. Huyu mdogo wangu hakuzaliwa na baba yangu, kwani huyu mama mwema alipokuja kuolewa na baba tayari alishaolewa na kuachana na mumewe na walikuwa na mtoto huyo.

Huyu mama ndiye ambaye ameniwezesha kuishi maisha haya ya uadilifu na amani niliyo nayo leo. Ndiye ambaye aliniwezesha kusoma hadi chuo kikuu na kupata ajira na baadae kuanza maisha ya kujitegemea. Ni kweli alikuwa ni mama yangu aliyekuja kunilinda.

Najaribu kufikiria,kuna akina mama wangapi wanoweza kumkubali mtoto wa mwanamke mwingine kama alivyo? Ni wachache kupindukia. Wengi juhudi yao siku zote ni kuona watoto wa kambo wanakorofishana na baba zao, wanateswa na kutupwa nje ya familia. Lakini ni kwa faida ya nani? Siku zote ni kwa hasara zao. Huja kugundua wamepata hasara wakiwa wamechelewa uzeeni.

Ninampenda na nitampenda kuliko mtu mwingine yeyote, mama Zakia Mudani, ambaye amenionesha maana ya kweli kuhusu maisha. Amenifundisha kwamba, suala siyo mama wa kambo, bali ubinadamu, kujua kupenda.

Alikuwa ni mama………………

**************MWISHO***************

Nov 21, 2009

NI MAMA!

Alikuwa ni mama!

Ø Amtazama mtoto na kusema bila mabadiliko atakufa mtu
Ø Awabadilikia mume na binamu zake dakika chache baada ya ndoa
Ø Atangaza kwa mtoto kwamba yeye ni mama aliyekufa zamani amerudi

Nina uhakika kuhusu watoto wanaoteswa na wazazi wao, wanavyojisikia. Nina uhakika kwa sababu, niliwahi kutokea kuwa mmoja kati ya hao. Lakini pia najua kuhusu watoto wanaoteswa na hata kudhuriwa na kimaisha na mama zao wa kambo. Hapa kwenye hili sitaki kusema chochote kwa sasa.

Kwa jina naitwa Almasi Halifa Nimetimiza miaka 49 kamili Julai mwaka huu, 2009. Nilizaliwa Kilosa ambako baba yangu alikuwa mwalimu wa shule ya msingi. Nikiwa na miaka minne hapo hapo Kilosa kwenye kitongoji cha Ulaya, mama yangu mzazi alifariki wakati akijifungua. Bahati mbaya zaidi ni kwamba alifariki yeye na mtoto wake, ambaye angekuwa ndiye mdogo wangu pekee.

Baada ya mama kufariki, baba aliomba uhamisho kwa imani kwamba, kifo cha mkewe kiliwa ni mono wa mtu. Alipewa uhamisho na kupelekwa sehemu inayoitwa Wami Dakawa humohumo mkoani Morogoro. Nikiwa na miaka minane, baba aliamua kuacha kazi. Wakati huo, kwa mujibu wa kumbukumbu zangu alikuwa kama amechanganyikiwa kidogo.

Nasema alikuwa kama amechanganyikiwa kwa sababu alikuwa ni mkali sana, mkatili, na anayeonesha kabisa kwamba, hakuwa na amani na nafsi yake. Pamoja na kwamba likuwa ni mwalimu {Kabla hajaamua kuacha kazi} Mimi mwanaye nilianza shule nikiwa na miaka minane baada ya kuhamia Dakawa. Tema huko akuanza shule kulitokana na shinikizo la wenzake.

Ukweli ni kwamba tangu kifo cha mama yangu, baba yangu alikuwa kama adui yangu. Nikiwa na miaka mitano alikuwa akiniachia kazi kama kupika mboga, hasa maharage na nyingine zenye kuhitaji kukagua maji tu. Nilifanya kazi hizo na kuna wakati nilikuwa nakosea.

Nikiwa na miaka mitano nilikuwa napigwa sdana kwa makosa ambayo hata mtu wa miaka 15 asingekwepa kuyatenda. Nilikuwa nashinda na kulala na njaa wakati mwingine. Kuna wakati ba aalikuwa anaondoka na kwenda kushinda kwenye kaduka kake kalikokuwa karibu na eneo la sabasaba, bila kuacha chochote. Sisi tulikuwa tukiishi mji mpya.

Nilikuwa nashinda na njaa au kulala na njaa kwa sababu alikuwa akiondoka asubuhi akiwa amesahau au kufanya kusudi bila kuacha chochote na alikuwa akichelewa sana kurudi. Hakuwa mlevi, lakini sijui alikuwa akipotelea wapi.

Kulikuwa na watoto jirani tuliokuwa tukisoma wote, ambao nadhani walikuwa wamewaambia wazazi wao kuhusu maisha yangu. Kwani wazazi wao waliwaambia waniambie niwe naenda kule nyumbani kwaokama kujisomea kidogo. Lakini nilijua walikuwa walikuwa wakitaka niende hapo kwa ajili ya kula.

Hii ilinisaidai kidogo kwa sababu, hata kama nisingekunywa chai asubuhi, kwa kuwa shule tulikuwa tukila buruga {aina ya uji wa njano}, nilijua jioni ningepata chakula cha kwa rafiki zangu. Sijui hata hivyo ilitokeaje,kwani baba alijua nakula ile nyumba ya jirani. Kwa kweli nilipigwa sana siku hiyo na alikwenda pel kuwatukana wale wasamaria wema.

Nilianza tena maisha ya mateso na shida. Lakini wale wenzangu walikuwa wakiniambia kwamba, nivumilie kwani nitakuwa mkubwa na nitalipiza kwa baba. Wakati nikiwa darasa la tatu walikuja ndugu zake babawawili kuishi nasi. Mmoja biamu yake na mwingine ndugu wa huyo binamu. Walikuwa bado vijanawadogo tu , hawakuwa wanzidi miaka 20.

Sasa hapo mateso yalikuwa makubwa sana. Hawa jamaa walikuwa wanafanya makosa na kunisingizia mimi. Walikuwa wakiiba fedha za baba, walikuwa wakiharibu vitu na nilikuwa nasingiziwa mimi. Nilikuwa napigwa sana. Hawa ndugu zake baba nao walikuwa wakinipiga sana bila makosa.

Walikuwa wakijitahidi sana kuninyima chakula na mambo ya namna hiyo. Nikiwa hilohilo datrasa la tatu niliamua kuacha shule. Sikuona sababu ya kusoma, na nilijua nisingemudu tena. Nilikuwa nikienda karibu na kiwanda cha tumbaku, eneo ambalo linaitwa Tumbaku kufanya vibarua. Kwa mwaka mzima sikuhudhuria shule na nnilianza kweli kuwa mtundu.

Huko nilianza hata kujifunza kuvuta bangi, ingawa mara chachechache. Nilijifunza kuchungulia wanawake wanaooga hapo karibu na kiwanda, kama walivyokuwa wakifanya wakubwa. Baba hakuwa akijua kwamba nilikuw siendi shule na pengine hata angejua asingejali , kama angejali ingakuwa ni kwa kunitimua hapo nyumbani tu labda.


Asubuhi nilikuwa na sare za shule na huku nikiwa na nguop za kazi kwenye mfuko wangu wa madaftari. Jioni, nilikuwa narudi kama vile nimetoka shule. Wale ndugu zake baba waligundua kwamba, nilikuwa sijali kuhusu chakula chaona nilikuwa nawajibuhovyo, hivyo walinikomoa. Walimwambia baba kuwa nakula kwa jirani na eti nimesema baba anamalizia fedha zake kwa wanawake.

Nadhani ujumbe waliotaka kumpa ndugu yao, yaani baba, bali wakaona ingekuwa salama kwao kuupitishia kwangu. Siku hiyo nilipigwa hadi jirani ikabidi waingilie kati. Baba alinitukana sana, hasa kwa kunisimanga kuhusu mama yangu kufa.

Nilitahayari sana na ilibidi nimwambie kwamba, kama yeye ana akili mbona ni masikini. Sijui hata nilifikiria nini kusema hivyo. Niliamua sasa kwamba sijali. Nilikuwa natoka asubuhi bila sare za shule bali na nguo zangu za kawaida na kwenda kibaruani. Nilikuwa nimekata tamaa bila shaka.
FUATILIA MKASA HUU WA KUSIKITISHA KESHO..........

Nov 8, 2009

HANDSOME ALIYEITIKISA KENYA-SEHEMU YA MWISHO.....

Simon Matheri Ikere

Mwili wa Simon Matheri baada ya kuuawa

Ndugu wasomaji wa Blog hii, nimekuwa nikipokea ujumbe kupitia simu yangu ya kiganjani kutoka kwa wasomaji wakinishauri kuwa nisiwe nachelewa kuweka muendelezo wa visa na stori ninazoweka humu na pia nisiwe nachelewa ku up date blog hii mara kwa mara.
Naomba nikiri kuwa, hiyo imetokana na mlundikano wa majukumu niliyo nayo kwa sasa, naomba mniwie radhi, na nitajitahidi kuweka mada mbali mbali humu kama kawaida.
Pia ningependa kuweka wazi kuwa hizi kesi au habari za kiuhalifu ninazoweka humu pamoja na ushuhuda sio habari au visa vya kufikirika bali ni habari za kweli kabisa.
Haya, sasa tuendelee ya ile habari ya kule nchini Kenya………

ILIPOISHIA…..
Kitendo cha kuchoma nyumba yake mwenyewe ambayo aliijenga kwa msaada wa baba yake, kilimuuzi sana mzazi huyo na hivyo kumfungulia mashtaka ambapo alifungwa miaka mitano jela.

ENDELEA….

Matheri alitumikia kifungo chake cha maiak mitano katika jela yenye ulinzi mkali ya Kaimiti ambayo hutumika kwa wafungwa sugu wa ujambazi. Katika kipindi ambacho alikuwa jela, huku nyuma familia yake iliishi kwa amani, ambayo hata hivyo ilitoweka mara baada ya Matheri kuachiwa huru kutokana na kumaliza kifungo chake.

Awali wazazi wake walidhani alikuwa amebadilika kitabia kutokana na kutumikia kifungo cha miaka mitanojela, kitu ambacho haikuwa sahihi. Kumbe katika kipindi hicho ambacho alikuwa akitumikia kifungo ndipo alipo alipohitimu na kuwa jambazi sugu.

Baba yake alikiri kwambanaamini mwanaye alifuzu kuwa mwizi na jambazi sugu kwa kufunzwa wakati alipokuwa katika jela ya kamiti, jela amayo hutumika kuwafunga wahalifu sugu. Baada ya kutoka jela, baba yake aliamua kumjengea mwanaye huyo nyumba mpya akiamini kwamba atakuw aamebadilika, lakini hali ilikuwa tofauti, na nyumba hiyo badaye ilikuja kuchomwa moto na na watu wenye hasira kali kutokana na kukerwa na vitendo vyake.

Alipotoka jela tu Matheri alinunua bunduki aina ya AK-47 kutoka kwa wakimbizi wa Somalia na katika hali isiyo ya kawaida, alimtishia kaka yake kwa bunduki hiyo baada ya kutofautiana katika mambo ya kawaida tu. Baada ya mkasa huo, ilibbbidi familia ilifahamishe jeshi la Polisi, ambapo Polisi walianza kumtafuta. Kama vile machale yalimcheza, Matheri alitowerka haraka sana pale nyumbani kwao na akawa anakuja pale mara chache sana tena usiku wa manane.

Pilika zake za ujambazi zilianzia katika wilaya ya Murang’a. Akiwa na washirika wake, Matheri aliendesha ujambazi katika wilaya hiyo, mpaka alipokoswakoswa kuuwawa na Polisi katika msitu mmoja ambapo walikuw awakifuatiliwa na Polisi ambao walikuwa wanatumia mbwa wa kunusa. Katika tukio hilo washirika wake wawili waliuawa nay eye aliponea chupuchupu baada ya kujitumbukiza katika mtowenye maji yaendayo kwa kasina kupotelea kusikojulikana.

Baada ya tukio hili Matheri alihamishia makazi yake katika jiji la Nairobi ambapo pia alikuwa akitoka na kuingia katika miji mikuu ya Afrika Mashariki na kufnya uharamia na kisha kutoweka kutoka mji mmoja hadi mwingineili kuwakwepa Polisi.

Katika kipindi ambacho Matheri aliendesha uharamia katika wilaya ya Murang’a, familia yake nayo haikusalimika. Mara nyingi familia hiyo ilivamiwa na wannchi wenye hasira kali na kuchomewa nyumba ili kulipiza kisasi. Mzee Ikere alidai kwamba kila wakti mtu anapovamiwa na majambazi katika miji ya Nairobi, Mombasa, Kisumu au mji wowote, Familia yake ilikuwa ikipata usumbufu mkubwa, kwani walikuwa wakipata wageni ambao huja kulipiza kisasi kwa kufanya uharibifu mkubwa ikiwa ni pamoja na kuchoma nyumba za familia hiyo.

Ilifikia mahali hata wizi mdogo mdogo wa kuku, jina la mwanye lilihusishwa na wizi huo, kitu ambacho haikuwa kweli. Tukio ambalo Mzee Ikere anasema hatalisahau ni pale aliposhambuliwa kwa mapanga na mikuki na watu wenye hasira kali ikiwa ni katika kulipiza kisasi, kiasi kwamba aliachwa na majeraha huku akivuja damu bila kupata msaada wowote kutoka kwa majirani zake. Ilitokea hata watu wenye magari waliotaka kumpa msada ili kumpeleka hospitalini walikuwa wakitishwa kwamba nao wangeshughulikiwa. Kutokana na usumbufu huo, ilibidi waombe msaada polisi ili familia hiyo ipate msaada wa ulinzi lakini hawakupata msaada huo.

Hadi kufikia mwaka 2007, jina la Simon Matheri Ikere lilikuwa likivuma nchini Kenya kutokana na uhalifu aliokuwa akiundesha yeye na genge lake. Lakini kama waswahili wanvyosema, hakuna marefu yasiyo na ncha. Ilipofika Februari 20, 2007 ukawa ndio mwisho wa mtu huyu.

Kuuawa kwa Matheri kulipokelewa kwa hisia tofauti na jamii ya Wakenya, miongoni mwao zilikuwa ni taasisi za watetezi wa haki za binadamu. Taasisi hizo ziliwashmbulia Polisi kwamba walitumia kauli ya Waziri wa Usalama wa raia, Mheshimiwa Michike vibaya. Taasisi hizo zilipinga waziwazi kuhusu kuuawa kwa Matheri na kuwashutumu Polisi kwamba hawakumtendea haki Matheri kwani alipaswa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria na kuhukumiwa kama mhalifu mwingine yeyote.

Naye mama yek mzaziMatheri, Martha Wanjiru akizungumza mara baada ya kupata taarifa za kuuawa kwa mwanye na Polisi, alisema kwamba, alijua kuwa ipo siku mwanaye huyo angeuawana hatimaye siku hiyo imefika. Mama huyo alikiri kwamba ni takribani mwaka mmoja ulikuwa umepita bila ya kumwona mwanaye.

Huku akionekana kujuta, mama huiyo alisema, “Kama ningejua, mamba ya mwanangu huyu niliyemzaa miaka 30 iliyopita, ingezaa mtoto atakayekuja kuwa muuajina kuniletea usumbufu mkubwa utakaoniumiza moyoni mwangukatika maisha yangu yote, hakika nisingemzaa, lakini hilo ni jambo ambalo siwezi kulifanya.”

Mama huyo anakiri kwamba kuna wakai aliwahi kumsihi mwanaye ajisalimishe mikononi mwa Polisi, kwani hiyo ndiyo njia pekee ambayo ingepelekea kufikishwa kwenye vyombo vya sheria na kuhukumiwa kwa haki, lakini mwanaye hakukubali, badala yake akaendelea na vitendo vyake vya ujambazi.

Naye mkewe Matheri, Bi Felistus Wanjiru akimwelezea mumewe, alisema kwamba Matheri alikuwa ni mpole sana na hakuwa ni mtu wa maneno mengi. Bi Wanjiru alidai kwamba katika kipindi chote alichoishi naye hakujua kwamba mumewe alikuwa ni jambazi sugu aliyekuwa akitafutwa na Polisi.

Hata hivyo hatua inayochukuliwa na Polisi nchini Kenya ya kuwauwa majambazi kama Matheri, imewagawa wakenya katika makundi mawili. Lipo kundi linaloona kama ile ilikuwa ni hatua sahihi ya kukomesha ujambazi nchini humo, na kundi jingine linaona kuwa, hiyo haikuwa ni njia sahihi ya kukomesha ujambazi.

Je, kw Polisi kuendesha mauaji ya namna hii kwa watu wanishukiwa kuwa ni majambazi sugu, hakuliweki Taifa la Kenya katika miongoni mwamnchi zinazokiuka haki za binadamu?
Je, hali hiyo haiwezi kuufanya uhalifu kuwa wa kutisha zaidi, kwani majambazi hawatosita kuuwa wakati wanapofanya uporaji, kwa sababu wanjua hata wao wakipatikana watauawa?

Hayo yote ni miongoni mwa maswali ambayo Wakenya wengi walikuwa wakijiuliza na bado wanjiuliza, na mwenye majibu ya maswali hayo ni serikali yenyewe ya Kenya

****************Mwisho*********************

Oct 31, 2009

HANDSOME ALIYEITIKISA KENYA-SEHEMU YA PILI

Ilipoishia..............
Baada ya kumuuwa Matheri Polisi katika upekuzi walioufanya katika nyumba yake walikuta bunduki aina ya AK-47 pamoja na risasi 26. Hata hivyo upo utata uliojitokeza katika taarifa zilizonukuliwa kutoka pande mbili, yaani upande wa Polisi na mke wa Matheri kwa upande mwingine.

Endelea kufuatilia kisa hiki hapa chini…………..

Kwani kwa upande wa Polisi walidai kwamba wakati wnmuuwa Matheri alitoka akiwa na bunduki aina ya AK-47 na hivyo kuwalazimisha Polisi kumuuwa ili kujihami, lakini kwa upande wa mkewe, Felister Wanjiru ambaye alikuwa na ujauzito wa miezi saba wakati huo, akihojiwa na kituo cha Luninga cha KTN alidai kuwa mumewe alitoka akiwa hana silaha yoyote, tena alitoka akiwa kifua wazi akiwa amevaa kaptula, maarufu kama Bukta huku akiwa ameweka mikono yake kichwani ili kuwaonesha Polisi kwamba hakuwa na silaha yoyote, lakini kwa mshangao Polisi walimmiminia risasi mumewe na kumuuwa palepale.

Akisimulia zaidi mkasa huo katika kituo hicho cha Luninga, Wanjiru alisema kwamba siku ya tukio alikuwa amelala na mumewe chumbani, mara akasikia michakato ya miguu nje ya nyumba yao, lakini mumewe hakuonekana kwamba alikuwa na wasiwasi, baadae walisikia sauti ya Polisi waliokuwa nje ya nyumba yao wakijitambulisha na kumtaka mumewe atoke nje na ajisalimishe haraka la sivyo wataichoma nyumba moto na kuwauwa wote waliomo ndani.

Mumewealiposikia hivyo alijificha chini ya mvungu wa kitanda ili kuokoa maisha yake. Baada ya kuona kwamba Polisi wanazidi kusisitiza msimamo wao, ilibidi amsihi mumewe ajisalimishe ili kuokoa maisha ya watoto wake, kwani katika nyumba ile walikuwa yeye Wanjiru na mumewe Matheri pamoja na watoto wao 6, huku Wanjiru akiwa akiwa na ujauzito wa miezi 7.

Akizidi kusimulia, Wanjiru alisema kwamba mumewe aliamua kutii amri ya Polisi na kutoka nje huku akiwa amevaa bukta na mikono yake ikiwa nyuma ya kichwa. Alipofika nje aliamriwa apige magoti huku akiwa ameweka mikono yake nyuma ya kichwa na aache kinywa wazi , kitu ambacho alitii.

Ndipo Polisi mmoja alipomsogelea mahali alipo na kutumbukiza mdomo wa Bunduki yake kinywani mwa Matheri na kisha kuifyatua sawia, huku kila mtu akishuhudia. Katika mauaji hayo, Polisi walikiri pia kumuuwa mtu mwingine ambaye inasemekana alikuwa ni mlinzi binafsi wa Matheri {Bodyguard}. Utata wa namna Matheri alivyouawa haukusumbua vichwa vya Wakenya walio wengi, kwani kwao hiyo haikuwa ni hoja, bali cha msingi kwao ilikuwa ni kusherehekea kuuawa kwa Matheri.

Katika kijiji alichozaliwa Matheri kilichopo magharibi mwa jiji la Nairobi vituo vya Luninga nchini Kenya vilikuwa vikionesha wakazi wa kijiji hicho wakishrehekea kwa nyimbo za kuwasifia Polisi kwa ushujaa wao wa kumuuwa mtu ambaye alikuwa ni tishio kwa usalama wao na mali zao.

Hatua ya kluuawa kwa Matheri inasemekana ni katika kutii amri ya waziri wa usalama wa raia nchini Kenya, Mheshimiwa John Michuki ambaye Wakenya walimpa jina la utani la “Kimeendero” au “Crusher” ya kuwaamuru Polisi kuwauwa majambazi pale wanpoonekana kukabiliana na Polisi kwa silaha.

Simon Matheri Ikere kijana mzuri mwenye sura ya mvuto na mpole kupindukia alikuwa ni mtoto wa nane kuzaliwa akiwa ni kitinda mimba wa familia ya Mzee Peter Ikere Gichungu aliyekuwa dereva wa malori nchini humu na mkewe Martha Wanjiru, mama wa kilokole.

Kwa mujibu wa maelezo ya wazazi wake, Simon Matheri Ikere alizaliwa mwaka 1977 na katika kipindi chote cha utoto wake hakuwahi kuonesha tabia ya wizi. Tabia walioijua aliyokuwa nayo tangu utoto wake ni ile ya kuwa na hasira za ziada ambazo hawadhani kama ndio chanzo cha mtoto wao kuwa jambazi sugu.

Baba yake alisema kwamba mwanaye alishindwa kuendelea na masomo ya elimu ya msingi katika shule ya msingi Kihara akiwa darasa la sita. Mzee huyo alikiri kutojua sababu hasa ya mwanaye kuacha shule akiwa darasa la sita ili hali alikuwa na maendeleo mazuri tu shuleni.

Baada ya kumuona mwanye ameacha shule, Mzee huyo akaamua kumpeleka katika eneo la Wangige ambalo ni maarufu kwa shughuli mbalimbali za ufundi, maarufu kama Jua Kali nchini Kenya.

Matheri alipelekwa katika eneo hilo ili akajifunze ufundi wa kuchomea vyuma {Welding}. Baba yake anakiri kwamba huenda katika eneo hilo la Wangige ndipo mwanaye alipojifunza tabia ya uchomaji wa nyumba moto {Arsonist}, ingawa hata hivyo wataalamu wansema tabia hii ni maradhi.

Siku moja miaka saba iliyopita ndipo vitendo hivyo vya uchomaji nyumba moto vilipoanza pamoja na usumbufu mdogo mdogo katika familia. Mzee huyo anakumbuka siku moja likuw ametofautiana naye na kutokana na hasira zake za ziada Matheri aliamua kuchoma nyumba yake mwenyewe na kisha kutoweka.

Kitendo cha kuchoma nyumba yake mwenyewe ambayo aliijenga kwa msaada wa baba yake, kilimuuzi sana mzazi huyo na hivyo kumfungulia mashtaka ambapo alifungwa miaka mitano jela.

Ni nini kitatokea baada ya Matheri kumaliza kifungo chake….Fuatilia kisa hiki kesho

Oct 30, 2009

HANDSOME ALIYEITIKISA KENYA.

Jiji la Nairobi, Moi Avenue


Siku ya Jumanne ya Februari 20, 2007 ni siku ambayo haitasahauliwea na Wakenya wengi, na hasa Polisi wa nchi hiyo. Ni siku ambayo Polisi zaidi ya 100 wa nchi hiyo kutoka kwenye kitengo maalum cha kupambana na uhalifu walifanikiwa kumuua jambazi mmoja sugu na aliyekuwa akitafutwa kwa udi na uvumba aliyejulikana kwa jina la Simon Matheri Ikerealiyekuwa na umri wa miaka 30.

Akiwa bado ni kijana mmbichi wa umri wa miaka 30, Simon Matheri Ikere alikuwa ni jamabzi hatari aliyekuwa akivuma katika viunga vya jiji la Nairobi kama mzimu kiasi cha Polisi kukiwekea kichwa chake dau la shilingi za Kenya zipatazo 150,000 kwa mtu yeyote ambaye angefanikisha kukamatwa kwake.

Ilikuwa ni majira ya saa nane na nusu za usiku wa Jumatatu kuamkia Jumanne, Polisi zaidi ya 100 waliizingira nyumba ya Simon Matheri Ikere iliyokuwa katika eneo la Athi River takribani kilomita 30 Kusini, Mashariki mwa jiji la Nairobi.

Katika tukio hilo ambalo lilitawaliwa na kurushiana risasi hatimaye ilibidi Polisi wamuombe mtuhumiwa ajisalimishe kwa kutoka nje ya nyumba yake ili kunusuru maisha ya watu wengine waliokuewa ndani ya nyumba ile. Simon aliamua kujisalimisha.

Wakati anatoka nje ya nyumba yake, Polisi walimshambulia kwa risasi na kumuuwa. Polisi walifanikiwa kumuuwJambazi huyo baada ya kupata taarifa kupitia kwa raia mwema, na kwa kutumia satelaiti walifanikiwa kujua mahali alipo kupitia simu yake ya mkononi, baada ya kupata namba yake ya simu kutoka kwa raia huyo mwema.

Msemaji wa Polisi nchini Kenya Gideon Kipunjatialisema kwamba Matheri alikuwa anatuhumiwa kwa mauaji ya watu zaidi ya 18 miongoni mwao wakiwa ni daktari bingwa wa maradhi ya ukimwi {AIDS} Prof. Job Bwayo ambaye aliuawa mwanzoni mwa mwezi huo huo wa Februari pamoja na mfanyakazi wa kimishenari wa Kimarekani aitwae Lois Andersnna binti yake Zelda White.

Mauaji ya Wamarekani hao yalitokea mnamo Januari 2007 katika tukio la kupora gari ambapo inasemekana Matheri na wenzie ndiyo waliohusika. Kipunjati alikiri kwamba Polisi walikuwa na ushahidi wa kina wa kumhusisha na mauaji hayo.

Naye kamanda mkuu wa Polisi wa jiji la Nairobi Njue Njagi akizungumzia tukio hilo alisema, ‘Leo ni siku kubwa kwa upande wa jeshi la Polisi, kwani tumefanikiwa kumuua jambazi sugu aliyekuwa akilisumbua jeshi la Polisi kwa muda mrefu.

Kamanda Njagi aliendelea kusema, ‘Mtu huyu alichukulia kuuwa kama kitu cha kufurahisha [hobby} lakini kwa uwezo wa Mungu leo polisi tumeweza kuzima vitendo vyake.’ Kmanda huyo aliendelea kubainisha kwamba Jeshi la Polisi bado linaendelea kuwasaka majambazi wengine watano ambao ni washirika wakuu wa Matheri.

Polisi wa nchini Kenya wanaamini kwamba Matheri alikuwa akiongoza genge la majambazi ambalo lilikuwa likiendesha uharamia katika miji mikuu ya Afrika Mahsriki, ambapo wakazi wa miji hiyo kwa muda mrefu wamekuwa majeruhi wa vitendo vya ujambazi vilivyokuwa vikiendeshwa na Matheri pamoja na genge lake.

Baada ya kumuuwa Matheri Polisi katika upekuzi walioufanya katika nyumba yake walikuta bunduki aina ya AK-47 pamoja na risasi 26. Hata hivyo upo utata uliojitokeza katika taarifa zilizonukuliwa kutoka pande mbili, yaani upande wa Polisi na mke wa Matheri kwa upande mwingine

Ni utata gani huo, fuatilia kisa hiki kesho…………..

Oct 29, 2009

NIKAONA MAITI ZAO, SEHEMU YA MWISHO

ILIPOISHIA……………………..
Nilikata kipande kile cha gazeti la kingereza kilichokuwa na habari ile. Nilichukuwa kipande hico na kukiwekamkwenye nDiary yangu. Deni, Ningelipa vipideni la watu? Nilijikuta nikipiga magoti na kuomba. Mungu alipe uwezo wa kuja kulilipa deni la mtu yule mwema. Kwa njia yoyote. Mungu naomba uje uniwezeshe kulilipa kwa sura na namna ujuavyo wewe. Nataka kulilipa deni ili nami niwe nimemfanyia jambo marehemu , niliomba. Nilirejea Dar siku hiyo hiyo

ENDELEA…………….

Kwa sababu ya mambo mengi na hasa baada ya matokeo ya usaili ule kuwa mbaya kwangu, nilijikuta nikiwa na mambo mengi na kusahau haraka sana kuhusu mtu yule aliyenisaidia mbaye ni marehemu. Nilifanikiwea hata hivyo kupata nafasi ya kusoma Chuo cha Saruji na baasae chuo cha ufundi na hatimaye nilibahatika kwenda nchini Uingereza. Mwaka 1991 nilianza shughuli zangu.

Ilikuwa ni mwaka 1995 nikiwa ofisini kwangu pale lilipokuwa jengo Nasaco ambalo liliungua mwaka 1996, ambapo lilijengwa upya na kubadilishwa jina na kuitwa Water Front. Nikiwa nafanya kazi zangu niliambiwa na sekratari wangu kwamba kulikuwa na kijana aliyekuwa anaytaka kuniona. Nilimuuliza ni kijana gani, akasema hamjui. Nilimwambia amruhusu aingie. Kina huyo aliingia ofisini. Alikuwa ni kijana mdogo wa umri miaka kama 17 au 18 hivi, mweupe mrefu kidogo. Alikuwa amevaa bora liende , yaani hivyohovyo huku afya yake ikiwa hairidhishi sana.

Nilimkaribisha ilimradi basi tu, kwani niliona atanipotezea bure muda wangu. Nilazima niwe mkweli kwamba sikuwa mtu mwenye huruma sana na nilikuwa naamini sana katika watu wenye pesa au majina. Nilimuuliza “nikusaidie nini kijana na ukifanya haraka nitashukuru maana nina kikao baada ya muda mfupi”. Nilisema na sikuwa na kikao chochote , lakini nilitaka tu aondoke haraka.

“Samahani mzee, nilikuwa na shida…..nimefukuzwa shule na sina tena mtu wakunisaidia kwa sababu …..nime….niko ….kidato cha pili na hivyo tu natafuta tu kama atatokea mtu……..
Nilimkatisha “Sikiliza kijana. Kama huna jambo lingine la kusema, ni bora ukaniacha nifanye kazi. Hivi unafikiri kama nikiamua kumsaidia kila mtu aliyefukuzwa shule si nitarudimkwetu kwa miguu! Nenda Wizara ya Elimu waambie……Kwanza wazazi wako wanafanya kitu gani, kwa nini washindwe …..Kwa nini walikupeleka shule ya kulipia kama hawana uwezo, wanataka sifa?”

“Hapana wazazi wangu walikufa na ninasoma shule ya serikali . Nimekosa mahitaji ya msingi na nauli ya kwendea shule. Nasoma shule ya Kwiro, Morogoro. Shangazi ndiye anayenisomesha, naye ana kansa nahivi sasa hata kazi hafanyi….,” Alianza kulia.
Huruma Fulani ilinijia na nilijiambia, kama ni nauli tu na matumizi, kwa nini nisiwe mwema, angalau kwa mara moja tu. “Baba na mama walifariki lini?” Niliuliza nikijua kwamba, watakuwa wamekufa kwa ukimwi, maana kipindi kile ndipo fasheni ya ukimwi ilipoanza, ambapo kila anayekufa huhesabiwa kwamba kafa kwa ukimwi.

“Walikufa kwa ajali nilipokuwa mdogo sana, nilipokuwa na miaka mitatu. Ndio shangazi yangu akanichukua na kunilea hadi sasa anakufa kwa kansa.” Yule kijana lailia zaidi. Naomba nikwambie wewe msomaji unayesoma hapa kwamba, kuna nguvu fulani na sasa naamini kwamba ziko nyingi ambazo huwa zinaobgoza maisha yetu bila sisi kujua.

Kitu Fulani kilinipiga akinini paaa! Nilijikuta namuuliza yuel kijana “Kwa nini umeamua kuja kwangu, ni nani alikuelekeza hapa na wazazi wako walikufa mwaka gani na wapi?”
Yule kijana alisema, “Nimeona nijaribu tu kwa mtu yeyote ambaye anaweza kunisaidia, na ndio nimejikuta nikiingia hapa, sijui……..sikutumwa na mtu. Wazazi wangu walikufa mwaka 1979 huko Same na mimi wanasema nilikuwa kwenye ajali, nikaokoka. Niliumia tu hapa. Alishika kwenye kovu juu ya paji lake la uso.

Nilihisi kitu fulani kikipanda tumboni na kuja kifuani halafi niliona kama vile nimebanwa na kushindwa kupumua. “Baba yako alikuwa anaitwa nani?” “Alikuwa anaitwa Siame….Cosmas Siame….” Niliinuka ghafla hadi yule kijana laishtuka . Nilikwenda kwenye kabati langu mle ofisini na kuchakura kwenye droo moja na kutoka na diary. Mikono ikinitetemeka, nilitoa kipande cha gazeti ndani ya diary hiyo, nilichokuwa nimekihifadhi.

“Ndio alikuwa anaitwa Cosmas Siame. Huyu ni mtoto wake, ni yule mtomto aliyenusurika.” Nilinong’ona. Nilijikuta nikipiga magoti na kusali. “Mungu, wewe ni mweza na hakuna kinachokushinda. Nimeamini baba kwamba kila jema tunalofanya ni akiba yetu ya kesho na kesho hiyo huanzia hapa duniani.” Halafu nillinyamaza na kulia sana. Nililia kwa furaha na ugundiuzi wa nguvu zinazomgusa binadamu kwa kila nalofanya.

Nilisimama nikiwa nimesawajika kabisa. Nilihisi kuwa mtu mwingine kabisa. Nilimfuata yule kijana na kumkumbatia huku nikiwa bado ninalia. “Mimi ni baba yako mdogo, ndiye nitakyekulea sasa. Ni zamu yangu sasa kukulea hadi mwisho” Naye alilia bila kujua sababu na alikuwa amechanganyikiwa kabisa. Nilirudi kwenye kiti na kumsimulia kilichotokea miaka 17 iliyopita.

Tuliondoka hapo na kwenda kumwona shangazi yake Ubungo, eneo la maziwa ambako alikuwa ampapanga chumba. Kutokana na hali yake nilimhamishia kwangu, baada ya kumsimulia kilichotokea. Huyo dada yake Cosmas alifurahi sana hadi akashindwa kuzungumza kwa saa nzima. Alifariki hata hivyo mwaka mmoja baadae, lakini akiwa ameridhika sana.

Kijana Siame alisona na kumaliza Chuo Kikuu na hivi sasa yuko nchini Australia anakofanya kazi. Ukweli ni kwamba ni mwanangu kabisa sasa. Naamini huko waliko Mbinguni wazazi wake wanafurahia kile walichokipanda miaka mingisana nyuma. Lakini nami najiuliza bado. Ilikuwaje Cosmas akanipa msaada ule? Halafu najiuliza ni kitu gani kilimvuta mwanae Siame hadi ofisini kwanguakizipita ofisi nyingine zote? Nataka nikuambie, usiwe mbishi sana bila sababu, kuna nguvu za ziada zinazoongoza matokeo maishani mwetu…………
*************MWISHO********************
Habari hii iliwahi kuandikwa katika gazeti la jitambue.

Oct 24, 2009

NIKAONA MAITI ZAO!

Ø Kumbe ni mtu na mkewe walionipa shilingi 90 punde tu!
Ø Nikasau kwamba nilikuwa na deni , nikaendelea na maisha
Ø Miaka 17 baadae nikiwa ofisini nikapata mgeni wa ajabu

Ni siku nyingi kidogo, mwaka 1979, lakini ni tukio ambalo liliniuma sana. Ilikuwa vigumu sana kulisahau na lilinifanya nijiulize, inakuwaje Mungu anakuwa mkatili kiasi kile. Lakini bila shaka ilikuwa ni wakati ule wa ufahamu mdogo. Hivi sasa ninafahamu mengi na hasa baada ya kujifunza maarifa haya ya utambuzi.

Ilikuwa ni mwaka 1979 nikiwa nasafiri kutokea Dar es salaam kwenda Arusha. Sijui ilikuwaje, lakini ilitokea. Tuliondoka Dar es salaam saa 12.30 jioni. Wakati ule mabasi yalikuwa yalikuwa yakisafiri jioni na usiku, sio kakma siku hizi.

Nilikuwa ninakwenda Arusha kwenye usaili kwa ajili ya ajira, nikiwa ndio kwanza nimemaliza kidato cha nne. Niliajiriwa moja kwa moja serikalini, kwani siku zile ajira zilikuwa ni za kumwaga. Hata hivyo sikuridhishwa na kazi niliyokuwa nafanya, hivyo niliomba kazi kwenye kampuni moja kule Arusha na niliitwa kwa usaili.

Tulifika mji unaoitwa Korogwe ambao wakati ule ulikuwa ndio mji maarufu kwa hoteli zake katika barabara yote ya Segera hadi Moshi na Arusha. Tulipofika Korogwe basi letu lilisimama kwa ajili ya abiria kupata chakula. Niliingia kwenye hoteli moja ambayo nakumbuka hadi leo kwamba ilikuwa ikiitwa Bamboo. Niliagiza chakula na kula haraka kutokana na muda mfupi wa kula uliotolewa na wenye basi la TTBS ambalo ndilo nililosafiri nalo.

Wakati wa kulipa ndipo niliposhangaa na kuogopa. Niliingiza mkono mifukoni na kukuta kwamba sikuwa na hela. Nilianza kubabaika na mwenye hoteli alisema hawezi kukubali ujinga huo, "Abiria wengine wahuni bwana, anakula na kujifanya kaibiwa, ukikubaliana nao kila siku hasara tu" Mwenye hoteli alisema kwa kudhamiria hasa.

Kulizuka zogo kubwa, huku mwenye hoteli akisema ni lazima anipeleke polisi. Ni kweli alimtuma mmoja wa watumishi wake kwenda kituo cha polisi ili nishughulikiwe……

Hapo Hotelini kulikuwa na bwana mmoja naliyekuwa amekaa pembeni na mkewe na watoto wao wakila. Yule bwana alipoona vile alimtuma mhudumu mmoja aniite. Niliondoka pale kaunta nilipokuwa nabembeleza na kuja kwa yule bwana.

Alikuwa ni kijana mtu mzima kidogo, mwenye miaka kama 50 hivi. Nilimsalimia na aliitikia, nilimsalimia mkewe pia. Yule bwana aliniuliza kisa cha vurugu ile na nilimsimulia. Aliniuliza sasa huko Arusha ningeishi vipi wakati wa usaili wakati nimeibiwa fedha zote na ningerudi vipi Dar. Nilimwambia nilikuwa napanga namna ya kurudi Dar, kama huko polisi ningeaminika.

Kama mzaha vile yule bwana aliniambia kuwa angenipa fedha za kutumia huko Arusha na nikirudi Dar nimrudishie fedha zake. Nakumbuka alinipa shilingi 90 kwa ahadi kwamba nikirudi Dar nimpelekee fedha zake ofisini kwake. Alinielekeza ofisini kwake, mtaa wa Nkuruma na kuniambia kuwa ameamua kunisaidia kwa sababu kila binadamu anahitaji msaada wa mwingine na maisha haya ni mzunguko. Nilimshukuru na kuondoka kukimbilia basini. Basi lilikuwa linanisubiri mimi tu. Nilipanda ndani ya basi na abiria wengine walinipa pole. Tuliondoka Korogwe, lakini haikuchukua muda basi letu lilipata tatizo la pancha ya gurudumu moja la mbele. Ilibidi tuegeshe pembeni ili litengenezwe.
Baada ya matengenezo, tuliondoka kuendelea na safari yetu.

Karibu na mji wa Same kwenye saa saba usiku, basi letu lilisimama ghafla. Abiria walisimama ndani ya basi na kulizuka aina ya kusukumana. Huko nje kulikuwa na ajali. Abiria tulishuka haraka na wengine huko chini walishaanza kupiga mayowe, hasa wanawake. Niliposhuka niliona gari ndogo nyeusi ikiwa imebondeka sana na hapo kando kulikuwa na maiti wawili.

Nilijua ni maiti kwa sababu walikuwa wamefunikwa gubigubi. Halafu kulikuwa na katoto kalikokuwa kanalia sana kakiwa kamefungwa kanga kichwani. Tumwahishe huyu mtoto hapo Same hospitali ameumia, ingawa sio sana. Nilikatazama kale katoto ka kiume kenye umri wa miaka kama mitatu. Kalikuwa kameumie kwenye paji la uso, lakini kalikuwa hai. Bila shaka wale walikuwa ni wazazi wake, kalikuwa yatima tayari. Machozi yalinitoka.

Baada ya kupata msaada na askari wa usalama barabarani kuchukua maiti wale tulipanda basini kuendelea na safari yetu. Kale katoto kalichukuliwa na jamaa fulani waliokuwa na Land Rover ya serikali kukimbizwa hospitalini. Ndani ya Basi mazungumzo yalikuwa ni kuhusu ajali ile tu, hadi tunafika Arusha. Tulichelewa sana kufika Arusha kwani tulifika kwenye saa tano asubuhi, badala ya saa mbili .

Nililala kwenye hoteli rahisi na kufanya usaili kesho yake. Ni hiyu kesho, baada ya usaili niliponunua gazeti ambapo nilipata mshtuko mkubwa ajabu. Kumbe wale watu wawili waliokufa kwenye ajali ile ya Same walikuwa ni yule bwana aliyenisaidia hela na mkewe. Yule mtoto wao ndiye aliyeokoka. Niligundua hilo baada ya kusoma jina lake na jina la kampuni aliponiambia nimpelekee fedha zake nikirudi Dar, pamoja na picha yake, mke na mtoto. Nililia sana, kama mtoto.

Nillishindwa kujua ni kwa nini afe. Nilijiuliza ni nani sasa angemlea mtoto yule? Yalikuwa ni maswali yasiyo na majibu na pengine maswali ya kijinga pia.
Nilijua kwamba nilikuwa na deni, deni la shilingi tisini. Kwa wakati ule shilingi tisini zilikuwa ni sawa na shilingi laki moja za sasa.
Kwa mara ya kwanza sasa nilijiuliza ni kwa nini marehemu yule aliniamini nakuamua kunipa fedha zile. Sikupata jibu.

Nilikata kipande kile cha gazeti la kingereza kilichokuwa na habari ile. Nilichukuwa kipande hicho na kukiweka kwenye Diary yangu. Deni, Ningelipa vipi deni la watu? Nilijikuta nikipiga magoti na kuomba mungu anipe uwezo wa kuja kulilipa deni la mtu yule mwema kwa njia yoyote. 'Mungu naomba uje uniwezeshe kulilipa deni la marehemu kwa sura na namna ujuavyo wewe. Nataka kulilipa deni hili ili nami niwe nimemfanyia jambo marehemu,' niliomba. Nilirejea Dar siku hiyo hiyo.

FUATILIA MKASA HUU WA KUHUZUNISHA..............

Oct 20, 2009

NI NGUVU ZINAZOONGOZA MAISHA YETU!

Mimi ni muumini wa nguvu za kimaumbile. Naamini kwamba kila kinachopandwa, hatimaye huvunwa kwa njia ile ile, kama leo hii mtu akitenda wema, ni wazi atavuna wema huo, iwe anataka au hataki. Kwa kawaida maisha yetu yanazingirwa na nguvu tunazopanda wenyewe ingawa hili limekuwa gumu kwetu kueleweka.

Naomba nikupe mfano wa watu ambao huenda unaweza kuwafahamu. Miaka mingi iliyopita, mkulima mmoja kule Uskochi, alikuwa akifanya kazi zake shambani. Ghafla alisikia kelele kutoka bondeni .

Mkulima huyo, bwana Fleming alikimbilia huko bondeni kuona kulikoni. Kufika huko, alikuta kuna kijana mmoja ambaye alikuwa anazama kwenye tope.

Kumbuka kwa wenzetu, kuna maeneo ambayo mtu anaweza kukanyaga na kujikuta akizama pole pole hadi kumezwa kabisa na tope na kufa. Mkulima huyu alijitahidi hadi akamwokoa kijana huyo.

Kwa kawaida wakulia wengi hawakuwa tayari kuhatarisha maisha yao, kuokoa mtu ambaye anazama. Kwanza, hadi mtu kufikia mtu kuzama shambani kwako maana yake ni kuwa aliingia eneo lako bila idhini. Lakini, kumwokoa mtu ingekuwa ni sawa na mtu anayeokoa kujiweka katika hatari ya kufa pia. Lakini mkulima huyu alijali zaidi utu wa yule aliyekuwa anaomba msaada.

Kesho yake asubuhi, mkulima yule alishangaa kuona mkokoteni wa farasi umefika nyumbani kwake. Mikokoteni hii ilikuwa ikimilikiwa na watu wenye uwezo au kutoka koo ya kifalme. Mgeni huyu alikuwa ameongozana na yule kijana aliyeokolewa. Mtu aliyekuwa na mkokoteni ule, ambao kwa sasa tungesema Benz ile, alijitambulisha.

Huyu alikuwa ni baba wa yule kijana aliyeokolewa na mkulima yule. Huyu mgeni aliuliza, 'wewe ndiye ndiye uliyemwokoa mwanangu jana? Ninashukuru sana kwa hilo. Nimekuja kukulipa kwa wema wako.' Mkulima Fleming alisema kwamba, hahitaji kulipwa chochote kwa kile alichofanya.

Wakati huo mtoto wa mkulima yule ambaye alikuwa makamu mamoja na kijana aliyeokolewa, alijitokeza kutoka ndani. Yule mgeni aliuliza, 'Huyu ni mwanao,' Yule mkulima alijibu kwa kujidai, akisema, 'ndiyo.' Yule mgeni alisema, 'naomba nimsomeshe kwa kadiri ambavyo ningemsomesha mwanangu.'

Halafu aliendelea, 'Kama ni mtoto ambaye atakuwa na moyo kama wa baba yake, basi atasaidia watu wengi sana na atafanya dunia kuwa mahali bora zaidi.' Mkulima alikubali ofa ile ya mwanae kusomeshwa. Kwa hiyo, kijana akawa amepata mfadhili mwenye fedha kumsomesha kutokana na wema wa baba yake.

Ni kweli, mgeni alimsomesha kijana huyu hadi kiwango cha juu kabisa cha elimu, kwenye shule bora kabisa za wakati ule. Kijana huyu alikuja kusomea udaktari kwenye chuo ambacho kilifahamika kama, St. Mary' Hospital Medical School, kilichopo London, Uingereza. Maana yake ni kwamba alikuwa ni Daktari.

Huyu kijana ni mtu maarufu sana hapa Duniani. Kwa nini? Ni kwa sababu, ndiye mtu aliyegundua dawa aina ya Penicillin. Huyu si mwingine, bali ni Sir Alexander Fleming.

Baada ta kumaliza masomo yake na kugundua dawa hiyo, kilitokea kisa kingine. Yule kijana aliyeokolewa kuzama topeni na yule mkulima, alipatwa na maradhi ya homa ya mapafu {Pneumonia}. Kilichookoa maisha yake kilikuwa ni dawa ya Penicillin ambayo iligunduliwa na mtu aliyesomeshwa na baba yake, katika kulipa shukrani ya msaada uliotolewa kwa mwanae.

Naomba nikwambie kwamba yule Tajiri hakuwa mwingine bali Lord Randolph Churchill, ambaye ni baba wa mtu aliyekuja kuwa maarufu sana duniani kwa uongozi na hekima yake, Sir Winston Churchill. Huyu bwana ndiye aliyeokolewa kule kwenye tope na kuja kuokolewa tena na Penicillin. Umeelewa?

Je, wakati mkulima yule anamwokoa kijana yule, bila masharti au kinyongo, alikuwa anategemea kupata kitu gani kutoka kwake au kwa baba yake, ambaye wala hakuwa akimjua? Hakuwa anategema chochote, bali alitenda wema tu. Tunapotenda wema huwa hatutarajii kulipwa.

Lakini tunapotenda wema, ni kwa namna gani tunaingia kwenye mfumo wa nguvu za kimaumbile? Naomba nitumie habari hii kukufahamisha. Kila jambo jema au baya tunalotenda linatuweka mahali ambapo tunaingia kwenye njia ya nguvu inayoendesha mambo ulimwenguni. Hatuna haja ya kuhangaika kujua, tumeingia katika nguvu gani, kwani tujue au tusijue, tutaingia tu.

Kwa mfano mkulima alimwokoa kijana, badala ya kusema , 'ngoja life, kwa nini hayasikii yakiambiwa yasiingie kwenye maeneo ya watu?' Kumwokoa kwake kulifanya baba wa kijana huyu kutaka kulipa fadhila. Mkulima alikataa malipo mengine yote, bali 'ofa' ya mwanae kusomeshwa . Kumbuka , mkulima kwa njaa yake angekubali hela haraka sana, lakini alikataa.

Kwa kukataa kuuza ule wema aliotenda kwa kijana akawa ameingia kwenye nguvu chanya zaidi. Kukataa huko kulizua tajiri kutaka kumsomesha mwanaye. Kama angekubali fedha, huenda mwanae asingekuja kusoma na kuwa daktari maarufu duniani na mgunduzi wa dawa iliyookoa maisha ya mamilioni ya watu.

Huyu tajiri, naye ameamua kulipa fadhila ambayo ni nguvu chanya. Pale mkulima alipokataa kupokea zawadi ya fedha, yule tajiri bado aliona atajisikia vizuri kumtendea jema mkulima. Alimwona kijana wake na akaona kumsomesha katika kiwango cha juu lingekuwa jambo ambalo lingempa ridhiko. Alifanya hivyo, na hiyo fadhila yake, ndiyo ambayo inakuja tena baadae kumwokoa mwanae.


Habari hii iliwahi kuandikwa katika Gazeti la Jitambue........

Oct 18, 2009

KINDUMBWENDUMBWE CHA MAISHA!!! SEHEMU YA MWISHO.....

Nilianza kuipata picha na niliojua kwamba yule mke wa mwenyeji wangu hakuwa akitaka yule binti kuishi nao, kwa sababu zake. Alikuwa akifanya mambo na kumsingizia yule binti. Nilijiambia kwamba siku ya kuondoka pale ningemambia yule jamaa kuhusu ile redio. Lakini ingesaidia chochote?

Kesho yake jumapili nyumba nzima ilijianda kwenda kanisani, isipokuwa yule binti ambaye niliambiwa kwamba anaitwa Patience. Huyu aliachwa kwa ajili yakupika chakula cha familia. Niliona bila shaka ule ungekuwa muda mzuri kwangu kuzungumza na binti yule. Walipoondoka wote nilimfuata Patience jikoni na kumwomba nimsumbue wakati anapika kwa kuzungumza naye.Alisema wala simsumbui. “Nitashukuru maan sina mtu ninayezungumza naye humu. Wote wananidharau hadi huyu dada anayesaidia kazi” Alisema.

Nilimwambia ninaelewa, nimeona na nilimpa pole. Nilimuuliza kama ni kweli anaibana ni mbeya na anafanya tabia chafu za kihuni. Yule binti alibadiliaka ghafla na kusema, “Yqaani wameshakwambia niko hivyo, sasa mimi nimemkosea nini mjomba na familia yake” Akianza kulia, nilijisikia vibaya na kujilaumu kwa kumwambia vile. “Patience, nisikilize. Hebu nichukulie mimi kama baba yako. Naomba utulie unisikilize, kw sababu siamini hata jambo moja waliloniambia” Patience aliacha kulia na kunitazama sana hadi nikaogopa. “unasemaji?” Nilijikuta namuuliza. “hapana” alisema akijifuta machozi. Kwa kweli nilipokuw nikimtizama nilishinda kujua kama nilikuwa ninampenda, ninamwogopa, ninamwonea aibu au ninamfananisha. Ili mradi tu nilishindwa kuelewa.

Nilijisikia vibaya kuwa katika hali hiyo, lakini sikuweza kujizuia. “samahani, mama na wewe mlikuwa manishi wapi kabla hajafariki? Nilimuuliza. Alinitazama tena kama awali. “Tulikuwa tunaishi Arusha” Nilitaka kujua vitru fulani ili niamue kama ningeweza kumsaidia kumpata baba yake.

Lakini nilikuwa naogopa, maswali mengine huenda yangemkera.

“Mama yako alikwambia baba yako alikuwa anaitwa nani?” Yule binti alishika vidole vyake na kuchezesha miguu kwa muda kabla hajasema, “kama jina lako” nilijua alikuwa akinitania au alitaka kutumia mbinu ili niondoke naye. Ningeweza hata kufanya hilo kwa sababu kwa maisha kama yale ni wazi angeharibikiwa.
“Kwanza wewe unajua jina langu?” Niliuliza kwa mzaha. “ nalijua, si nilimsikia mjomba akisema akimwambia shangazi, Mr……….akija atatumia chumba cha kwanza. Alisema na nilianza kuingiwa na wasi wasi.

Alilotaja ni jina la ukoo, hivyo niliona niendelee na maswali, nikijua labda binti yule angekuwa ni mtoto wa ndugu yangu “Jina la kwanza na baba yako alikwambia ni nani?” Nilimuuliza. “Alinitajia, nimelisahau, alikuwa akipenda kutaja hilo la pili” Binti alisema.

Halafu alisema, “ Ninayo picha yake alipiga na mama, mnafanana naye kidogo. Ngoja nikaichukue .” aliondoka na kwenda huko chumbani kwake. Alikuwa akilala, kwenye kijichumba ambacho nadhani kilikuwa hasa ni stoo karibu na choo cha jumla cha mle ndani.

Nilijua ni mzaha mwingine, lakini nilitaka kumjua huyo mama na baba yake. Alirudi baada ya dakika kumi, bila shaka hiyo picha ilifichwa mbali sana. Alinipa picha hiyo na niliipokea kwa shauku kubwa. Nilitegemea kumwona ndugu yangu au mtu yeyote ninayemfahamu. Sikumwona yeyote kati ya hao ninaowafahamu. Ilikuwa ni picha ya mwanamke ambaye nilikutana naye kwenye semina ya maziwa, pale Shirika la Elimu kibaha mwaka 1981.

“Germana!” Nilinong’ona. Nilihisi nikiloa jasho mwili mzima na kwa muda fulani sikujua hasa nilipokuwa. Nilijikuta nikikaa kweky kiti hapo jikoni. Ni kama ndoto, ni ka hadithi, ni ka sinema fulani.
Nakwambia ukweli sijawahi kuhisi hali ile maishani na sijui kama nitakuja kuhisi, maana nashindwa hata kukueleza.
Yule binti alinishika na kunitazama machoni, “Unamjua mareehemu mama?” Alniuliza na sikuweza kumjibu. Nilitembe na mwanamke huyu ambaye ndio najua kwamba ni marehemu, siku moja tu kwenye semina ile. Hakuna aliyekumbuka kuchukua taaarifa kamili za mwenzake, kwa kuzingatia kwamba hatukuwa waajiriwa na tulikuwa ndio tuaanza maisha, vijana tunaochemka. Mambo ya semina, kutenda na kusahau.

“Kumbe Germana alizaa aliza mtoto mzuri hivi, mtoto wangu. Damu yangu inateswa na kudhalilishwa hivi”. Niliinama na kuanza kulia. Halafu niliinua kichwa na yule binti alikuwa akibubujikwa na machozi pia.
“Mi-mi, mimi ni baba yako Patience. Nisamehe, tusa-tusamehe sana halikuwa kosa letu……sikuweza kuendelea.

Waliporudi kanisani walishngaa kukuta tukiwa na Patience kule chumbani mwangu tukiongea na kucheka sana. Yule mke wa mwenyeji wangu ambaye sasa ni shemeji yangu alimwita Patience kwa nguvu na kisirani.

“Umeanza siyo? Unataka kumvuruga huyo baba wa watu, kisa?”
“Yaani wewe mtoto nitakuuwa tu, lazima” Nilimambia Patience akae kwanza hapo chumbani. Nilitoka mimi na kumfuata mke wa jamaa yangu, “Hapana dada, ni mimi nilimwita”

halafu nilimwita mwenyeji wangu aliyekuwa akitokea chumbani mwake kuja sebuleni.
Alipokuja nilimkabidhi ile picha niliyopiga na dada yake, alipoichukuwa aliitizama na kunitizama, aliitizama tena na kunitizama. Halafu alikwenda kukaa kwenye kochi na kushusha pumzi kwa nguvu.

“Naomba radhi, mimi ni baba wa mtoto Patience. Nimeamini kilichonileta huku Tanga siyo hii kazi yako bali ni nguvu ya damu yangu…..Mke wamwenyeji wangu aliingilia kati. “Ni kitu gani?”
Niliwasimulia kila kitu.

Sitaki kukuchosha. Hivi sasa Patience anasubiri kujiunga na masomo chuo kikuu baada ya kufaulu vizuri mtihani wake wa kidato cha sita. Amechelewa kusoma, ndiyo, lakini anataka kusoma na anamudu. Kumbuka jambo moja, Kila binadamu unayemtendea jambo baya, unaitendea damu yako jambo baya bila kujua. Kila binadamu unayemtendea jema, unaitendea jema damu yako bila kujua.

Sisemi kwa ubaya, lakini yule mke wa rafiki yangu alifariki mwaka 2001 kwa ugonjwa ambao inadaiwa kwamba ni ukimwi. Hali ya uchumi ya mumewa inatisha sana. Tazama naye yule mama marehemu aliacha watoto watatu. Je huko alipo atajisikia vipi watoto wake leo wakitendwa kama alivyokuwa akimtenda Patience? Kwani kuwapenda wengine gharama yake ni kiasi gani?

Je sisi wanaume tuna watoto wangapi huko nje ambao hatuwajuiwala kuwatambua? Lakini ni mara ngapi tunatamani na kuwafanya watoto hao kuwa wapenzi wetu?
Hatuoni tunafanya mapenzi na damu zetu?

*************************MWISHO***************************

Oct 17, 2009

KINDUMBWENDUMBWE CHA MAISHA!!!

  • Ilikuwa ni siku moja Kibaha na mimba ikatungwa sawia.
  • Mama akaiba redio nikimwona, asubuhi akasema ni binti.
  • Picha ikaletwa kimzaha, lakini hali ikabadilika ghafla sana.........................


    Nilikaa na wale jamaa kwa siku tatu tu, lakini niliona mambo ambayo binadamu anaposimuliwa anaweza kudhani kwamba kuna dhihaka anayotakiwa kufanyiwa, yaani haiwezekani.

    Niliondoka Dar Es Salaam siku ya ijumaa kwenda Tanga. Nakumbuka ilikuwa ni August mwaka 1995. Nilikuwa nakwenda kwa jamaa ambaye aliniita kwake kwenda kumsaidia kukagua shughuli fulani ambazo alitaka kuzifanya. Wakati ule nilikuwa najitegemea, nilikuwa sijaingia serikalini kiajira.

    Nilifika mjini Tanga na kumkuta mwenyeji wangu na mkewe wakiwa kituo cha basi wakinisubiri. Tulisalimiana na walisema wamefurahi kunifahamu nami nilisema nimefurahi kuwafahamu. Ilikuwa ni mara yetu ya kwanza kukutana. Walipewa jina na mawasiliano yangu na jamaa yangu mmoja.

    Nilifika nao nyumbani kwao na kukaribishwa vizuri sana. Walikuwa wakiishi Raskazoni. Ilikuwa ni nyumba ya kifahari kwa kweli. Lakini nilibaini kwamba mama au mke wa yule mwenyeji wangu ndiye aliyekuwa na kauli pale nyumbani. Kwa kipindi cha saa moja tu tangu kufika nilipata picha hiyo bila matatizo.

    Wakati wa kula chakula cha usiku, nilitambulishwa kwa watu wa nyumba ile. Haikuwa nyumba ya watu wengi. Kulikuwa na watoto watatu wa yule mwenyeji wangu. Mkubwa alikuwa wa kiume aliyekuwa na umri kama miaka tisa, wa pili wa kike na wa tatu wa kike pia. Halafu kulikuwa na ndugu wa kiume wa mwanamke, kijana ambaye alikuwa ndio kwanza amemaliza kidato cha nne.

    Halafu kulikuwa na msichana wa kumsaidia kazi za ndani au house girl kama wanavyoitwa. Hawa wote nilitambulishwa kwao hapo mezani wakati wa kula. Lakini wakati tunakaribia kumaliza kula msichana mwingine mwembamba mweusi alikuja pale mezani na kukaa kitini, karibu wote tulikuwa tumeshashiba.

    Alianza kujipakulia chakula bila kusema neno. Ilikuwa inaonesha kwamba alikuwa ametoka kufanya kazi kwenye sehemu yenye maji kwani gauni lake lilikuwa na majimaji.
    Nilijua ni msaidizi wa ndani pia. Lakini niliona kwamba sio haki kumtendea vile , yaani kumwacha afanye kazi wakati wengine wanakula . lakini sikuwa nimeenda pale kwa sababu ya upelelezi.

    Nilianza kazi yangu iliyonipeleka pale usiku ule. Nilipewa chumba kilicho karibu kabisa na sebule, ilikuwa nifanye kazi ya kupitia mafaili kadhaa kabla sijaandika tarifa yangu ya kuwasaidia wale jamaa kupata walichokuwa wanahitaji. Naomba nisiseme ni kazi gani hasa. Kwa hiyo nilikuwa nimepania kufanya kazi hadi usiku mkubwa sana kama sio alfajiri.Nilianza kazi kwenye saa nne, nikimwacha mwenyeji wangu na familia yake hapo sebuleni, wakiangalia televisheni. Ilipofika saa sita usiku nilihisi kiu. Niliamua kuvumilia, lakini kiu ilinizidi na niliamua kwamba ningekwenda tu jikoni kutafuta maji ya kunywa.
    Nilitoka chumbani mwangu na kuelekea jikoni ambako bado kulikuwa na taa iliyokuwa ikiwaka. Nilipofika jikoni nilishangaa kukuta kukiwa na mtu. Alikuwa ni yule msichana ambaye sikutambulishwa kwake. Alikuwa anamalizia kuosha vyombo ilikuwa inakimbilia kwenye saa sita na nusu usiku.

    “Pole sana, naomba maji ya kunywa, samahani.” Yule binti aliitika kwa kusema “sawa baba”, huku akiinama kwa heshima. Aliniletea chupa ya maji kutoka kwenye jokofu. “Hapana, napenda ya moto, kama yapo” nilimwambia. Aliitikia kwamba yapo na kunichukulia chupa mezani hapo jikoni nilimwangalia na kugundua kwamba alikuwa analia.

    Kwa kuwa nilishangaa wakati ule wa kula, na hapa saa sita na nusu za usiku mtoto wa miaka 14 au 15 anasafisha vyombo na halafu kule kulia, nilijua kulikuwa na jambo. Nilimuuliza kama analia, na alisema hapana. Nilimwambia, ni usiku na anatakiwa kwenda kulala. Alisema anakwenda kulala.
    Nilikuwa na uhakika alikuwa analia na alikuwa pia anajitahidi kufuta machozi ili nisijua. Kalikuwa ni kasichana kadogo, kazuri sana pamoja na kufujwa kule. Kama ningekuwa kijana bado ni wazi ningeoa msichana wa aina ile. Bahati mbaya zaidi ni kwamba mke wangu alifariki miaka mitano tu nyuma na nilikuwa bado na maumivu. Hisia zile ziliniumiza zaidi.

    Nilirudi kule chumbani nikiwa nimeanza kuingiwa na wasiwasi. Lakini sio wasi wasi tu bali hata huruma. Kwa nini awe yule binti, na kwa nini sikutambulishwa kwake?
    Sikupata jibu

    Sikupata jibu. Ile hali ya kusafisha vyombo hadi saa 6:30 usiku, tena peke yake huku akilia, ilinikera sana, na nilijiambia siondoki pale bila kujua kitu kuhusu binti yule. 8:30 nilisikia kama miguu ya mtu huko sebuleni, nilihisi kwamba angekuwa ni yule binti. Hali hii ilinifanya niwe na hofu kidogo, kwa sababu mawazo yangu yalikwenda kwenye ushirikina hasa kwa kuamini kwangu kwamba, hapo Tanga palikuwa na ushirikina sana.

    Nilizima taa ya chumbani mwangu pole polepole na kuchungulia. Aliyekuwa hapo sebuleni alikuwa ni mke wa yule mwenyeji wangu. Alikuwa amevaa gauni lake la kulalia na alikuwa anachukua kitu juu ya kabati ya sebuleni. Nilivutiwa kutazama zaidi. Niliona akichukua redio fulani ndogo nzuri sana ambayo hata jioni ile niliiona na kuitamani.

    Bila shaka kwa shughuli za yule mwenyeji wangu, kuwa na vitu kama redio ya aina ile lingekuwa ni jambo la kawaida. Yule mama aliichukua redio ile na kuitia kwenye mkoba wake mkubwa wa kike na aliuweka mkoba huo kwenye kabati nyingine ndogo pale sebuleni. Halafu aligeuza na kurudi chumbani mwake.

    Nilirejea chumbani mwangu nikijiuliza ni kitu gani hicho. Nilishindwa kujua yule mama alitaka kuipeleka wapi ile redio, na kwa nini aliiweka kwenye mkoba wake, usiku kama ule. Sikuweza kupata jibu , bila shaka hata kama ingekuwa ni wewe ingekuwia vigumu kupata jibu. Niliamua kuendelea na kazi nyangu.

    Kwenye saa kumi kamili usiku nilisikia mtu huko sebuleni. Nilifungua amlango wangu wa chumba na kugundua kwamba ni yule binti. Alikuwa anafanya usafi. Niliwaza. Kulala saa saba na kuamka sa kumi alifajiri! Lakini kwa nini iwe ni yeye tu. Hilo likawa ndilo swali. Niliamua kulala nikiwa nimeumia sana.

    Kwenye saa 12:30 asubuhi nilishtushwa na kelele za kilio cha mtu. Mtu huyo alikuwa akipigwa hapo sebuleni. Nilitaka kurejea kulala, lakini ilikuwa vigumu kwangu kutokana na kipigo na kelele hizo. Niliamua kufungua mlango wa chumba changu na kwenda sebuleni.

    Yule binti wa usiku na alfajiri ambaye nilikuwa sijajua jina lake ndiye aliyekuwa akipigwa. Alikuwa akipigwa na mke wa mwenyeji wangu kwa mkanda. Kutokana na kauli za mama yule na yule binti mwenyewe , ilionekana kuwa alikuwa akituhumiwa kuiba kitu fulani. Mwenyeji wangu na wanaye pamoja na yule house girl walikuwa wakishuhudia kipigo kile kama vile wakiangalia sinema..

    “Shangazi mimi sikuiba,siwezi kuiba, mimi sio mwizi” Yule binti alikuwa akilia kwa maumivu na alikuwa amelala chini akiwa hoi.
    Yule mama aliponiona aliacha kumpiga na aliondoka kwenda chumbani kwake huku akisema, “Nikija jioni nikute redio yangu, ama marehemu mama yako anilipe”
    “Yaani mtoto kila siku wewe tu ndio kisirani ndani ya nyumba. Nimeshamwambia mjombako wewe ni kibwengo na mikosi haitaisha humu ndani……

    Nilijua ni ile redio ambayo yule mama alikuwa ameiweka kwenye mkoba wake ambao bado ulikuwa pale juu kabati ndogo pale sebuleni. Nilijua kwamba, yule binti alikuwa akipigwa kwa kuonewa kabisa.
    Lakini ni mimi tu na yule mama ndio tuliokuwa tunaujua ukweli huo, halafu na mungu.

    Nilimtazama yule binti pale chini alipokuwa amelala kwa maumivu na nilihisi tu machozi yakinidondoka, Ingawa nilikuwa sijajua, yule msichana ni nani pamoja na kwamba likuwa akimwita yule mama shangazi, kwangu alionekana kuwa binti mwenye adabu na hekima pia.

    Baada ya kunywa chai yule mke wa mwenyeji wangu akiwa hayupo , nilimuuliza yule mwenyeji wangu kuhusu yule binti. Aliniambi yule binti ni mtoto wa marehemu dada yake, ambaye alimzaa na mwanaume ambaye mama yake alikuwa anadai kwamba walikutana tu kwa bahati mbaya na hakujua kama alipata ujauzito. Hivyo hakuwa na anuani yake kamili. Huyo dada yake alifariki miaka sita iliyopita akimuacha yule binti na umri wa miaka minane.

    ‘Ndio nikamchukua, lakini kumbe alishaharibika na kwa kweli anatusumbua sana. Ni msichana ambaye hata shule alikataa, alipomaliza tu la saba. Na kazi yake ndio hiyo ya wizi, kama hakuiba redio, simu, saa, deki basi utapata kesi ya umalaya.

    Kama siyo hivyo basi umbeya mtupu. Mtaa wote unapata habari zinazoenda nyumba hii, basi tu sijui inakuwaje, siju ni laana kutoka huko kwa upande wa baba yake…….!

FUATILIA KISA HIKI CHA KWELI KESHO......................

Oct 14, 2009

NJIA YA MAISHA YAKO INAPOFUNGWA GHAFLA, SEHEMU YA MWISHO


Nilitembea asubuhi hiyo hadi hospitalini. Nilikwenda upande wa utawala na kuomba nimwone mama mkubwa. Ilikuwa ni vigumu sana kwa sababu ya watu ambao siku hizi wanitwa ‘wapambe’ Walikuwa wananizuia kwa maelezo kwamba mama mkubwa haonwi hovyo tu. Wakati tunabishana, kwani nami nilikuwa mkali nikiwa sijui nilitoa wapi nguvu hiyo ya kubishana, alitokea mamammoja mzungu aliuliz kulikoni, ambap walimweleza. Alinisogelea na kuniambia nimweleze shida yangu. Sikumwambia kuwa niliota kuhusu mama mkubwa bali nilimsimulia kwa kifupi madhila yangu na kumwambia nilikuwa nataka msaada w kusoma.Alinisikiliza sana na baadae alisemaangepanga nionane na huyo mama mkubwa. Saambili baadae nilikuwa ofisini kwa mama mkubwa. Alikuwa ni mama wa kizungu mtu mzima sana, lakini mjanja na msikivu sana. Nilizungumza naye kwa kirefu nikimweleza kia kitu. Alishindwa kuvumilia kwani alimwaga chozi.
Hapo nikafanikiwa kupata mfadhili wa kunisaidia kusoma. Nilikwenda shuleni na kuendelea na masomo. Nilikuwa ninaishi chini ya uangalizi wa mzee mmoja aliyekuwa anaitwa Alois, ambaye nimeambiw ameshafariki. Nilikuwa nikiishi kwenye chumba kimoja karibu na wodi ya wagonjwa hapo hospitalini. Wale ambao bado wapo hospitalini pale kama watumishi wanakumbuka, bila shaka. Nilimaliza darasa la saba na kuanguka kwa njia ambayo bado ni mshangao kwangu, hadi leo. Mama mkubwa alisikitika sana. Alimwomba Mzee Alois anitafutie shule nirudie. Nilirudia shule nyingine ya jirani. Mwaka mwaka uliofuatia nilifaulu peke yangu shuleni hapo.

Niliendelea na masomo. Bila shaka huhitaji kujua habari za shule ya sekondari. Lakini nilimaliza kidato cha sita mwaka 1987 na kumaliza masomo ya chuo kikuu nchini Uholanzi mwaka 1992. Nilirudi nchini na kuanza kazim kwenye kampuni9 moja ya madini kule shinyanga.

Mwaka 1994 nilikwenda Turiani, lengo likiw ni kwasalimu wote ambao nilikuw nafahamiana nao pamoja na dada yangu. Kwa kweli nilikuw nimemsamehe dada yangu yule kutoka ndani kabisa ya moyo wangu. Niliamua kwa makusudi niende nikashukie kwake. Nilipofika pale nyumbani kwake kulikuwa na mabadiliko sana. Ile nyumba ilikuwa imechakaa karibu kuanguka na palionyesha ukiwa wa wazi. Nilibisha hodi na mama mmoja mtu mzima sana alifumgua mlango kutokea ndania na kusimama mlangoni.
Kwa muda sikuweza kumjua. Lakini htimaye nilijua kuwa ni dada yangu.
‘Dada shikamoo, habari za siku’ nilimsalimia, lakini yule mama pale mlangoni alishindwa kujibu na kwa muda fulani ilionekana kama vile hakuwa anajua kinachoendelea. ‘Marahaba’ Alijibu, lakini ilikuwa ni kwa mazoea tu. ‘Nani mwenzangu, maana na huu uzee nao,’ Alisema akijichekesha.

‘Ni mimi Joseph, mdogo wako Joseph, mtoto wa mzee Richard Mbega wa Sindeni.’ Nilisema kwa kumfafanulia. Nilimwona dada akijishika vizuri pale mlangoni, lakini hakuweza. Alienda chini pole pole na kukaa kati kati ya mlango. Kw muda fulani nilijua alikuwa hajui alipo na kinachoendelea.

Wakati nikiwa najiuliza nifanye nini mama mwingine aliingia kutokea huko nyuma ya nyumba. Nilimtazama lakini sikumfahamu. Yeye alipiga kelele. ‘Kaka Jose jamani, kaka Jose,wala siamini…….’ Ilikuwa zamu yangu kushngaana laijua hilo kwani aliniambia, ‘Ni mimi mpwa wako Msekwa.’ Nilihisi kitu kikilipuka huko moyoni na matumbo yangu yalishikw na kubana ghafla.

Msekwa, alikuwa ni mama mzima, amechakaa na kuchoka kabisa. Kati yetu, yeye angeonekana kuwa mkubwa sana kuliko mimi. ‘Mungu wangu nashukuru nimekukuta…’
Halafu tulimsikia dada yangu akipiga yowe la kilio akidai kwamba hakuwa anajua alichokuwa anakifanya. Akiwa anaongea Kizigua alisema, ‘Mungu wangu mie nifanyeje sasa, naumbuka ….’ Nilimbembeleza, ingawa Msekw alisema nimwache augulie kwa sababu anastahili.

Baada ya kupumzika, nilijua kwamba wale wapwa zangu watatu wengine, aliyekuwa hai ni mmoja tu wa kike. Mmoja alifariki kwa kuajribu kutoa ujauzito na yule wa kiume alikuwa amefariki kwa kunywa sana pombe. Huyu mwingine alikuwa ameolewa na kuachwa na alikuwa eneo linaloitwa Dakawa. Nilikaa Turiani siku tatu na nilimwomba Msekwa tuondoke wote aje Dar ajifunze kozi yoyote. Hapa ninaposimulia makala haya, ni muuguzi siku nyingi. Dada yangu alikataa katakata kuja kwangu kwa aibu.

Inasikitisha hata hivyo kwamba, miezi mitatu tu tangu nilipofika kwake alifariki.Wanasema kila wakati alikuwa akijilaumu kwa yale aliyokuw amenitendeana alianza kujiambia kwamba, hana sababu ya kuishi kwa sababu hana maana. Naamini tunapanda nguvu hasi na huja kuturudia wenyewe.

Tulienda kuzika na kurejea Dar. Juhudi yangu yote ilikuwa ni kumpata yule shemeji yangu, iwe yuko hai au kaburi lake lilipo ili angalau nilijengee kama zawadi yangu kwake. Lakini juhudi zangu ziligonga ukuta kwa kadiri nilivyojitahidi. Nilikwenda hadi TPC, Moshi lakini sikumpata.

Hata hivyo hatimaye nilimpata katika mazingira ambayo sitaweza kuyasimulia hapa.
Naamini kwa simulizi hii, kuna jambo ambalo umejifunza. Katika maisha haya tunayoishi ni vyema tukawa tunapanda mbegu chanya na sio hasi, kwani kwa kupanda kwetu mbegu hasi, ndio hatimaye huturudia mara tatu zaidi ya kile tulichopanda na maumivu yake kihisia huwa ni makubwa sana. Lakini kama tukipanda mbegu chanya, hakika mavuno yake huwa makubwa kuliko kawaida, hebu jaribu uone.
Jambo lingine ni kusamehe, kusamehe ni muhimu kwetu, hata kama utakuwa umefanyiwa jambo baya kiasi gani. Kwa kusamehe kwetu tunakuwa tumejipa nafuu dhidi ya maumivu ya kihisia pale tukumbukapo juu ya yale tuliyotendewa na wenzetu. Zipo faida nyingi sana tunazopata pale tunaposamehe, lakini kubwa zaidi ni kule kumudu kusahau yale tuliyotendewa na hivyo kuwaza mambo mazuri ya yenye tija katika maisha yetu, badala ya kufikiria mabaya au kulipiza kisasi dhidi wale waliotutendea kinyume na matarajio yetu.

*******MWISHO********
Ndugu wasomaji, habari hii hainihusu mimi binafsi, bali iliwahi kuandikwa katika gazeti la jitambue. Hii ni habari ya kweli kabisa ambayo ilimpata msomaji wa gazeti la Jitambue, ambapo kwa hiyari yake aliamua kuiweka habari ya maisha yake katika gazeti hilo ili wasomaji wapate kujifunza kupitia uzoefu wake. Ukweli ni kwamba, katika gazeti la Jitambue tulikuwa tukiandika ushuhuda mbalimbali kutoka kwa wasomaji wetu ambao walijitolea kuandika historia za maisha yao. Na mimi nimeona sio vibaya nikizirejea baadhi ya stori hizo ili wasomaji wa kibaraza hiki nao waweze kujifunza.

Oct 13, 2009

NJIA YA MAISHA YAKO INAPOFUNGWA GHAFLA, SEHEMU YA PILI


Mwaka 1976 nilianza masomo ya darasa la nne kwenye shule ya msingi Turiani. Kutoka shuleni hadi tulipokuwa tunaishi kwenye kambi za watumishi wa kiwanda cha sukari ni mbali sana, kiasi cha kilomita nane. Nilikuwa natoka asubuhi sana nyumbani nikiwa sijanywa chai na kurejea jioni.

Mwezi wa kwanza tangu kuanza masomo hali ilikuwa mbaya ingawa siyo sana. Kuna wakati nilikuwa ninalala na njaa, hasa zile siku ambazo shemeji yangu alikuwa akiingia usiku. Shemeji yangu alikuwa ni dereva wa magari ya kusomba miwa kutoka mashambani kwenda kiwandani. Kulikuwa na shifti mbili za kazi, usiku na mchana.

Shemeji yangu alikuwa ndiye mlinzi wangu kutoka katika shutuma, kashfa na mateso kutoka kwa dada yangu, ambaye marehemu mama alikuwa akimsema kwa uzuri siku zote. Kwa maana hiyo ni kwamba, nilikuwa nimeweza kwenda shule kwa sababu, shemeji yangu alikuwa upande wangu, niliweza kula na kulala kwa sababu ya shemeji yangu.

Huyu dada alikuwa na watoto wanne, mmoja wa kiume na watatu wa kike. Watoto watatu walikuwa walikuwa wannichukia na kunitendea kama kwamba nilikuwa nimeokotwa na kuletwa pale nyumbani kwao. Mmoja wa kike ambaye alikuwa darasa la pili, ndiye aliyekuwa ananijali na kunihurumia. Kama kweli watoto huchukuwa roho za wazazi wao kama watu wanavyosema, huyu alichukua roho ya baba yake.

Mwezi wa pili tangu kuanza shule, shemeji yangu alipatwa na malaria na kulazwa kwenye hospitali ya misheni inayoitwa Bwagala. Kwa wiki moja aliyolazwa, nilijua hasa maana ya roho mbaya. Ile siku alipolazwa sikula chakula na asubuhi yake nilikuta nguo zangu za shule zimeloweshwa na kutupwa nje. Dada yangu alinipiga sana, akidai kwamba mimi ni mchawi na ninaharibu bure pesa za mume wake, kwani sikuwa na uwezo wa kusoma.

Kama sio jirani mmoja ambaye namkumbuka kwa jina hadi sasa, Richard, kuingilia kipigo kile, naamini ningevunjwa mbavu au eneo fulani la mwili lingedhurika. Watoto wa dada mabo ni wapwa zangu walikuwa wakishangilia wakati napigwa na shule hawakwenda siku hiyo. Niliondoka hapo nyumbani baada ya kipigo hicho hadi hospitalini Bwagala. Nilikuwa mtu wa kwanza kuingia wodi ya wagonjwa siku ile.

Shemeji yangu aliponiona alijua kuna jambo. Sikutaka kumsimulia, lakini aliniomba nimwambie kumetokea kitu gani. Nilimsimulia. Alinitazama kwa muda mrefu sana kabla hajaniuliza, ‘lakini masomo unayaonaje?’ nilimwambia, ninaamini akiendelea kuwepo nitafaulu darasa la saba na kusoma zaidi. Alitabasamu na kuniambia ‘nitakuwepo na utafika mbali, mungu hawezi kukunyang’anya kila kitu.’

Nilimwona akigeukia upande wa pili wa kitanda chake na nina uhakika alilia. Aligeuka tena kunitazama kama baada ya dakika kumi. Aliingiza mkono wake mfukoni kwenye lile pajama la hospitalini alilokuwa amevaa na kutoa kitu. Alinyoosha mkono na kunipa. Zilikuwa ni hela. Sikumbuki zilikuwa ni kiasi gani, ingawa kwa kiwango cha sasa ninaweza kusema zilikuwa ni shilingi 2,000.

Nilisita kuzipokea, lakini macho yake yalinilazimisha kuzipokea. ‘Kafue hizo nguo zako, kesho uende shule. Kumbuka ukitoka shuleni pita pale midizini ule kabisa mghahawani, kabla hujaenda nyumbani. Usimwambie una hela au umekula.’ Aliniambia. Nilimtazama yule mtu pale kitandani na kuanza kulia. Nilishindawa hata kumwambia ‘asante,’ Nilikutana na dada yangu mlangoni wakati naondoka pale wodini. ‘Nyooo, mwanaharamu …..’ Nilimsikia akisema.

Kwa shida shida hivyohivyo nilimaliza darasa la nne na kuingia darasa la tano. Muhula wa kwanza na wa pili wa darasa la nne nilikuwa mtu wa kwanza darasani. Hii ilisaidia na kuniumiza pia. Nilianza kupata marafiki wa nje na nyumbani ambao walikuwa wakinisaidia nilipokuwa na shida kwa sababu walikuwa wakihitaji msaada wangu kimasomo. Lakini kwa nyumbani hali hiyo iliongeza chuki kutoka kwa dada na wapwa zangu. Ni kale kadogo tu, kalikokuwa kanaitwa Msekwa ndiko kalikokuwa kanafurahiya mafanikio yangu.

Shemeji aliamua kuwa na utaratibu wa kunipa senti kumi kila siku kwa ajili ya kula shuleni na ikawa ni siri yangu. Kuna wakati alikuwa akifika shuleni kuulizia maendeleo yangu, nadhani kwa makusudi ili waalimu wajue kwamba alikuwa na mtoto mwenye akili sana. Hii ilitokana na ukweli kwamba, hakuwa anaulizia matokeo ya watoto wake, ambao walikuwa wakishika namba za mwisho mwisho. Lakini bila shaka alikuw akitaka kunipa moyo, kunionesha kwamba kuna mtu anayenijali. Hii ilinipa nguvu sana na nilimchukulia kama baba yangu kabisa. Nilianza kuona uzito wa kumwita shemeji.

Lakini upande wa ndoa yake kulikuwa na tatizo. Kila siku kulikuwa na zogo kati ya shemeji na mkewe , yaani dada yangu. Jambo ambalo nilijifunza kwa shemeji ni subira na uvumilivu. Hakuwa akipenda sana kelele na kila zogo lilipoanza alikuwa akijibu kidogo na akiona dada haelewi alikuwa akijiondokea zake kunyoosha miguu kama alivyokuwa akiita mwenyewe. Kwa mara ya kwanza nilianza kuonja upendo wa mzazi wa kiume na kuonjeshwa roho mabaya inavyokuwa kwa mwanamke. Nilimshukuru mungu.

Lakini hali hiyo haikudumu. Nikiwa darasa la sita, jambo ambalo halikutegemewa na mtu lilitokea. Shemeji yangu alipata ajali ya gari wakati akitoka kusomba miwa. Gari lake lilimgonga mwendesha baiskeli na kumjeruhi sana. Kutokana na kosa hilo, alisimamishwa kazi, na baadae alifukuzwa. Kwa hiyo alitakiwa kuhama kwenye nyumba ile ya kampuni. Ilikuwa bahati kwamba wakati akiwa kazini alikuwa amejenga nyumba ya vyumba viwili iliyoezekwa kwa makuti kijijini Manyinga, umbali wa kilomita mbili kutoka kiwandani.

Ilibidi tuhamie hapo Manyinga. Alijitahidi kutafuta kazi kila mahali, lakini ilishindikana. Dada yangu alimwongezea machungu kwa kumsimanga. Nakumbuka siku moja walikuw2a wakigombana huko chumbani kwao usiku. Nilimsikia dada akimwambia shemeji kwamba, asipoangalia ataolewa. Alimwambia maneno hayo kwa kizigua.
Baada ya kauli hiyo sikusikia tena sauti ya shemeji na mimi binafsi niliumia kuliko hata yeye bila shaka. Asubuhi kabla sijaenda shuleni, shemeji aliniita na kuzungumza nami. ‘Nasafiri leo, usimwambie mtu. Nataka kwenda Moshio kwa kaka yangu, nikajaribu kama nitafanikiwa kupata kazi. Nina kaka yangu yuko kule TPC, nadhani atanisaidia.’ Halafu aliendelea. ‘Jitahidi, nikiwa kule nitajitahidi kuhakikisha kwamba unasoma hadi ufike Makerere.’ Alisema na kutabasamu. ‘Una akili sana na mungu amekupangia jambo kubwa maishani. Vumilia shida, kwa sababu zitakufundisha kuishi na kukabiliana na lolote baya maishani.’ Halafu akatoa shilingi 120 kutoka mfukoni na kunipa.

Niliondoka kwenda shule na inasikitisha kusema kwamba huo ulikuwa mwisho wa kuonana na shemji yangu nikiwa mtoto. Alipoondoka yale mateso yalianza na bila shaka yalikuwa makubwa kuliko mtu anavyoweza kufikiria. Ni mengi kiasi kwamba siwezi kuyaeleza yote. Lakini nayakumbuka yale makubwa ambayo pia ni mengi sana kiasi kwamba nikianza kuyasimulia nitakuchosha wewe msomaji. Lakini kubwa kuliko yote lilikuwa ni lile la kuunguzwa na kwa mafuta ya kula shavuni. Nasema kuwa hili ndilo kubwa zaidi kwa sababu ndilo lililobadili kabisa maisha yangu.

Hili lilitokea wakati niliwa darasa la saba, ikiwa ni miezi minne tu kabla ya kufanya mtihani wa mwisho.Nilikuwa na uhakika kwamba ningeweza kufaulu iwe au isiwe. Sikuw nauwezo wa kubahatisha kwa kweli. Nilikuwa ninayaelewa maisha. Nakumbuka baada ya shemeji kutoroka, dada yangu hakuwa na njia isipokuwa kuanza biashara ya maandazi na vitumbua. Mimi ndiye niliyekuwa naandaaa unga wa vitumbua na kukanda ule wa maandazi na pia kuchoma vitumbua na maandazi. Pamoja na kufanya kazi hizo kila siku sikuwa ninaruhusiwa kuonja hata kipande cha andazi wala kitumbua. Nilikuwa ninaondoka nyumbani asubuhi bila kunywa chai.

Siku ya tukio nilikuwa ndio namalizia kuchoma maandazi kwenye saa 12.30asubuhiili nijiandae kwenda shule. Mama alikuja na kukagua kazi. Aliona andazi moja likiwa limeungua. Alilichukuwa na kuniuliza, ‘Hivi mama yako ndiye ananunua unga huu unaouchezea?’ Nilitaka kujiteta lakini kabla sijafanya hivyo , nilihisi kitu fulani kikiparuza katika shavu langu. Ni mafuta ya moto! Dada alikuwa amechukuwa kijiko mcha mboga kilichokuwa hapo karibu na kuchota mafuta ya moto na kunimwagia. Halafu nilihisi maumivu ambayo ni vigumu kuyaelezea. Nilikurupuka kutoka pale na kutoka nje nikipiga kelele. Huko nje nilishika shavu langu na kutoka na ngozi. Nilikuwa nimeungua sana.

Kama vile kujihami dada yangu alitoka nje na kupiga kelele kwamba nimemwibia fedha zake zote za biashara. Majirani walikuja kuona kulikoni. Namkumbuka Mzee mmoja wa kichaga au kipare ambaye alikuwa na duka hapo kijijini, aliponiona alisema, ‘tumpeleke hospitalini, ameungua sana’ Wazo lake lilikubaliwa haraka na majirani wengine nilikimbizwa Bwagala Hospitalini.

Je wewe unaamini katika ndoto au maono? Mimi naamini kwa sababu nilishuhudia. Lakini kwanza ngoja niendelee na habari yangu hii yenye kufundisha.

Nilipelekwa hospitlini na wale wanakijiji. Dada na wanae hawakujali kabisa. Kale kabinti kake ka mwisho yaani Msekwa, kalilia sana kalipoona nimeunguzwa. Nakumbuka nilipolazwa hospitalini ndiko pekee kutoka nyumba ile kalikokuja kunitazama.

Nililazwa hospitalini kwa wiki mbili na wale wanakijiji walionipeleka hospitalini ndio waliochangishana na kunilipia gharama za kukaa hapo hospitalini. Nilitoka nikiwa na nafuu kubwa, ingawa shavu langu lilikuwa na alama kubwa ya kuunguzwa kule. Hata hivyo nilijua kwamba, hata baada ya kupona ningebaki na kovu hilo mileleNilipotoka hospitalini sikuweza kurejea kule kwa dada yangu na wale wanakijiji walionisaidia pia waliogopa kunipokea. Waliogopa kwa sababu dada yangu alikuwa akiwatisha kwamba nikifa watanila nyama. Ilibidi nifikirie namna mpya ya kuishi. Kumbuka wakati ule, tena vijijini, watu hawakuwa wanjua kitu kinachoitwa haki za binadamu, achilia mbali haki za mtoto. Watu walikuwa waoga kuingilia mambo ya familia za watu, hata kama mtu anakufa.

Unajua ni kwa nini nimekuuliza kuhusu maono? Ni hivi. Saiku ile nilipotoka hospitalini nililazimika kwenda kwenye mashamba yampunga ambapo niliomba kibarua cha kufukuza ndege kwa wenye mashamba hayo. Nakumbuka watoto wengi na watu wazima walikuwa wakifanya kibarua hicho. Kwa bahati nzuri mama mmoja aliniambia angenisaidia lakini malipo yangu ningepata baada ya mavuno. Aliniambia ningekula na kulala kwake hapo hapo shambani. Niliona kama vile nimepata dhahabu. Nilikubaliana naye.

Ilikuwa ni usiku wakati nikiwa bado sijapata usingizi vizuri, nilipokiona kitu hicho. Hapo kwenye kibanda cha shambani nilimokuwa, niliona kitu kama kivuli kidogo. Kivuli hicho kililkuwa mbele yangu. Kwa sababu ya giza sikujua kama ni kivuli cha mtu au hapana.

Niliogopa kupindukia na nilikuwa natetemeka pale kwenye godoro la sufi nilipokuwa nimelala. Halafu nilisikia kama sauti, ambayo sikujua kama inatoka kichwani mwangu au kwenye kile kivuli. Ilikuwa ikisema 'Muone tu mama mkubwa, ni lazima usome, ile sauti ilirudia tena na tena. Ilikuwa ni sauti niliyokuwa ninaifahamu.

Ilizidi kunisisitiza tena na tena. Nilishindwa kuvumilia ambapo nilipiga yowe kubwa na kuamka. Nilipapasa hapo chini na kuchukua kiberiti. Niliwasha kibatari huku mikono yangu ikitetemeka. Nilitazama mle kibandani na sikuona kitu. Nilikumbuka sauti ile kwa mbali sana. Ilikuw ni sauti ya mama yangu au mdogo wangu, sikuwa na uhakika sana.

Nilianza kufikiria kuhusu huyo mama mkubwa. Mimi sikuwa na mama mkubwa, sasa ni mama mkubwa yupi ambaye huenda sauti zile zilikuwa zikinielekeza kwake. Nilijiuliza karibu usiku mzima. Hatimaye kwa njia fulani ya ajabu nilikumbuka kwamba, wakati nikiwa nimelazwa pale hospitalini Bwagala, kulikuwa na watu waliokuwa wakimtaja mtu aliyeitwa mama mkubwa, ambaye wengine walisema ndiye mwenye hospitali ile.

Nilichukuliwa na usingizi kwenye saa kumi na nilishtushwa na mama mwenye shamba. Alikuwa akiniita huku akitukana kwani mpunga ulikuwa unashambuliwa na ndege. Nilitoka kibandani kwa kasi na kukutana naye mlangoni. ‘Samahani mama nimechelewa kuamka…’Hakusubiri nimalize kwani alinitaka niondoke pale shambani kwake saa ile ile. Niliondoka bila kuhitaji kujitetea, labda nilishazoeshwa kuishi kwa amri.
ITAENDELEA....................

Oct 10, 2009

NJIA YA MAISHA YAKO INAPOFUNGWA GHAFLA!

Ni kidonda kikubwa cha hisia, lakini nimemudu kukiponyesha na sasa limebaki kovu tu ambalo halina mauamivu kwangu. Kidonda hiki cha kihisia kilitokana na mkwaruzo ulioanzia kwenya familia yetu, yaani kwa wazazi wangu. Ndoa ya wazazi wangu haikuwa ndoa imara na wala mtu asingepaswa kuiita ndoa.

Nilizaliwa mwaka 1965 katiaka kijiji cha Segera, mkoani Tanga, kabla ya wazazi wetu hawajahamia Sindeni wilayani Handeni wakati huo, ambako ndiko nyumbani kwa baba yetu. Mama yetu alikuwa anatokea maeneo ya Mombo mkoani Tanga. Tulizaliwa wawili tu kwa baba na mama, mimi na mdogo wangu wa kike.

Nakumbuka Tangu nikiwa mdogo sana, nilishuhudia mama yangu akiwa anadhalilishwa. Alikuwa anapigwa sana, wakati mwingine alikuwa anavuliwa nguo mbele yetu au hata kutoka nje akikimbia uchi. Nakumbuka hata nilipokuwa naanza darasa la kwanza kuna siku nilichelewa darasani na mwalimu aliyekuwepo aliniuliza kama nilikuwa naamua ugomvi wa baba nyumbani ndio maan nikachelewa. Darasa zuima lilicheka na jambo hili sikulisahau kirahaisi. Ni ajabu kwamba hata zamani kulikuwa na waalimu wahuni.

Tukiwa wawili, mimi na mdogo wangu nyumbani, tulikuwa kama wakiwa kabisa. Mama yetu kwa kweli alikuwa mama ambaye ni adimu kumpata kwa ukarimu na uadilifu wake. Sisemi hivyo kwa sababu ni mama yangu , hapana. Hata jirani na waliomfahamu walijua jambo hilo na kulisema. Nakumbuka kila wakati alipenda sana kutupa moyo kwamba, maisha ni juhudi, uvumilivu na hekima.

Nikiwa darasa la nne mwaka 1975 na mdogo wangu akiwa anaanza la kwanza ndipo jambo baya kabisa lililotugusa na pengine kunifanya hivi nilivyo leo lilipotokea. Ilikuwa ni jumamosi nakumbuka nikiwa nimetokea shambani kuhamia ndege wasiharibu mpunga.

Niliporudi nyumbani hapakuwa na dalili ya kuwepo mtu. Giza lilikuwa limeingia, lakini nyumbani kulikuwa hakujawashwa taa. Niliingia ndani na kumwita mdogo wangu aliyekuwa akiitwa Selina. Lakini hakukuwa na jibu, wakati nikitaka kutoka nje nilisikia kama sauti ya mtu huko chumbani kwa wazazi wangu.

Niliita 'mama' na nilihisi kama nimeitikiwa. Nilibisha hodi na kuingia chumbani kwa wazazi wangu. Kwa sababu kulikuwa na giza sikuweza kuona vyema madhari ya chumba. Nilitoka na kwenda nje kwenye kibanda kilichokuwa kinatumika kama jiko. Nilichukuwa kiberiti na kurudi chumbani. Niliwasha taa.

Mama yangu alikuwa amelala kitandani akiwa ametapakaa damu usoni. Hakuwa na uwezo wa kuongea kwa sauti ingawa alikuwa akiongea . Nilimsogelea huku nikiwa nimeogopa sana. Alinyoosha mkono kama vile kuomba nimshike. Nilimshika mkono na alizungumza kwa shida sana. ‘Ni …ba…baba yako, laki….lakini msamehe tu. Mungu…..’ Halafu alinyamaza.

Wakati huo huo watu wawili waliingia ndani. Walikuwa ni wanawake rafiki zake mama. Pamoja nao alikuwepo Selina, ambaye kumbe alitumwa na mama kwenda kuwaita. Wanawake wale walikwenda moja kwa moja pale kitandani na kumkagua mama hukuwakimsemesha. Lakini bila shaka waligundua kwamba mambo sio shwari. Mmoja alitoka haraka.

Nilitoka na kusimama sebuleni, wakati huo huo tulimwona baba akiwa na katibu kata pamoja na viongozi wengine wa kijiji, wakiingia. Naye baba alikuwa na jeraha usoni lillokuwa likitoka damu bado. ‘Basi , wakamshambulia hapa, mimi kufika, ndio nikapigwa panga la uso nikadondoka….’ Alisema baba akiashiria kwamba, mama alikuwa ameshambuliwa na watu fulani. Viongozi wale waliingia chumbani kwa wazazi wetu moja kwa moja na huko tulimsikia yule mama aliyebaki mle chumbani akilia.

Ndivyo mama yetu alivyokufa na bila shaka ni mimi na mama na pia mungu ndio tuliojua kwamba, aliyemuuwa alikuwa ni baba na sio hao watu ambao baba aliwasingizia. Tulianza sasa kuishi maisha magumu sana ambayo siyo rahisi mtu kuamini unaposimuliwa. Tulikuwa tunakula kwa kubahatisha, shule tulisimama kwa sababu baba alikuwa kama vile anataka kuona tunakufa kama mama yetu……………

Nakumbuka kuna siku alinipiga sana kwa sababu tulichukua unga na kukoroga uji na kutumia sukari yake kidogo iliyokuwa mle nyumbani. Alinipiga hadi nikapoteza fahamu. Wakati ananipiga alikuwa akiniambia kuwa ataniuwa kama mama. Ukweli ni kwamba ilifika mahali ambapo niliona ni vyema kufanya jambo moja tu, ama kufa au kutoroka. Lakini nilipofikiria kufa, wazo la mdogo wangu lilinifanya kurudi nyuma. Niliamua kwamba, ingekuwa ni vizuri kwetu kutoroka. Mdogo wangu alikuwa mwerevu na mwenye upendo mkubwa na alinikumbusha mama yetu kila wakati.

Kama baba angekuwa anawaruhusu jirani au wale rafiki mama kutusaidia, huenda tungeishi kwa shida, lakini tungesoma. Lakini baba alikuwa mbogo kwa mtu yeyote ambaye alikuwa anajaribu kutupa msaada. Tulipanga na mdogo wangu tuondoke pale nyumbani na kwenda kwa dada yetu, mtoto wa mama yetu mkubwa aliyekuwa akiishi Mtibwa ambapo nauli yake ilikuwa ni kama shilingi tano.

Lakini usiku wa kuamkia siku ambayo ilikuwa tuondoke, Selina alianza kujisikia vibaya. Usiku alikuwa amepandwa sana na joto na alikuwa anatetemeka. Alikuwa na malaria bila shaka. Hali hii ilimuanza kama wiki wiki mbili nyuma, lakini ilikuwa ikiisha baada ya kunywa vidonge vya aspro. Ilikuwa kama saa sita usiku na baba alikuwa hajarudi. Niliamua kwenda kuwajulisha majirani ili waje watupe msaada. Wakati natoka nilikutana na baba mlangoni. Aliniuliza nilipokuwa naenda na nilimweleza.
'Kwani umeambiwa mimi sijui kulea, yaani mwanangu akasaidiwe kama manamba, rudi ndani.' Aliniambia na kunipiga kibao. Nilirudi ndani nikiwa ninalia kwa uchungu na mambo mengi. Baba aliupiga mlango komeo na kuutia kufuli kwa ndani. 'Toka nione, unajifanya kidume sana.'
Hakuja kumwangalia Selina na mimi nilikaa kwenye kitanda cha mdogo wangu hadi asubuhi. Kulipokucha na baba alipoondoka nilikimbia kwa majirani kuwambia kwamba, mdogo wangu alikuwa amezidiwa. Ukweli ni kwamba wakati huo mdogo wangu alikuwa amezidiwa kupita kiasi.

Jirani walifika kwa woga na kuamua kwenda kwanza kwa katibu kata kutoa taarifa ili baba asiwafanyie vurugu. Waliporudi tulimchukuwa mdogo wangu hadi kituo cha afya, Alifanyiwa vipimo na kuonekana ana malaria na tatizo la tumbo. Aliandikiwa dawa.
Inasikitisha sana kusema kwamba Selina alifariki usiku wa siku ile. Najua hivyo ndivyo ilivyo, kwamba sitakuja kulia kama nilivyolia siku ile. Maishani mwangu naamini sitakuja kum-miss mtu kama nilivyom-miss mdogo wangu mpendwa. Hata mke wangu siku hizi huwa ninamwambia na anakubali kwamba hata angekuwa yeye ingekuwa hivyo hivyo.

Kifo cha mdogo wangu kimenisumbua kwa miaka mingi hadi mwaka 2001nilipoanza kusoma gazeti la Jitambue, ndipo nilipojifunza kusahau na kujua kwamba kila jambo linakuja kwa sababu maalum na kwa kawaida ni vizuri tu, kama tutapenda iwe hivyo.
Tulimzika mdogo wangu na hakukuwa na matanga. Hakuna jirani ambaye alikuwa tayari kufanya matanga ya kifo cha aina ile. Usiku wa siku ile ndipo nilipoondoka pale kijijini na nasikitika kusema kwamba, sikurudi tena kijijini hapo hadi nilipokuwa mtu mzima, ambapo nilikwenda kutengeneza kaburi la mama na la mdogo wangu Selina.

Nilifika Mtibwa na kuulizia kiwandani ambapo nilielekezwa. Niliulizia hadi nikafika kwa dada yangu. Huwezi kuamini kwamba, swali la kwanza aliloniuliza huyo dada yangu ni kama nilikuwa nimekwenda pale kuishi au kusalimu tu. Nilipomsimulia kisa chote, Alinimbai kuwa pale kwake siyo nyumba ya kutunza watoto yatima.
Alimsimulia mume wake kwamba mama yangu alikuwa mtu mbaya sana. Alieleza kwamba, mimi na marehemu mdogo wangu tulikuwa tumelelewa kwa kudekezwa na hatukuwa watoto wanaoweza kishi na mtu. Inashangaza kwa sababu, huyu dada yangu mwenyewe nilikuwa najuana naye siku ile, nilikuwa simjui bali kumsikia tu kutoka kwa marehemu mama.

Mumewe alisikiliza maneno yake bila kusema neno. Baadae, huyo shemeji yangu aliniambia tunyooshe miguuili nikakijue kiwanda cha sukari. Tukiwa njiani alinimbia kwamba haamini kuwa dada yangu , yaani mkewe anasema kweli. Aliniambia kwamba, anachojua ni kwamba atanisaidia hadi nisome na kumaliza masomo yangu.

Ndugu msomaji maelezo ya habari hii yanayofuata ni yenye kuumiza kidogo, kwa sababu, yanaonyesha nyuso nyingi za binadamu na nyuso nyingi za uadilifu na uovu wake. Nimeona upate pumziko na kutafakari haya ambayo nimekusimulia kwanza, nisije nikakujaza nguvu hasi nyingi zaidi bila sababu.
Habari hii iliwahi kuandikwa katika Gazeti la Jitambue.....

Oct 1, 2009

UJUMBE WA SIMU: VIFO NA TALAKA


Simu hizi, mara nyingi huleta balaa

Nimekuwa nikisikia kuhusu vurugu za ndoa zinazotokana na simu za mkononi. Kwa upande wangu nilikuwa sijawahi kupambana na tukio lolote la kindoa linalohusu simu hadi hivi karibuni. Nimekuwa nikiamini kwamba simu zinaweza kusaidia mtu kujua kama mwenzake yuko kwenye uhusiano wa nje au hapana. Hadi sasa naamini hivyo, lakini, naamini pia kuwa zinaweza kuzua mtafaruku na kuvunja ndoa wakati hakuna jambo la maana.

Mimi Binafsi kwenye ndoa yangu sijawahi kuwa na uhusiano nje. Lakini kwa mazingira ya kazi yangu, nimezoeana sana na wanawake na pia wanaume. Nataniana sana na wanaume na wanawake, kiasi kwamba, kama mtu hajui anaweza kudhani nina uhusiano na wanawake hao.

Simu yangu hupata ujumbe wa aina mbalimbali ukiwemo wa utani kutoka kwa wanaume na wanawake. Utani huo unaweza kuwa wa kimapenzi, kifamilia, kikazi au mwingine mwingi. Kwa kazi yangu utani huu hunipa nguvu na hisia za ukaribu na watu, lakini kubwa zaidi hunifanya niwe mtani wa wanawake wengi wanaonifahamu kuliko kuwa kitu kingine.

Wiki kadhaa zilizopita kwa bahati mbaya au kwa kusudi, mke wangu alifungua ujumbe ulio kwenye simu yangu. Aliposoma alikutana na ujumbe wenye neno Dear. Bila shaka neno hilo likiwa limeandikwa na mwanamke, lilimfanya kuuliza maana ya neno lile.
Hakujali ujumbe ulisema kitu gani, bali alijali neno Dear. Kidogo lilitutikisa. Lakini mambo yaliisha.

Lakini walisema muonja asali haonji mara moja. Nadhani aliona kusoma ujumbe unaotumwa kwenye simu yangu kunamfanya apate nguvu au kuthibitisha anachotaka kuthibitisha, Siku nyingine tena kwa kile kinachoitwa bahati mbaya, alisoma tena ujumbe kwenye simu yangu.

Ujumbe huu sasa ulikuwa na neno Darling, sio Dear tena. Pamoja na neno hilo kulikuwa na maneno yenye kuonesha kwamba, aliyeniandikia anataka tuwe wapenzi na tushiriki tendo na kwamba, angependa anipeleke mahali kwa siku mbili na nisije nikaanza kumkumbuka mke wangu.

Kwa kweli nadhani ujumbe huu na hasa neno Darling, ulimvunja nguvu mke wangu kiasi kwamba, alilia kwa muda mrefu wa usiku. Nilihuzunika kwa hilo. Lakini nilijiambia na kujiuliza, ‘alikuwa na haki gani kukagua ujumbe kwenye simu yangu?’ Ukweli ni kwamba, simu ni yangu na watu ninao wasiliana nao , nawajua mimi na najua ni kwa nini nawasiliana nao kwa namna fulani. Yeye akisoma ujumbe wa aina yoyote, atafanya majumuisho yake na sio ya hali halisi.

Kwa mfano, mwanamke huyu ambaye, mke wangu alisoma ujumbe wake alianza kuniita Darling, baada ya siku moja kimzaha kuniuliza, ningependa kuitwa nani na yeye, bosi, mheshimiwa, baba fulani, au jina langu. Nilimuuliza, ‘mbona umesahau kutaja neno Darling?’ Kwa utani, kuanzia siku hapo akawa ananiita Darling.

Ujumbe aliousoma mke wangu, ulikuwa ni utani, ambapo alikuwa anasema, akija kunitembelea atanipeleka mahali na kwa sababu mimi najifanya naaminika, nimwombe mke wangu ruhusa ya siku mbili kwamba naenda semina. Tulijibizana kwa muda mrefu kwa ujumbe katika mzaha kama tulivyokuwa tumezoea.

Bila shaka kila mmoja kati yetu alikuwa huru, kwani kila mmoja alijua kuwa anachokifanya ni mzaha. Lakini hata kama mtu mwingine angetulia, ujumbe ule ulikuwa unaonesha utani wa wazi kabisa. Lakini kwa mke wangu ingekuwa vigumu kuona mzaha ndani ya ujumbe ule. Siyo kwake tu, bali hata kwako na kwa mwingine, ingekuwa hivyo. Kwa nini?

Hapa ndipo panawaumiza wengi kwenye suala la ujumbe kwenye simu. Hadi mtu achukue simu ya mpenzi wake na kuanza kukagua ujumbe uliotumwa humo au majina ya watu walio kwenye orodha ndani ya simu hiyo, ni lazima ana wasiwasi na mwenzake. Kwa sababu ya wasi wasi huo, chochote atakachokiona ambacho kinaonesha dalili za kukosa uaminifu, hatatumia akili kukipima, bali ataendeshwa na mihemko.

Ni kweli simu za mkononi zinatajwa kama moja ya vitu vinavyoweza kusema kama mtu anatoka nje. Kwenye kitabu chake, hayati Munga Tehenan cha Mapenzi Kuchipua na Kunyauka, anasema kuhusu mtu kupigiwa simu na kukimbia kwenda kusikilizia mbali na mahali mwenzake alipo.

Nimesoma makala kadhaa zinazohusu madhara ya simu za mkononi, lakini sijaona ujumbe au Message zikipewa uzito. Ujumbe hauna uzito kwa sababu kinachoonekana kwenye ujumbe ni mwendelezo wa jambo ambalo mtu asiyehusika na ujumbe huo hawezi kulijua.

Najaribu kufikiria namna ambavyo mke wangu angejisikia endapo angesoma ujumbe niliokuwa nimetumiwa na rafiki yangu siku nne nyuma kabla ya tukio hilo. Huyu rafiki yangu tunafahamiana sana na alituma ujumbe unaosema, ‘Kama unataka nimwambie mkeo unapomalizia fedha zako sawa. Mwenyewe anajua ana mume mwaminifu kweli, kumbe hajui jitu lina nyumba ndogo kila wilaya ya mkoa wa Dar.

Huu ulikuwa ni mzaha kutoka kwa huyu jamaa yangu. Lakini kwa mke wangu huu usingekuwa mzaha, kama ambavyo haikuonesha kuwa ni mzaha kwenye maelezo ya yule mama. Ndilo tatizo la ujumbe. Unakuwa hujui kitu kimeanzia na kinakwenda wapi.

Ninachotaka kusema hapa sio kuwambia wapenzi kwamba ujumbe wowote wa kimapenzi kwenye simu hauna maana. Kuna wakati ni kweli ujumbe husika una maana hiyohiyo inayosomeka. Kupitia ujumbe, mtu anaweza kumfumania mwenzake. Lakini, kwa sehemu kubwa ujumbe wa simu hauna nguvu na unaweza kusababisha ndoa kuingia doa na hata kuvunjika bila sababu.

Ni jambo la hekima kwa mwanamke au mwanaume kumchunguza au kufuatilia nyendo za mwenzake moja kwa moja. Kama unadhani mumeo au mkeo siyo mwaminifu, ni vyema kutumia mtu au watu wakafuatilia nyendo zake. Kama kweli anatoka nje, hauwezi kuzidi mwezi mmoja kabla hujapata ushahidi kuhusu jambo hilo. Huna haja ya kutegemea robo taarifa kama hizo za ujumbe wa simu. Ni kweli kwamba kuna matumizi mabaya ya simu kutumika kutongozana, kutaarifiana kuhusu uhusiano na mengine. Lakini siyo kila ujumbe wenye kunuka mapenzi una maana ya mapenzi.

Ninachowapenda waislamu kwenye ndoa ni lile suala la fumanizi. Wanasema ili ithibitike kwamba, kweli mtu amezini, ni lazima kitendo hicho kithibitishwe wakati kinatendeka na wanokithibitisha ni lazima wawe watu wanne. Kwa nini nawapenda kwa hilo?

Kuna mazingira mengi ambapo mtu anaweza kuamini kabisa kwamba, mwenzake anatoka nje. Hata anapowasimulia wenzake nao watampambisha moto kwa kumwambia, ‘haiwezekani, ni lazima wana uhusiano,’ wakati hakuna jambo kama hilo. Tunaona sana mambo haya kwenye sinema zinazooneshwa kwenye televisheni zetu.

Kwa upande wangu naweza kusimama na kuzungumzia ukweli kuhusu ujumbe wa simu kwa sababu, nina uzoefu wa kutosha, ambao umenisaidia kujifunza. Hata kabla ya uzoefu huo, nilishapata uzoefu mwingine unaohusu simu ambao unaonesha kwamba, ni lazima kuna ndoa nyingi sana zinayumba au kuvunjika kwa sababu ya simu, iwe ujumbe au kupiga kabisa.

Nikipi kinasema kweli, ni tabia ya mtu kama tunavyoijua au ujumbe tuliouona kwenye simu? Nafikiri kuwa unamjua vipi mume au mke wako, ndilo jambo la msingi kwanza. Kama humwamini, ni lazima utapata mazingira ya kuthibitisha wasiwasi wako. Utachakura kwenye simu yake, utapekua mkoba wake, utakagua mifuko ya nguo zake na hata ‘diary’ yake utaikagua kila wakati. Kwa sababu lengo ni kuthibitisha kwamba siyo mwaminifu, ni lazima utathibitisha.

Kwa uzoefu wangu wa simu za mkononi na uhusiano, ninaingia wasiwasi mkubwa kwamba, kwa kadiri simu hizi zinavyokuwa nyingi mikononi mwa watu na hasa wapenzi, ndivyo ambavyo mapenzi yanaporomoka. Badala ya kusaidia kukuza uhusiano, zinasaidia kuvunja uhusianvo lakini wamiliki wa simu hizi ndio ambao wanapaswa kulaumiwa.

Kushinwa kujua kwamba, simu kila mmoja ni yake na yaliyomo ndani ya simu ni yake na yeye ndiye mwenye kujua maana yake, hilo huwaumiza wengi. Niliwahi kupokea ujumbe kwenye simu ambao unasema, ‘kumbe umeshikwa na mkeo, wewe mpumbavu kweli. Kumbe umekuwa unapoteza bure muda wangu.’ Kabla sijakaa sawa, nikatumiwa ujumbe mwingine na mtu huyo huyo akisema, ‘Kama unaona vipi tuachie hapahapa kabla hatujafika mbali, tusije kuumizana bure.’

Ilibidi nimpigie simu huyo aliyetuma ujumbe huo. Nilipomwambia kwamba huenda amekosea namba , alikiri.
Lakini alisema kuna mtu ameanza kufanya naye biashara na amegundua kuwa kila kitu ni hadi mke wa huyo jamaa aamue. Hivyo ameamua kumwonya, kwani kwa sababu hiyo tayari wameshapata hasara.

Je mke wa huyo jamaa angeuona ujumbe ule kwenye simu ya mumewe angeelewa hivyo? Sio rahisi, angeelewa kwamba huyo mwanamke ni hawara wa mumewe na anataka wavunje uhusiano kwa sababu hampi anachokitaka, yaani kuwa naye muda mwingi au wote.

Ubaya wa ujumbe ni kwamba huwezi kuzuia usiingie, tofauti na kupigiwa,ambapo unaweza kukata simu au unaweza kuacha mtu azungumze wakati simu umeiweka mbali.

Hapo hakuna ushahidi unaoachwa, Ujumbe huacha ushahidi ambao ni dhaifu sana, hata hivyo. Kama nilivyosema awali, kuna kuvunjika kwa ndoa kwingi sana, kutokana na simu za mkononi.

Lakini bahati mbaya ni kwamba, kuna kuuana au kujiua au kuuawa ambapo chanzo ni simu za mkononi. Ni kwa nini binadamu awe kipofu kirahisi kiasi hicho?Kwa nini simu ndio imfundishe kuhusu mwenzake, badala ya mwenyewe kumjua mwenzake?

Habari hii iliwahi kuandikwa katika gazeti la Jitambue

Sep 26, 2009

MASAIBU YALIYONIKUTA USIKU WA JANA!

Ilikuwa ni kazi kweli kweli, lakini yote yalikuwa ni majaaliwa

Kuna wakati Rais wa awamu ya pili ndugu Ali Hassan Mwinyi aliwahi kusema kuwa moto mkubwa huanzishwa na cheche, akimaanisha kuwa jambo lolote kubwa linaweza kuanzishwa na jambo dogo sana.

Jana wakati narudi kutoka katika mihangaiko yangu majira ya saa tatu usiku nilipata mkasa ambao mpaka leo hata sijui ilikuwaje, nilipanda basi la kuelekea Buguruni pale maeneo ya Posta majira ya sa tatu usiku hivi. Tulipofika Maeneo ya Kariakoo walipanda abiria wengine watatu lakini walionekana kuwa wamelewa sana. Wakati tukiendelea na safari mara ukazuka mzozo kati ya mmoja wa wale abiria waliolewa na abiria mwingine, kisa huyo abiria mwingine kakanyagwa na yule mlevi.

Vikazuka vita vya maneno, ilianza taratibu hivi, lakini kwa jinsi basi lilivyokuwa likiendelea na safari na ndivyo wimbo wa matusi kati ya abiria hao ulivyozidi kupamba moto, kutahamaki wakaanza kutupiana matusi ya nguoni na ya kudhalilisha sana haya yakilenga kuwadhalilisha wazazi wa kike, naamini mmeelewa mpaka hapo namaanisha nini.

Nilianza kuhisi shari mapema kabisa lakini sikuwa na jinsi nilikaa siti ya mwisho, kwani kama ningekaa karibu na mlango ningeshuka, lakini basi lilijaa na hapakuwa na njia ya kupita.
Vita ile ya matusi na ilianza kuwa kuwahusisha abiria wengine ambao walikerwa na matusi ya wale abiria walevi, ghafla wakaanza kupigana huku basi likiendelea kwenda kwa kasi. Mara zikazua kelele za abiria wengine wakimtaka dereva asimamishe basi ili watu washuke kwenye basi ili kuepuka ule ugomvi ambao sasa uligeuka kuwa ugomvi wa kupigana zilizidi mle ndani ya basi.

Dereva alisimamissha basi na kwa kuwa walikuwa wamengushana sakafuni kwenye basi ilibidi tupite juu ya viti ili kuelekea mlangoni, nilipoukaribia mlango abiria mmoja akamuamrisha dereva apeleka basi kituo cha Polisi pale Buguruni, nilikuwa bado sijateremka, ghafla basi likaondolewa kwa kasi ajabu, abiria mmoja akanisukuma na kujikuta niko chini kwenye lami na niliona tairi la nyuma la lile basi likipita usawa wa uso wangu, kutahamaki nikasikia sauti ya gari lingine likifunga breki za ghafla, nilipogeuka niliona gari dogo likiwa usawa wa pale nilipoangukia, nilijizoa pale na kujisogeza kando ya barabara, huku wapita njia wakinizunguka kutaka kujua kama nimeumia au la, ili wanikimbize hospitali. Nilijichunguza na kuona kuwa nina michubuko kidogo katika mikono yangu kutokana na kuangukia kwenye lami, lakini nilihisi mkono wangu wa kulia ukiuma kwa mbali, niliyapuuzia yale maumivu na hata niliposhauriwa niepekwe hospitali nilikataa kwani hata basi lenyewe lilishatokomea kusikijulikana.

Nilipanda basi lingine na kurudi nyumbani kwangu, nilipolala, ndio nikanza kusikia mausmivu makali ya mkono wangu wa kulia, na sikulala pamoja na kumeza vidonge vya kutuliza maumivu. Alifajiri na mapema niliwahi hospitalini na baada ya kupigwa X-Ray ikaonekana kuwa mkono wangu umeteguka kwenye kiungo. Nikatibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani.

Bado najiuliza, hivi ilikuwaje, kwa nini wale abiria ambao hawakulewa hawakuwapuuza wale abiria waliolewa na kuwaona kama wajinga hivi ili kuepusha shari? kwa nini walishindwa kuwavumilia kwa dakika chache ambapo kila mtu angeshuka kwenye basi na kuelekea nyumbani kwake?

Ni kitu gani wangepoteza kwa kuwapuuza walevi wale? Hivi kama lile gari lingenikanyaga ni nani angelaumiwa, ni wale abiria walevi au dereva? Na lile gari dogo je? kama dereva asingefunga breki ingekuwaje?

Pamoja na kuwa mkono wangu wa kulia umefungwa bendeji na hauna kazi lakini kwa kutumia mkono mmoja wa kushoto nimemudu kuwapasha yaliyonikuta jana
.

Sep 18, 2009

BADILIKA, JIONDOE AU KUBALI ILI UISHI.

Huwezi kupingana na hali halisi

Yapo makosa matatu ambayo mtu huwezi kuyafanya bila kujua athari zake. Makosa hayo ni kulaumu, kuunga mkono na kulalamka. Makosa ambayo mtu anaweza kuyaepuka kwa kuona ukweli kwamba ni yeye anayewajibika kwa nafasi yake.

Lipo swali moja kubwa ambalo watu huuliza, nalo ni: ‘Ni vipi nitadhibiti kile kinachonitokea ama kile watu wengine wanachoweza kusema ama kufanya?’ Jibu ni wazi, nalo ni kwamba huwezi kudhibiti kile kinachokutokea.

Kitu pekee uwezacho kudhibiti ni jinsi unavyokabiliana na hali iliyopo mbele yako. Wapo wanaopenda kukabiliana na matatizo yao kwa kulaumu watu wengine ama kujaribu kuunga mkono na kutetea kile ambacho wao walifanya kabla ya hali hii kutokea, ama kulalamika kuhusu hali hiyo.

Uamuzi wa kubadili, kuacha ama kukubali hali iliyopo ndilo jibu sahihi la makosa matatu ambayo watu hufanya.

Ni wazi, chaguo hili linatakiwa kufanyika tu wakati unapokuwa kwenye hali usiyoipenda. Unawezaje kuamua kuachana ama kubadili hali ambayo kwako wewe imezoeleka? Watu wengi wanafanya hivyo na mara nyingi bila kujua. Wakati unapojikuta kwenye hali usiyoipenda, fikiria mambo haya matatu kabla ya kuanza kulaumu, kushutumu ama kujilazimisha kukubali:

BADILI: Unapojikuta kwenye hali usiyoipenda, unaweza kufanya jitihada za kuibadili au kubadili mtazamo wako kuhusu hali hiyo . Ikiwa uko katika uhusiano unaodhani haukusaidii kwa mfano, unaweza kwenda kwa washauri nasaha, unaweza kuzungumza na mwenzi wako na kujaribu kuufanya uhusiano huo uwe bora zaidi ama waweza kubadili mtazamo wako wa namna uhusiano wenye faida unavyotakiwa kuwa.

Mara nyingi huu ni uchaguzi mgumu sana kuufanya kwa sababu inaweza ikalazimu kumkabili mtu mwingine kutoka katika tabia isiyo na faida kwako. Kubadilika kunatuondoa kwenye nafasi yetu tuliyoizoea na ambayo tunaiona inatufariji na kunahitaji ujasiri mkubwa kufanya hivyo.

Kuamua kuacha kumtegemea mpenzi kukupa furaha na kutafuta furaha kutoka vyanzo vyenye kuaminika zaidi siyo jambo rahisi, lakini ni muhimu.

JIONDOE: Kama umeshindwa kubadili hali kwa sababu yoyote ile umeshindwa kumfanya mtu abadili tabia yake kwa mfano,ni bora kujiondoa, ondoka kabisa.
Kujiondoa kunakufanya uondokane na hali isiyofurahisha na kunasafisha njia kwako kwa ajili ya kuchagua jambo jingine mbadala.

Ni wazi,watu wengi hukimbilia kuchagua njia hii, hukimbilia kujiondoa kwa sababu huogopa sana kujaribu njia ya kwanza ya kubadili hali ama kubadilika wao wenyewe.

Lakini ingawa kukimbilia hatua hii bila kujaribu ya kwanza si busara, kuna wakati ambapo kujiondoa ni hatua pekee ifaayo kuchukua. Hata hii nayo inahitaji ujasiri mkubwa kwa sababu, mara nyingi akili zetu hutuweka katika nafasi ya kutumia methali ya ‘Zimwi likujualo’ kama utetezi wa kuendelea kuvumilia madhila yasiyo muhimu tunayokumbana nayo.

KUBALI: hatua ya mwisho unayoweza kuchukua kukubali. Ziko hali ambazo huwezi kuzibadili na kukwepa ukweli wa jambo hilo, ni sawa na wendawazimu. Hebu mfikirie mfungwa wa kisiasa kama ilivyokuwa kwa mzee Nelson Mandela wa Afrika Kusini na wenzake.

Wakati alipokuwa akishikiliwa jela, asingeweza kuibadili hali ile, wala asingeweza kuamua kuondoka. Hakuna jingine aliloweza kufanya ila kukubali hali halisi na kufanya kila analoweza kuishi katika hali hiyo.

Kuna wakati kukubali linakuwa ni chaguo la kwanza tunalopaswa kuelekeza macho yetu, wakati tukiwa tunafikiria njia bora ya kubadili hali au kujiondoa.

Nina hakika kila mtu anapotazama mambo yanayozunguka maisha yake, atakutana na moja ambalo haridhishwi nalo kwa asilimia 100. Utafanya nini kushughulikia hilo, utajaribu kubadili hali au mtazamo wako wa hali? Uko tayari kujiondoa ikiwa una hakika huwezi kubadili hali au uko tayari kubadili mtazamo wako kuhusu jambo hilo ili uweze kuendelea nalo? Uko tayari kukubali kile ambacho huna uwezo wa kukibadili na wala huwezi kujiondoa?

Nafasi ni yako kutumia busara zako kuchagua.

Kumbuka, maisha unayoishi ni chaguo lako mwenyewe, ingawa ni vigumu kuliona na kukubali jambo hilo.

Sep 14, 2009

YAWAJE MTU ASIONWE WAKATI YUPO?

Kwa kawaida huwa tunajidanganya na kudhani tunajua mengi sana kuhusu maisha au yote kuhusu maisha, wakati ukweli ni kwamba tunayoyajua ni yale kidogo tu ambayo tumekutana nayo au kujifunza maishani. Mara nyingi mtu anapozungumzia nguvu fulani zilizoko kwenye dunia hii au ulimwenguni anaweza kuonekana kituko.

Hebu soma habari hii ya kweli ambayo imewahi kuandikwa kwenye vyombo mbali mbali vya habari huko Ulaya siku za nyuma.

Peter wa Gloucestershire huko Uingereza alipatwa na jambo lenye kushangaza sana mwaka 1987. Akiwa katikati ya sherehe ya jamaa yake mmoja alishikwa na haja ndogo.
Aliamua kwenda kujisaidia maliwatoni. Nyuma yake kulikuwa na mwanamke aliyekuwa anelekea huko huko maliwatoni {kumbuka sherehe ilikuwa nyumbani ambapo vyoo havikutengwa vya wanawake na wanaume}

Peter alijisaidia haraka na kutoka ili huyo bibie naye akajisaidie. Alimsalimia wakati anatoka chooni baada ya kujisaidia, lakini yule mwanamke hakuitikia. Kwa Peter halikuwa ni jambo la maana sana na hakulitilia manani. Alienda zake sebuleni ambako muziki na vinywaji vilikuwa vikiendelea. Alipofika hapo alienda kukaa kwenye meza ambapo rafiki zake walikuwepo.

Alipokaa alichukua kinywaji chake na kuanza kuzungumza na hao rafiki zake. Lakini hao rafiki zake walionekana kumpuuzia. Kila aliposema wao hawakumjibu wala kumtazama, waliendelea tu na mazungumzo yao. Peter alijua wameamua kumfanyia mzaha, hivyo aliamua kunyamaza ili kujua lengo la ule mzaha wao.

Kwa kuwa alikuwa ameshikwa na hamu ya sigara, aliamua kuinuka na kumfuata bibi yake ili ampatie moto awashe sigara yake. Ajabu ni kwamba, alipofika pale kwa bibi yake na kumnyooshea mkono ili ampatie sigara aliyokuwa anavuta ili awashe yake, bibi yake hakuonekana kujali. Peter alinyoosha mkono karibu na bibi yake huyo, lakini bibie aliendelea kucheza bila dalili kwamba mbele yake alikuwa akiona mtu.

Peter kuona hivyo alikasirika. Ni mzaha gani wakijinga, aliwaza!Rafiki zake pale mezani wamempuuzia na bibi yake tena anampuuzia, kwa nini? Aliamua kurudi chooni ili ajikague vema, huenda kuna kitu hawataki kumwambia kwamba amechemsha, hasa mavazi.

Peter anasimulia: Nikarudi chooni, kufika namkuta yule mwanamke bado anasubiri pale mlangoni labda akiamini kwamba, labda sijatoka humo. Nilipomuona bado anasubiri, nilikumbuka kwamba, nilipotoka nilimsalimu na hakuitikia. 'Yule mwanamke aligeuka na kuniona. Aliponiona alishtuka sana, 'kumbe umeshatoka wala sikukuona, ningejikojolea nikiwa hapa hapa, 'yule mwanamke alisema kwa mshangao'

Peter alisema alipoenda tena sebuleni rafiki zake na bibi yake walimuuliza alipokuwa muda wote huo. 'chooni ndio ukae mwaka mzima?' Walimwambia.
Anasema, alipowauliza kama ni kweli hawakumwona, walimwambia, hawakumwona. Aliwaeleza kilichotokea na wakabaki wameshangaa.

Je wewe imeshakutokea hali kama hiyo? Kama bado au kama hujawahi kuisikia , haina maana kama haipo. Hiyo ni hali yenye kuwatokea watu kwa idadi ya kutosha. Tofauti iko kwenye kiwango tu. Wengine huwatokea kwa muda mfupi sana, kama sekunde tano au kumi na wengine hata dakika tano au zaidi, kama ilivyotokea kwa Peter.

Ni hali ambayo mtu anapoteza uwezo wake wa kuonwa na wengine. Mtu anaamini kwamba wengine wanamuona kama kawaida, wakati wala hawamuoni. Hawamuoni mwili na wala hawasikii sauti yake. Hali hii ambayo kitaalamu hufahamika kama invisibility, huwatokea wengi pengine hata ukiwemo wewe, bali inakuwa vigumu kung'amua kwa sababu unaweza kutafsiri kama dharau.

Kwa mfano, kuna siku nilikuwa ninampa kondakta wa basi la daladala nauli, nikaona hapokei, bali anapokea za wengine tu. Kuona hivyo nilikasirika sana, na kuacha kumpa. Nilishuka kituo kinachofuata nikiwa nimenyoosha mkono ili achukue pesa zake, lakionoi wala hakunitazama, alikuwa anawadai wengine tu.

Kwa sababu naijua hii hali ya invisibility, sikushangaa sana, nilitabasamu. Kwa asiyeijua ataitafsiri kwa njia mbali mbali na hivyo hatajua ukweli.
Kuna wakati mtu anakwenda hotelini, halafu anakuta wahudumu wote wanampita tu , hadi baada ya dakika fulani, kama vile wahudumu wanatoka usingizini ndio wanamwona na kumfuata. Mwingine anaweza hata kufoka, lakini wahudumu wanaonekana hawamjali , kumbe hawamwoni.

Hivi ni kitu gani kinatokea hadi mtu haonekani? Hilo ni swali ambalo bado halijapatiwa jibu. Lakini, huenda Wajapani watatoa jibu hivi karibuni, kwani wamegundua tayari.

Habari hii iliwahi kuandikwa katika Gazeti la Jitambue.

Aug 20, 2009

MATANGAZO YA BIASHARA YALIYOJAA ULAGHAI HAYA HAPA!!!

Duka la Runinga

Kutokana na utandawazi pamoja na soko huria, siku hizi tumeshuhudia muingiliano wa mkubwa wa kibiashara ambapo yako makampuni mengi ya kigeni yamefungua biashara hapa nchini na hivyo tumejikuta tukiwa tumezungukwa na bidhaa mbalimbali toka nchi za Magharibi na Asia kwa ujumla.

Kutokana na hali hiyo tumejikuta tukishuhudia matangazo ya biashara kila mahali kuanzia kwenye vyombo vya habari hadi kwenye vipeperushi, na hivyo hata ile methali yetu ya chema chajiuza na kibaya chajitembeza inaonekana kupitwa na wakati.

Mfumo huu wa matangazo ya biashara upo wa aina nyingi sana hivyo ni vyema tukajifunza baadhi ya matangazo yaliyojaa ulaghai ili tuwe makini wakati wa kufanya manunuzi.

Yapo matangazo yanayotolewa katika mfumo wa aina mbalimbali yakionesha bidhaa zinazouzwa kwenye duka husika likiwa na bei halisi na punguzo maalum kwa muda maalum. Matangazo ya aina hii hujulikana kama Informative advertisement na ni mazuri kwa kuwa yanamfanya mnunuzi aweze kuchagua bidhaa akiwa nyumbani na huku akiwa na uhakika na bei, hivyo kupanga bajeti kulingana na kipato chake.

Lakini inashauriwa kuwa makini na matangazo ya aina hii, kwani mengi yamejaa ulaghai kwa kiasi fulani. Kwa mfano, unaweza kukuta bidhaa imeandikwa kuwa, sasa inauzwa kwa kupunguzo la asilimia 25. Hapo mnunuzi lazima ujiulize kuwa ni asilimia 25 ya bei gani?

Kwani yawezekana kweli kuna punguzo la asilimia 25, lakini vile vile kuna uwezekano pia, kuwa bei ya awali iliongezwa asilimia 50 zaidi ya bei halisi, hivyo unaweza kukuta bei ya bidhaa ile ni ghali ukilinganisha na maduka mengine.

Hivyo inashauriwa kufanya utafiti na kulinganisha bei katika maduka mengine, kwani hii itakusaidia kuepuka gharama za ziada zilizojificha.

Aina ya pili ya matangazo ya biashara ni hii inayohusisha bidhaa ambazo zimejijengea umaarufu ulimwenguni pote. {Brand name Advertising}. Naamini kuwa wengi sio wageni wa bidhaa kama Sony, JVC, Nokia kwa upande wa vifaa vya Elektroniki, Lee na Levi kwa upande wa nguo za Dangriz maarufu kama Jeans, au Nikon na Minolta kwa upande wa kamera.

Mara nyingi bidhaa za aina hii huwa zinajiuza zenyewe kutokana na umaarufu na uimara wake, ingawa pia bei yake ni ghali kutokana na umaarufu wa bidha yenyewe. Hivyo utakuta mara nyingi mtu anayetaka kununua bidhaa za aina hii huwa anajiandaa kifedha kwa kuwa anajua kabisa bei haitakuwa ndogo.

Lakini pia ningependa kutahadharisha kuwa siku hizi kumeibuka makampuni/viwanda vinavyotengeneza bidhaa zinazofanana kabisa na bidhaa nilizotaja hapo juu na kuandika jina linalofanana na majina niliyoyataja awali, lakini majina yenyewe yanaweza kubadilishwa herufi mojawapo ili isifanane na bidhaa halisi au kubadilisha alama pia ili isiwiane na bidhaa halisi.Hii inafanyika makusudi ili kuepuka kufunguliwa mashitaka na makampuni husika ambayo ndiyo wazalishaji halisi wa bidhaa hizo.

Mara nyingi bidhaa hizi huuzwa kwa bei rahisi sana, ukilinganisha na bei ya bidhaa halisi, hivyo mnunuzi anapoona, kwa haraka hununua bila kuchunguza na kujikuta amenunua bidhaa duni.

Aina ya tatu ya matangazo ni ile ambayo haimtendei haki mteja, kwa kutumia lugha laghai kushawishi wateja, ambapo lugha inayotumika inakuwa inaukweli lakini inapotosha kwa upande mwingine. Aina hii ya tangazo la biashara hujulikana kitaalamu kama Deceptive Advertising.

Hebu tuangalie mfano huu ufuatao kuhusiana na mchele. Unakuta tangazo kwenye gazeti linalosomeka “Jipatie mchele safi toka Kyela kwa bei ya shilingi 800 kwa kilo moja”.
Kwa haraka msomaji anaamini kuwa mchele unaolimwa Kyela unapatikana kwa bei rahisi kiasi kile, hivyo inamgharimu mteja kusafiri au kuendesha gari lake umbali wa kama kilomita 30 kufuatilia mchele kutoka Kyela, lakini anapofika pale anagundua kuwa ule mchele sio wa Kyela na hauna ubora kama mchele wa Kyela.

Anapomuuliza mwenye duka, kuwa kwa nini ametangaza kuwa anauza mchele kutoka Kyela wakati hana huo mchele wenyewe, mwenye duka anamjibu kuwa duka lake ndilo linaloitwa Kyela Trading Company, hivyo alikuwa anamaanisha jina la duka lake.

Kwa hiyo kwa mfano huo utakuta kuwa tangazo la mwenye duka lile halikuwa na makosa, bali lilikuwa linapotosha wateja, kwa sababu wateja wengi wangedhani kuwa duka lile linauza mchele kutoka Kyela, hivyo kwa kuzingatia usumbufu alioupata katika kufuatilia mchele ule atajikuta hana budi kununua mchele huo usio wa Kyela japo hata kilo moja kuliko kurudi mikono mitupu.

Aina ya nne ni ile ambayo mwenye duka anatangaza kuwa aina fulani ya bidhaa inapatikana dukani kwake kwa bei pungufu ya karibu shilingi elfu kumi au elfu hamsini ukilinganisha na bei ya maduka mengine. Ningependa kuelezea aina hii ya tangazo kwa kutumia mfano ufuatao.

Fikiria unasoma tangazo la duka linalouza runinga (TV) kwa bei labda teseme yenye punguzo la karibu shilingi 40,000, ukilinganisha na bei ya maduka mengine. Ukizingatia kuwa mkeo na watoto, wamekuwa wakikughasi kuhusu umuhimu wa kununua runinga na baada ya kuzunguka sana madukani ukakuta aina ya runinga unayoitaka, lakini inauzwa ghali ukilinganisha na bajeti yako, hivyo ukaamua kuahirisha.

Lakini kwa bahati unakutana na tangazo kwenye gazeti ambalo lina tangazo la duka linalouza runinga uliyokuwa unaitafuta kwa bei ambayo hukuitarajia. Unafunga safari hadi kwenye duka hilo na unapofika unakuta runinga hizo hazipo, unapomuuliza muhusika, anakuonesha maneno yaliyoandikwa kwenye tangazo hilo, chini kabisa, tena kwa maandishi madogo sana yanayosema kuwa runinga zile zilikuwa zinauzwa kwa idadi maalum, hata hivyo anakwambia kuwa anazo runinga nyingine nzuri sana zaidi ya zile zilizoisha. Kwa kuwa umekuja tayari na fedha inakuwa ni rahisi kwake kukuchota ununue runinga hizo ambazo hazina ubora ulioukusudia kwa bei kubwa na pengine ambayo hukuitaka.

Aina hii ya matangazo hufanana na hii ambayo hutumiwa sana na wauza magari. Ni ile ambayo muuzaji hutumia picha katika tangazo kupotosha. Kwa mfano unataka kununua gari. Baada ya kusoma matangazo kwenye magazeti, unakutana na tangazo la kampuni fulani inayouza magari ambapo unakutana na picha ya gari ulilokuwa unatamani kulimiliki likiwa linauzwa kwa bei ambayo unaimudu.Unapofika pale dukani unakuta picha uliyoiona kwenye tangazo haifanani na gari halisi ulilokuwa unalitaka, kwani mara nyingi picha huwa zina mvuto wa pekee.

Wakati umebaki ukijiuliza, muuzaji anakuonesha aina nyingine ya gari zuri na anakuahidi kukupunguzia bei kama utataka kulinunua. Baada ya majadiliano mnakubaliana bei ambayo inakubidi ukaongeze fedha kidogo, na kwa kuwa gari lenyewe ni zuri sana na lina ubora kushinda lile ulilolitaka, unajiona u mwenye bahati, hivyo unaondoka huku ukiahidi kurudi siku inayofuata kununua gari hilo.

Unapofika pale siku inayofuata, yule muuzaji anakupeleka ofisini. Wakati anaanda makabrasha ya kusaini kabla ya kupokea fedha au hundi, mara inapigwa simu, yule muuzaji anapokea ile simu na kuongea nayo, baada ya majadiliano fulani kwenye simu, anakwambia kwamba, mwenye duka kasitisha uuzwaji wa gari lile kwani amegundua kuwa ataingia hasara, hivyo itabidi uongeze fedha kidogo. Kwa kuwa ulijiandaa kununua gari unajikuta huna jinsi, unaongeza fedha zaidi na kununua gari lile, hasa ukizingatia kuwa wauzaji wa maduka ya magari wana lugha nzuri ya kushawishi, inakuwa ni vigumu kwako kujinasua au kuukwepa mtego huo. Baadae ukichunguza utakuta umeuziwa bei sawa au zaidi ya bei ya maduka mengine. Aina ya tangazo hili la biashara hujulikana kama Low-Ball Phenomenon na wauzaji wengi wa magari wamethibitisha kuwa wateja wengi hununua magari kwa mfumo huu, hivyo kuwaingizia faida.

Sina maana kwamba matangazo yote ni ya ulaghai, au matangazo yote ni mabaya, hapana. Ninachotaka ukifahamu ni kwamba , usipokuwa mwangalifu unaweza kujikuta umeongozwa vibaya na matangazo na kununua kitu ambacho wala hukuwahi kukifikiria kabla na pengine kwa bei kubwa zaidi.

Lakini unaweza pia kujikuta ukiwa mtumwa wa matangazo kwa maana ya kuyaamini sana kiasi kwamba utadhani kila kinachotangazwa ndivyo kilivyo. Pia unapaswa kujua kwamba kuna wanaotangaza bidhaa halali na kwa njia halali ambao hao unaweza kuwabaini kwa kuzingatia kile ambacho nimekwambia. Kila ukisoma tangazo likague vizuri kabla hujaamua.

Tukutane wakati mwingine………

Aug 16, 2009

WAUAJI WADOGO WA KISHETANI, SEHEMU YA MWISHO

Familia ya Lillelid


Mnamo Novemba 1997 watuhumiwa wote walifikishwa katika mahakama ya Greene County na kusomewa mashitaka 29 wote kwa pamoja.

Jaji aliyekuwa akiendesha kesi hiyo James Backner alikataa mapendekezo yaliyotolewa na jopo la mawakili waliokuwa wakiwatetea watuhumiwa kuwa kila mmoja ashitakiwe na kosa lake.

Jaji huyo alisema, watuhumiwa wote watashitakiwa kama kundi.
Wakati kesi hiyo ikiendeshwa, siri nyngi za watuhumiwa zilianikwa pale mahakamani.

Akitoa ushahidi wake mama yake Natasha aitwae Madona Wallen aliiambia mahakama kuwa mwanaye alikuwa ni mfuasi wa shetani na alikuwa ni muumini wa Ouija, ambayo ni imani kuwa watu walio hai wanaweza kuwasiliana na watu waliokufa.

Mama huyo alikiri kuwa, kuna wakati aliwahi kumuona mwanae, midomo yake ikiwa imetapakaa damu baada ya kunywa damu.
Naye rafiki wa karibu wa Natasha aitwae John Slayer aliyekuwa na umri wa miaka 19 akitoa ushahidi wake mahakamani alikiri kwamba, siku moja Natasha na mwenzie Karen walimuomba wamkata kifuani ili wapate kunyonya damu, naye akawaruhusu, ndipo wakamfunga kitambaa usoni kasha wakamkata na kuanza kumnyonya damu.

John alikiri pia kuwa zoezi hilo la kunyonya damu liliendelea kwa mtuhumiwa mwenzao John Risner na rafiki yao mwingine aitwae Jason Cecil.

Jambo lililowashangaza watu wengi wakati wa kusikilizwa kwa kesi hii ni kitendo cha Crystal Sturgil kumtaja mtuhumiwa mwenzake mwenye umri mdogo kabisa kuliko wote Jason Bryant kuwa ndiye aliyefyatua risasi na kuwauwa Lillelid na familia yake.

Wakati huo Jason alikuwa amehifadhiwa kwenye jela ya watoto ya Arizona akisubiri kusikilizwa kwa shauri lake tofauti na wenzie kutokana na umri wake.

Hata hivyo, kuna wakati alinukuliwa na mfungwa mwenzie aitwae Richard Arvizo akijisifu kwa kuuwa. Kwa mujibu wa maelezo aliyoandikisha polisi chini ya kiapo, Richard alidai kuwa, alipomuuliza Jason kama anajisikiaje kuuwa ? Jason alijibu kwamba, kuuwa huwa kunampa furaha na nguvu za ajabu.

Ushahidi mwingine uliotolewa pale mahakamani ni ule wa mwalimu aliyekuwa akimfundisha mmoja wa watuhumiwa Dean Mullins.
Akizungumzia tabia ya mwanafunzi wake wa zamani, mwalimu huyo alikiri kwamba, kuna wakati aliwahi kutoa zoezi la kuandika insha.

Mwalimu huyo anakumbuka maelezo yaliyoandikwa na Dean Mullins kuhusiana na namna ya kutoa macho kwenye mwili wa mtu aliyekufa.
Katka maelezo yake juu ya nadharia hiyo, Deana aliandika, “Imesemwa kuwa macho ni ufunguo wa rohoni, kwa hiyo kama nikiyachukua macho ya watu waliokufa nitakuwa nimechukua na roho zao pia, napenda sana nadharia hiyo”

Mtuhumiwa mwingine Crystal Sturgil maelezo yake yalikuwa ni yakusikitisha.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa mahakamani, ilibainika kwamba binti huyo alilazimika kukimbia nyumbani kwao na kuishia kuhama hama kutoka kwa ndugu huyu hadi mwingine kutokana na kunyanyaswa kijinsia na baba yake wa kambo.

Karibu watuhumiwa wote walikuwa wanatokea katika familia zilizosambaratika na zilizowapuuza. Lakini hiyo haikumfanya mwanasheria Berckley Bell kuyafumba macho yake dhidi ya yale yaliyofanywa na watuhumiwa hao.

Akizungumzia juu ya adhabu wanayostahili watuhumiwa pindi wakipatikana na hatia, mwanasheria huyo aliitaka mahakama itoe adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa watuhumiwa wanne waliokuwa na umri zaidi ya miaka 18, ambao ni Joseph Risner, Dean Mullins, Crystal Sturgill pamoja na Natasha, na adhabu ya kifungo cha maiasha bila uwezekano wa kupewa msamaha kwa watuhumiwa wawili waliokuwa na umri wa miaka 18 ambao ni Jason Bryant na Karen Howell.

Mnamo February 20, 1998 watuhumiwa wote walifikishwa mahakamani na kusomewa mashitaka na Jaji James Backner.
Jaji Backner alipomaliza kuwasomea mashitaka aliwauliza kama watuhumiwa wote kwa pamoja wanakubaliana na mashitaka yote yaliyosomwa mbele yao au la.

Jibu lililotoka kwa watuhumiwa wote lilikuwa ni “ndiyo tunakubaliana na mashitaka yote tuliyosomewa”

Sikun ya hukumu, Jaji wa mahakama hiyo alisoma hukumi ambapo aliwahukumu watuhumiwa wote kifungo cha maiasha jela bila uwezekano wa msamaha wa parole.

Mara baada ya kumalizika kusomwa kwa hukumu hiyo, dada wa Delfina Lillelid aitwaye Ivette Zelaya alimpongeza jaji kwa kutoa hukumu hiyo, ambayo aliieleza kama adhabu nzuri inayowastahili watuhumiwa zaidi ya kunyongwa.

Akiongea na waandishi wa habari Zelaya alisema , “Ninayo furaha kubwa kwamba vijana hawa hawatapata fursa ya kuishi maisha wanayoyataka kwa kitendo chao cha kudhulumu roho ya dada yangu na familia yake na kuziacha familia zao zikiwa salama”

Aug 15, 2009

WAUAJI WADOGO WA KISHETANI!

Familia ya Lillelid
Wasomaji wapendwa, nimekuwa nikipokea maombi ya wasomaji wa gazeti la Jitambue ambalo limesimama kuchapishwa kutokana na sababu za kiufundi wakitaka nirejee makala zangu za Kesi za Utata ambazo nilikuwa nikiandika katika gazeti hilo.

Naheshimu sana maoni ya wasomaji wangu na kwa kuanzia nimeona nianze na mkasa huu ambao ulitokea nchini marekani mwaka 1997.

Kesi hii niliwahi kuiandika katika gazeti la Jitambue, si vibaya nikirejea Kesi hii wakati nikiandaa makala nyingine.

********************************

Ilikuwa ni jumapili majira ya saa 2:20 usiku, April 6, 1997, kitengo cha ulinzi wa jamii katika mji wa Greene County ulioko jimboni Tennessee nchini Marekani, kilipokea simu kupitia namba ya dharura ya kupokelea matuki ya uhalifu au hatari inayotumika nchini humo.

Mpiga simu alitoa taarifa kuwa katika eneo lao imesikika milio ya bunduki. Iliwachukuw dakika 10 askari wawili waliokuwa zamu katika kitengo hicho, Sajenti Frank Waddell na mkuu wa Kitengo hicho msaidizi Jeff Morgan kufika kwenye eneo la tukio.

Walipofika tu kwenye eneo hilo walipokelewa na hali ya kutisha, kwani kulikuwa na miili ya watu wawili iliyokuwa imelala chini huku ikivuja damu na hivyo kufanya eneo lote la tukio kutapakaa damu.

Miili hiyo ilikuwa imelala pembezoni mwa barabara na ilikuwa ni ya mwanaume na mwanamke. Kwa haraka haraka walionekana kama wanakaribia kufikisha umri wa miaka thelathini au ndio wanatimiza miaka thelathini. Wote wawili walikuwa wamepigwa risasi kadhaa mwilini na walikuwa wameshakufa.

Katika mwili wa mwanamke kulikuwa na mtoto mchanga wa kiume ambaye alikuwa amemlalia mwanamke huyo huku akikoroma na pembeni kidogo kulikuwa na binti wa miaka mitano au sita ambaye naye alikuwa amepigwa risasi, lakini aligundulika kuwa bado yuko hai, ingawa alikuja kufariki saa kadhaa baadae akiwa anatibiwa hospitalini.

Hata hivyo, yule mtoto mchanga ambaye alikuwa amepigwa risasi ya jicho , kama miujiza, madaktari walifanikiwa kuokoa maisha yake. Akieleza hali aliyoikuta katika eneo la tukio mbele ya waandishi wa habari, mkuu wa kitengo cha usalama wa jamii katika eneo hilo Terry Jones, huku akitokwa na machozi alisema “Kwa jinsi tulivyokuta watoto wale ilionekana kama vile walikuwa wamekumbatiwa na wazazi wao kabla hawajakata roho, na ukweli kwamba hatufahamu majina yao au kama ni watu wa familia moja au la”

“hakuna Pochi, vitambulisho, fedha au kitu chcochote kilichopatikana kutoka katika eneo la tukio, ambacho kitaweza kurahisisha kuwatambua wahanga hawa” Aliendelea kufafanua mkuu huyo wa kitengo cha jamii Terry Jones.

Mkuu huyo aliendele kuwaambia waandishi wa habari kuwa hata gari walilokuwa wakisafiria wanafamilia wale nalo halikuwepo katika eneo hilo la tukio.
Akijibu mojawapo ya maswali ya waandishi wa habari, Jones alisema kwamba, hata mwonekano wa familia ile uliashiria kuwa ilikuwa ni familia ya watu wanaoheshimika, hivyo mpaka kufikia hapo wanalichukulia tukio lile kama la mauaji ya kihalifu.

Hata hivyo polisi walikuta gari lingine aina ya Chevrolet likiwa limekwama kwenye mtaro umbali wa mita chache kutoka katika eneo la tukio na namba zake pamoja na vielelezo muhimu vinavyohitajika kuwepo kwenye gari vilikuwa vimeng’olewa, na hata taa ya za mbele za gari hilo zilikuwa bado zinawaka.
Jones aliendelea kusema kuwa anaamini kuwa huenda gari lile aina ya Chevrolet lilikuwa likiendeshwa na wauaji, na analazimika kuamini kuwa wauaaji walikuwa ni zaidi ya mtu mmoja, ambapo waliwalazimisha wanafamilia wale kuendesha gari lao mpaka katika eneo la tukio na baada ya kuwauwa waliamua kutoroka na gari la wanafamilia ile.

Uchunguzi wa awali ulionesha kuwa gari lile la aina ya Chevrolet lilikuwa likimilikiwa na na mama mmoja aitwae Mary Castle, karani wa duka anayeishi Paintsville katika jimbo la Kentucky nchini humo.

Akihojiwa na askari wa upelelezi wa Paintsville aitwae Tom Haney alidai kwamba gari lake liliazimwa na mwanae wa kiume aitwae Joseph Risner (21) siku mbili nyuma na tangu alipochukua gari lake hajapata kumuona, si yeye wala gari. Mama huyo alitoa picha ya mwanae huyo na Haney aliituma kwa njia ya fax haraka kwenda Greene County katika kitengo cha ulinzi wa jamii.

Wakati h huo askari wa Tennessee waliitambua miili ya wanafamilia ile kuwa ni ya Vidar Lillelid aliyekuwa na umri wa miaka 34 mhamiaji kutoka nchini Sweden, mkewe Delfina aliyekuwa na miaka 28, binti yao aitwae Tabitha aliyekuwa na umri wa miaka 6 na mtoto wao mdogo wa kiume aitwae Peter aliyekuwa na umri wa miaka 2.

Familia ile ilikuwa inasafiri ikitokea katika mji wa Johnson ulioko katika jimbo la Kentucky, walikokwenda kuhudhuria mkutano mkuu wa kidini wa dhehebu la mashahidi wa Jehova.

Majira ya sa saba na robo za mchana ikiwa ni kabla ya kutimia masaa 24 tangu tukio lile kuripotiwa gari la Lillelid lilikamatwa na askari wa upande wa Mexico, kutokana na nyaraka za umiliki wa gari lile kutiliwa mashaka na askari wa upande huo.

Watu wote sita waliokuwa wakisafiri na gari hilo wakiwa ni wavulana watatu na wasichana watatu na walikamatwa kwa kutuhumiwa kuiba gari na kuhusika na mauaji ya familia ya Lillelid.

Vijana hao walitambuliwa kwa majina ya Joseph L Risner, aliyekuwa na umri wa miaka 21, Dean Mullins na Karen Howel wote wakiwa na umri wa miaka 20, Natasha Cornet na Crystal Renea Sturgil wakiwa na umri wa miaka 18 na Jason Blake Bryant aliyekuwa na umri wa miaka 15, wote wakiwa ni wakazi wa Paintsville katika jimbo la Kentucky.

Vijana hao walikuwana muonekanao wa kihuni kama walivyo watumiaji wa madawa ya kulevya, kwani walikuwa wamejichora katika miili yao picha za kutisha huku wakiwa wamejitoga masikioni puani,kwenye ulimi, kidevuni, midomoni, kwenye nyusi, na kujivika vipuri, pia walikuwa wamekata nywele zao katika mtindo wa ajabu.

Wapelelezi wa Tennesee walipata shida kidogo katika kufuatilia nyendo za vijana wale kutokea Kentucky hadi katika mpaka wa Mexico. Kwa kmujibu wa maelezo ya watuhumiwa ilionesha kwamba, watuhumiwa wote sita walikutana April 6, 1997 na walipanga kusafiri kwenda katika jimbo la New Orleans ambapo wangekutana na marafiki zao.

Risner aliazima gari la mama yake aina ya Chevrolet na wote sita waliondoka na gari hilo hadi kwa afisa mmoja wa kitengo cha uthibiti wa silaha na kuvuja kasha wakaiba bastola aina ya Caliber namba 25 na makasha mawili ya risasi pamoja na fedha kiasi cha dola 500 za Kimarekani.

Baada ya wizi ule, vijana hao wote sita walisafiri kupitia barabara kuu ya kusini kuelekea jimboni Virginia. Majira ya saa 12:20 za jioni wakiwa wanakatisha viunga vya maeneo ya Virginia walisimamishwa na askari wa usalama barabarani na kutozwa faini kwa kuendesha gari kwa mwendo wa kasi. Risiti waliyopewa baada ya kulipa faini ilikutwa kwenye eneo mla tukio.

Kwa kujibu wa askari wa usalama barabarani wa Virginia walikiri kwamba vijana wale hawakuwa wamelewa wala kuonekana kama walikuwa wametumia dawa za kulevya.

Saa moja baadae gari hilo lilionekana likiwa limeegeshwa kando ya barabara kuu iendayo katika mji wa Greene County Tennesee. Kwa mujibu wa shuhuda aliyeliona gari hilo lililokuwana vijana hao sita, waliokuwa na muonekano wa kihuni alidai kwamba gari hilo lilikaa katika eneo hilo kwa takribani dakika 45.

Wakati huo huo familia ya Lillelid ilikuwa ikisafiri kurejea nyumbani kwao matika mji wa Powell jimboni Tennessee wakiwa katika msafara wa mgari kadhaa yaliyokuwa yakiendeshwa na marafiki zao ambao wote walikuwa wakitokea katika mkutano mkuu wa kidini wa mashahidi wa Jehova.

Inasemekana, Lillelid alikuwa amechoka hivyo akaamua kuegesha gari lake pembeni ya barabara ili apate kupumzika, na kuwaacha rafiki zake wakiendelea na safari. Kumbe wakati Lillelid anaegesha gari lake hakujua kama jirani kulikuwa na gari lingine aina ya Chevrolet limeegeshwa likiw na vijana sita ambao wangekuja kumdhuru.

Mmoja wa mashuhuda alidai kwamba waliwaona watuhumiwa wakiongea na Lillelid na kasha waliyaona magari yote mawili yakiondoka kutoka katika eneo lile.

Polisi wanaamini kwamba huenda gari la Lillelid lilitekwa na watuhumiwa na kundeshwa na mmoja na watuhumiwa hadi katika eneo la tukio ambapio waliwapiga risasi wote na kuwauwa lakini wakimuacha mtoto Peter akiwa amejeruhiwa vibaya.

Huku wakiamini kwamba wamewauwa wote, watuhumiwa waliamua kuondoka na magari yote mawili yaani lile la kwao aina ya Chevrolet pamoja na lile la Lillelid, lakini kutokana na wembamba wa barabara waliyoingia, gari lao lilikwama kwenye mtaro.

Ili kuepuka kupoteza muda waliamua kutelekeza gari lao, lakini kabla ya kulitelekeza gari hilo, waling’oa namba za gari pamoja na nyaraka muhimu ambazo zingefanya gari lile kufahamika mmiliki wake kirahisi. Walichukua fedha, vitu vya thamani na vitambulisho vyote walivyokuwa navyofamilia ya Lillelid ili kuchelewesha kutambuliwa kwao.

Baada ya kukamatwa watuhumiwa wote sita walirejeshwa katika mji wa Greene County Tennessee walikotokea katika jimbo la Arizonana kuwekwa katika gereza kuu la mji huo kwa mahojiano zaidi.

Siku chache baada ya watuhumiwa wote kuwekwa rumande, walikiri kwamba Natasha Cornett ndiye aliyekuwa mkuu wa kikundi na pia msemaji mkuu.

Natasha aliwashangaza askari wa upelelezi pale aliposema kwamba yeye ni mtumishi wa shetaninatasha alifafanua kwamba amekuwa akliwasiliana na shetani tangu akiwa na umri mdogo.

Akihijiwa na polisi kuhusiana na maelezo yake hayo, kwa maneno yake mwenyewe Natasha alisema , “Nadhani nilikuwa naitwa na mtu nisiyemwona, na kulikuwa na roho nisiyoiona ambayo ilikuwa ikizungumza na mimi tangu nikiwa na umri wa miaka miwili. Nimekuwa kwa umri na kimo huku nikiandaliwa kuwa mtumishi wa shetani”

Akjibu mojawapo ya maswali ya askari wa upelelezi, Natasha alikiri kuwa yeye ni mpinzani wa Masihi Yesu Kristo na binti wa shetani.
Natasha alizidi kusisitiza kuwa maisha yake yalitawaliwa na nadharia za ajabu kiasi cha kuasi imani ya kikristo aliyokuwa nayo mama yake.

Maelezo ya Natasha yalitoka katika vyombo vya habari nchini marekani na hivyo kutomfurahisha wakili aliyekuwa akimtetea aitwae Eric Conn. Hata hivyo wakili huyo alimuonya Natasha kutoonge na waandishi wa habari au mtu yeyote kuhusiana na kesi hiyo.

Na ili kujenga mazingira mazuri ya kumtetea mteja wake, wakili huyo aliitisha mkutano wa vyombo vya habari na kukanusha madai yaliyokuwa yakitolewa na mamlaka ya kisheria jimboni Tennessee kwamba mauaji yaliyofanywa na watuhumiwa yalikuwa ni utekelezaji wa imani ya dini ya kishetanina badala yake wakili huyo alisisitiza kwamba watuhumiwa walikuwa na matatizo ya kiakili, ambapo wanalindwa kisheria na kifungu kinachowalinda watu wenye matatizo ya kiakili dhidi ya makosa waliyoyafanya.

“Kila mtu anayeizungumzia kesi hii anaihusisha na dini ya kishetani, hiyo si sahihi hata kidogo,” alikanusha wakili Eric Conn, na hakusita kusema hadharani kuw atatumia kifungu cha sheria kinachowatetea watu wenye matatizo ya kiakili dhidi ya makosa waliyoyafanya.

“Huwezi kuyatenganisha makosa haya na matatizo ya kiakili kwa sababu kulikuwa na nguvu isiyo ya kawaida iliyokuwa ikiwaendesha vijana hawa kufanya yale waliyoyafanya,” alisema wakili huyo.

Hata hivyo pamoja na Natasha kukatazwa kuongea na vyombo vya habariau mtu yeyote kuhusiana na kesi ile, hakuacha kuzungumza na vyombo hivyo kuhusiana na imani yao ya kishetani yeye na watuhumiwa wenzake.

“Kuna wakati najihisi kama nimerukwa na akili, lakini hapana, nadhani mimi sio mwendawazimu” alinukuliwa akisema Natasha.
Kwa mujibu wa rafiki zake Natasha alijulikana kama binti aliyekuwa na tabia ya kuongoza wanaume na tabia hiyo amekuwa nayo hata katika kikundi chao. Natasha alikanusha kwamba alikuwa ni kiongozi wa kundi lao.

“Mimi sikuwa na wafuasi na sisi sio wafuasi wa dini ya kishetani bali ni kikundi cha marafiki tulio na utashi w aina moja” alisema Natasha.
Akizungumzia juu ya minong’ono iliyoanza kuenea kwamba, yeye Natasha alikuwa na uhusiano maalum wa kusagana na mtuhumiwa mwenzie Karen Howell, lakini tuhuma hizo alizikanusha pia.

Akizungumza juu ya minong’ono hiyo, Natasha alisema, “Karen ni rafiki yangu wa karibu na sio urafiki wa kusagana. Kwa kawaida huwa tunabusiana lakini sio kama mnavyofikiria”

Natasha aliongeza kuwa alikuwa na mpango unaoratibiwa na shetani wa kuwaandaa vijana wote duniani ili waasi. Alidai kwamba vita ya mwisho ya Armageddon iko karibu kuanza lakini baba yao shetani hajawaambia tarehe maalum vita hiyo itakapoanza, na aliwaomba waandishi wa habari wawatangazie watoto wote ulimwenguni kusimamia haki na imani zao kwa kuzipigania kwa jinsi watakavyoweza. (Armageddon ni vita takatifu vilivyozungumziwa katika Biblia agano jipya itakavyopiganwa mwiso wa dunia kati ya wafuasi wa shetani na watakatifu kwa mujibu wa maandiko ndani ya Biblia)

Natasha aliongeza kusema kuwa anamwamini wakili wake Eric Conn na nguvu za shetani, “ naamini baba yangu shetani atanisaidia na kunilinda” alisema Natasha.


ITAENDELEA..............................

Aug 2, 2009

KUFANIKIWA AU KUTOFANIKIWA NI UCHAGUZI WETU WENYEWE

Ukiamini utafanikiwa

Ili kufanikiwa kwenye lengo lolote katika maisha, ni lazima uamini kwamba utafanikiwa. Kama usipofanya hivyo, una nafasi kubwa ya kushindwa.
Unaweza kuwa na malengo mapya uliyoyapanga na ambayo unaanza kujaribu kuyatekeleza. Lakini ni lazima ufanye hivyo ukiwa na imani kubwa kwamba utafanikiwa.
Waweza kuona kazi uliyo nayo hivi sasa haikusaidii sana na hivyo kuamua ghafla kuiacha.
Waweza kufanya hivyo huku ukiwa hujaamua kitu gani cha kufanya, na hivyo kulazimika kutumia kipindi cha pengine miezi sita ama hata zaidi inayofuata kujaribu kufikiria nini cha kufanya.


Huwezi kufanikiwa katika kile unachokitaka kufanya ikiwa hutaamua kuyafanya mawazo yako hayo uliyonayo kuwa vitendo. Hata ukiwa na kiu na hamu kubwa kiasi gani ya kufanikiwa, bila kuhamasisha nafsi yako na kuanza kufuatilia lile unalotaka kulifanya, kufanikiwa itakuwa ndoto kwako. Hilo litashusha ari yako na kujikuta unarudi kulekule ulikotoka, kwenye kazi ya kuajiriwa.
Lakini wakati wote huu, vyanzo vya mafanikio huwepo karibu nawe tayari kutumiwa nawe kwa ajili ya kukuletea mafanikio unayoyataka. Lakini bila kuiamini nafsi yako kwamba unaweza kufanikiwa, huwezi kufanikiwa.


Hivyo ni lazima ujifikirie katika mambo unayoyafanya, unafanya mambo yako yanayokuelekeza kwenye malengo yako ukiwa na imani kwamba utafanikiwa. Je, unayo picha ya mafanikio yako akilini mwako na hisia kwamba hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa?
Hebu kaa chini na ufikirie kuhusu mambo uliyowahi kuyafanya na ukashindwa katika kipindi cha miaka michache iliyopita. Jiulize ikiwa kweli ulijiamini kwa dhati kwamba utafanikiwa.
Mara nyingi utakuta katika matukio hayo ulikuwa na mashaka ndani yako kuhusiana na uwezo wako wa kufanikiwa na hivyo iko haja ya kujihamasisha kabla ya kuanza kupiga hatua kuelekea kwenye lengo lako. Unatakiwa kuamini kwamba utafanikiwa.


Ni kwa nini imani hiyo ni muhimu kiasi hicho? Kwa kawaida huwa tunaanza kujenga imani tangu tukiwa wadogo. Mara baada ya kuzaliwa kwetu, huanza kujenga au kujengewa imani.
Na baadaye tunaendelea kujijengea imani wakati tukiendelea kukua na huwa tunabadili imani kutoka za zamani na kujenga mpya, kutegemea vitu vingi. Tunahitaji kufanya haya ili kuyafanya maisha yetu hapa duniani yawe rahisi na ya kweli.


Siku zote tunaamini kwamba tunapoamka vitandani mwetu asubuhi, tunahitajika kuweka miguu yetu chini ili kuweza kusimama ardhini kabla ya kuendelea na shughuli zetu nyingine na si kuruka hewani hadi kwenye dari ili kuweza kutoka vyumbani mwetu kwa shughuli zetu za kawaida.


Tumejifunza hili tangu tukiwa wadogo kabisa na sasa hatuna haja hata ya kufikiria kila siku kwamba hivyo ndivyo tunavyotakiwa kufanya. Vivyo hivyo, pia hatuna haja ya kufikiria ni kwa kiasi gani nguvu ya uvutano ina mchango gani katika kusimama kwetu kila asubuhi tangu tunapoamka vitandani mwetu.


Wakati unapofungua mlango wa nyumba yako, unageuza ufunguo wako kuelekea upande uliko ubao wa kufungia mlango ama upande wa tofauti na mwenendo wa mikono ya saa.
Hiyo ni imani tunayojijengea tangu tukiwa watoto wadogo kabisa, tunapoanza kujifunza kufungua na kufunga milango.


Kila unapokutana na mlango mpya hatuwi na wasiwasi kwamba tunajua vile mlango unavyofunguka kwani tunakuwa na hakika (akilini mwetu) na namna mlango huo utakavyofunguka. Tunazunguusha funguo kuelekea upande uliko mlango tu! Ni rahisi. Hiyo ndiyo imani tuliyonayo.


Huoni sababu ya kufikiria uwezekano wa kukutana na mlango unaofunguka vinginevyo. Lakini hakuna atakayekataa kwamba wengi tumewahi kukutana na milango inayofunguka kwa mwelekeo tofauti na ule tunaoamini ndio utaratibu ‘unaokubalika.’ Inaudhi sana unapokutana nao kwa mara ya kwanza.


Hata baada ya mwaka mzima wa kufungua mlango kwa mwelekeo huo, bado imani uliyojijengea kutokana na uzoefu wako kwamba mlango haufunguki kwa mwelekeo huo, utakuwa nayo, na hivyo utakuwa ukikasirika kila mara utakapofungua mlango huo. Imani unayojijengea moja kwa moja huathiri tabia yako, hata kama imani hiyo si sahihi kama unavyofikiria.
Hebu tufikirie kitu kingine! Dunia ni duara ama si duara? Umelijuaje hili? Si kwamba umeambiwa na watu tu? Una uhakika gani? Wapo wanaoamini kwamba dunia ni ya ubapa kutokana na wanavyoiona kila wanapochungulia madirishani.


Kama ungeamini kwamba dunia ni ya ubapa, ni wazi ungepatwa na wasiwasi mkubwa wakati unaposafiri kwenye mashua kwamba huenda mngefika mwisho na kuangukia nje ya dunia. Lakini hivi ndivyo watu walivyokuwa wakifikiria. Kilikuwa ni kikwazo kikubwa kwa ugunduzi kwa miaka mingi ya mwanzoni. Imani waliyokuwa nayo watu moja kwa moja iliathiri vitendo vyao, na hilo lilikwaza matokeo yao. Fahamu tena kwamba imani si lazima zioneshe ukweli uliopo duniani. Si kila siku milango hufunguliwa kuelekea mwelekeo uliko mlango.
Imani kuhusu dunia kuwa ubapa ilibadilishwa mara wagunduzi walipoanza kuzunguuka dunia. Imani huathiri moja kwa moja matendo yetu hata hivyo. Wakati mwingine, tunachukua hatua hata imani zetu zinapokuwa si sahihi, na hii yaweza kutukwaza. Hii ni kweli kuhusiana na imani tulizonazo kuhusu nafsi zetu na uwezo wetu.


Vipi kuhusu nafsi zetu? Kama tufanyavyo mambo tuliyoyazoea bila kufikiria kutokana na imani tunazojijengea kama vile kufungua mlango, tunafanya hivyo hivyo kutokana na imani tunazojijengea kuhusu nafsi zetu. Ikiwa tutajenga imani za kutukwaza kuhusiana na nini kinawezekana kufanikisha, jibu letu litakuwa kukwamisha matokeo ya vitendo vyetu tunavyochukua. Matokeo yake tunakwaza pia matokeo tunayoyapata.


Ikiwa tunaamini kwamba kuna kila uwezekano wa kushindwa katika kile tunachofanya mawazo yetu ya kina (subconscious mind), itafanya kazi ya kujenga mazingira yatakayounga mkono imani yetu hii. Wakati mambo yanapokuwa magumu, hatutakuwa na haja ya kufanya jitihada zaidi iliyo muhimu katika kufanikiwa; kushindwa kwa mara ya kwanza kutaunga mkono imani yetu hiyo na hivyo kutufanya tukate tamaa na kuachana na kile tunachofanya.

Jul 27, 2009

MABINTI HAWA HUOLEWA NA BABA ZAO

Huolewa na baba zao
Kila jamii ina visa asili, yaani imani ambazo zinaonekana kama kweli, wakati hazina ushahidi wa aina yoyote kuwa zina ukweli. Lakini, kila kisa asili, kina chimbuko lake. Chimbuko hilo husema kuhusu ambavyo jamii hiyo imekuwa ikiyatafsiri mambo.

Moja ya visa asili katika jamii yetu na jamii nyingine duniani ni kwamba, mwanamke anapoolewa na mwanamume na wakaishi kwa muda mrefu, hatimaye watu hao hutokea wakafanana sura.
Lakini, je kuina ukweli wowote katika jambo hili? Jibu ni kwamba, kuna ukweli ambao hata hivyo unahitaji maelezo zaidi ya yale ambayo tumeyazoea, yasiyo na uchambuzi.
Ni kweli, kuna wanawake ambao wanafanana sura na wanaume ambao wako nao kwenye ndoa.
Hata hivyo, suala la kuishi kwa muda mrefu halina ukweli. Kufanana kwa mke na mume huweza kujitokeza hata kabla hawajaoana.

Si watu wengi ambao wanajua kwamba, baba anapokuwa anampiga mama, yaani mkewe, watoto wanapoona vipigo hivyo, huathirika na wanakuja kutumia uzoefu huo ukubwani. Kama mume anampiga mkewe mara kwa mara kwa mfano, watoto wa kiume kwenye familia hii, wako kwenye uwezekano mkubwa sana wa kuja kuwapiga wake zao.

Tafiti nyingi zinaonesha kwamba, wanaume ambao huwapiga wake zao, wanane kati ya kila kumi walishuhudia baba zao au walezi wao wa kiume wakiwapiga wake zao.
Lakini, pia inaonesha kwamba, wale watoto wa kike ambao waliona mama zao wakipigwa na baba zao, wako kwenye nafasi kubwa ya kuja kuolewa na wanaume ambao nao wanapiga.
Kinachotokea ni kwamba, watoto hawa wa kike, ukubwani hutafuta wanaume ambao wana tabia kama za baba zao, wakiamini bila wenyewe kujua kwamba, wakiwapata wanaume hao watalipiza namna mama zao walivyofanyiwa na baba zao.

Bahati mbaya, badala ya kulipiza, hujikuta wanashindwa kutoka kwenye uhusiano huo wa mateso kwa visingizio mbalimbali. Hii hata hivyo, haina maana kwamba, wanawake wote wanaoteswa kwenye uhusiano wanaendelea kukaa humo kwa sababu hii. Wengine hukaa humo kutokana na utegemezi wa kihisia au kutokana na kutojiamini na hata sababu za kijamii, zikiwemo imani za dini.

Hata hivyo, wataalamu wamegundua kwamba, suala sasa siyo baba kumpiga mama peke yake, bali uhusiano kati ya mtoto wa kike na baba yake. Inaelezwa kwenye tafiti kadhaa kwamba, kama mtoto wa kike anaelewana vizuri sana na baba yake, kuna uwezekano mkubwa kwamba, mtoto huyo atakuja kuolewa na mtu ambaye anafanana na baba huyo.
Awali, tafiti zilipoonesha uwezekano huo, ilionekana kama porojo, lakini hivi karibuni jambo hilo limethibitishwa na vyombo vingi vya kiutafiti.
Hii imefanyika baada ya vyombo hivyo kuwatumia wanawake wengi katika kujaribu kuthibitisha jambo hilo.

Taarifa za kitafiti ambazo zimeripotiwa kwenye jarida la Evolution and Human Behavior, zinaonesha kwamba, mtoto wa kike ambaye ana uelewano wa karibu sana na baba yake utotoni, akija kuwa mkubwa, bila kujua atakuja kuvutwa na mtu ambaye anafanana sura na huyo baba yake.
Baadhi ya watafiti wanasema, labda hapo ndipo mahali ambapo panachimbuka ile imani kwamba, mtu na mkewe wakiishi kwa muda mrefu huja kufanana.
Pengine siyo suala la muda mrefu, bali zaidi ni kwamba, mwanamke ambaye anafanana na mumewe ni mwanamke ambaye alipokuwa mdogo alipendwa au kuelewana sana na baba yake.
Watafiti wengi waliofanyia kazi suala hili wanasema wamegundua kwamba, mtoto wa kike ambaye hakuwa na uelewano mzuri na baba yake, kwa kawaida havutwi kabisa na wanaume ambao wana sura kama ya baba yake.

Labda hii inaweza pia kuelezea ni kwa nini baadhi ya wanawake wazuri sana huolewa na wanaume ambao ni wabaya wa sura (kama jamii inavyowahukumu). Ni kwamba, inawezekana baba yake msichana alikuwa na sura nzuri na hawakuwa na uhusiano mzuri. Ni wazi, mwanamume mwenye sura ya aina ya baba yake hatamvuta. Lakini, hapa inategemea uzuri huo ulikuwaje, kwa sababu anachofuata msichana siyo uzuri au ubaya wa sura, bali sura inayofanana na ya baba yake au isiyofanana na ya baba yake.

Lakini, kama mtoto wa kike alielewana sana na baba yake ambaye ana sura mbaya kwa mujibu wa vipimo vya jamii, atajikuta akivutwa na wanaume wenye sura kama ya baba yake (mbaya) ambapo itakuwa rahisi kwake kuolewa na mmoja kati yao na siyo na wale wenye sura nzuri.
Hebu fikiria kuhusu mtoto wa kike ambaye anafanana na baba yake, halafu anaelewana sana na huyo baba.

Ina maana kwamba, atakuja kuolewa na mwanamume ambaye siyo tu kwamba, anafanana na baba yake, lakini pia ambaye anafanana naye (mwanamke). Kwa kuwa kuna idadi kubwa ya watoto wa kike wanaofanana sura na kuelewana na baba zao, ina maana ndoa za wanaofanana nazo ni nyingi. Lakini, je utafiti huu unataka kuwafundisha wale akina baba ambao jamii inawahukumu kwamba, wana sura mbaya, kutokuwa karibu na watoto wao wa kike ili kuwaepusha kuja kuolewa na wanaume wenye sura kama zao? Bila shaka hilo si lengo la utafiti huu.

Ukweli ni kwamba, kama msichana amempenda mwanamume, maana yake ameona kwake ni mzuri, tofauti na jamii inavyoona.
Kama jamii imepanga viwango vya uzuri na ubaya, ni suala la mtu kuviamini au kutoviamini viwango hivyo. Watafiti wote wanakubaliana jambo moja kwenye utafiti huu, kwamba huenda wanawake huchagua wenza kwa kigezo hiki cha maelewano yao yalivyokuwa na wazazi wao.
Ni kwamba, mwanamke anaweza kumwona mwanamume mwenye sura nzuri, ambayo pengine ni kinyume na ile ya baba yake (mbaya), na akajua kwamba ni sura nzuri.

Lakini, linapokuja suala la kuoa, akachagua sura mbaya ambayo ni ya baba yake. Ninaposema sura nzuri au mbaya, ninazungumzia jamii inavyoona, kwani ukweli ni kwamba, hakuna sura mbaya au nzuri, bali mtu mwenyewe anayetazama anavyoona.
Inaelezwa kwamba, suala ni yupi mzuri kwenye ubongo wa binadamu, halipangwi na wale tunaowaona, bali zaidi hupangwa na wale ambao tulikuwa na uhusiano nao wa dhati na mzuri sana tulipokuwa wadogo. Hapa, baba kwa mtoto wa kike ndivyo ilivyo.
Makala hii iliwahi kuandikwa katika gazeti la Jitambue.

Jul 18, 2009

HIVI KUNA UKWELI KWAMBA WANAWAKE WALIOAJIRIWA HUJITONGOZESHA KWA MABOSI?

Eti hujitongozesha kwa mabosi!!!

Kuna dhana kwamba wanawake walioajiriwa wanakabiliwa na mazingira ambayo yanawalazimisha kuingia kwenye vitendo vya kutoka nje ya ndoa zao, ukilinganisha na wanawake ambao hawajaajiriwa hususani mama wa nyumbani jambo ambalo katika maisha ya kawaida bila utafiti linaonekana kama vile ni kinyume yaani akina mama walio majumbani ndio ambao hutoka nje zaidi.

Niliwahi kuwahoji wanawake kadhaa jijini Dar, mwanamke mmoja kati ya watano alikiri kwamba yuko tayari kujitongozesha kwa bosi ili kujaribu kulinda nafasi yake kazini au kupandishwa cheo. Nilifanya mahojiano hayo ili kujua idadi wanaume wanaotumia nafasi zao kazini kuwadhalilisha wanawake kijinsia.

Lakini bila shaka suala la mapenzi kwa wanawake walioajiriwa lina nguvu na kwa hiyo limekuwa likifanyiwa tafiti katika sehemu mbalimbali duniani. Tofauti na tafiti ambazo zimefanywa hivi karibuni zinaonyesha kwamba mwanamke mmoja kati ya kumi walioajiriwa huwa anaonyesha tabia za kimapenzi au kujitongozesha kwa bosi wake.

Tafiti hizi zinaonyesha kuwa yule mmoja kati ya kumi ambaye hujitongozesha kwa bosi huishia kutembea naye au hata kuolewa naye kama hana mume na pengine kuvunja ndoa yake. Inaelezwa pia kuwa mmoja kati ya wanawake kumi wanaojitongozesha kwa mabosi huwa anapandishwa cheo. Hii ina maana kwamba wanawake wanaopandishwa vyeo kwenye maeneo ya kazi huenda mmoja kati ya kila kumi hupandishwa kwa sababu za kimapenzi hata hivyo siyo lazima iwe hivyo.

Katika mahojiano na jarida moja nchini Marekani mwanamke mmoja kati ya watano alikiri kwamba yuko tayari kujitongozesha kwa bosi ili kujaribu kulinda nafasi yake kazini au kupandishwa cheo. Jarida hilo halikufanya mahojiani ili kujua idadi wanaume wanaotumia nafasi zao kazini kuwadhalilisha wanawake kijinsia.

Wanawake wenye watoto ambao walihojiwa kwenye tafiti hizo walisema kwamba ajira zinawasumbua na wamefikiria kuwa ni ngumu kujigawa kazini na nyumbani kishughuli.

Tafiti hizo hata hivyo hazikulenga katika kuonyesha kwamba wanawake ni dhaifu bali huenda zimelenga katika kuonyesha kwamba idadi ya wanawake wanaojitongozesha kwa mabosi ni ndogo kuliko inavyotazamwa au kuaminika na pia kuonyesha kwamba bado wanawake walioajiriwa wako kwenye nafasi kubwa zaidi kushiriki mapenzi kuliko wale walioko majumbani. Ni juu ya wanawake ambao wanadhani ni halali kuuza thamani zao kwa ajili ya kazi kubadili mwenendo huo..

Jul 10, 2009

NI MAREHEMU KATIKA MWILI MWINGINE?

Hivi huyu nishamuona wapi?

Kuna wakati unakuwa mahali, halafu unahisi kwamba ulishakuwa mahali hapo kabla, na pengine ukiwa na watu wale wale. Lakini, kwa unavjojua, hujawahi kuwepo hapo, wala kuwa na kuwa na watu hao.

Hali ya uzoefu huu kufahamika kitaalamu kama Déjà vu. Kama nilivyosema awali kwamba, unakuwa katika sehemu ngeni unashangaa kuona kama kwamba, ulishawahi kwenda sehemu hiyo huko nyuma.

Unaona na mtu kwa mara ya kwanza lakini unapata mawazo kama uliwahi kuonana naye huko nyuma. Hiyo ndiyo Déjà vu.

Neno Déjà vu, asili yake ni lugha ya kifaransa ikiwa na maana kwamba, Tayari nilishawahi kumuona au mahali hapa niliwahi kupaona kabla, ikiwa na maana kwamba mtu anakutana na kitu kipya katika mazingira mapya na anagundua kwamba aliwahi kukumbana na hicho kitu kabla, pengine katika mazingira hayo hayo.

Inasemekana kwamba, mambo haya ya Déjà vu ni ya kawaida. Kila watu saba katika kial kumi wanasema kwamba waliwahi kuukumbana nayo angalau mara moja katika maisha yao.

Neno hili Déjà vu lilitumiwa kwa mara ya kwanza na Emile Boirac (1851-1917), ambaye alikuwa mtafiti wa Kifaransa wa mambo ya akili za ziada za watu. Kuna maelezo mengi ya uzoefu huu, kama ifuatavyo: Unakutana napicha kwa mara ya kwanza lakini unagundua kwamba uliwahi kuiona zamani.

Unafika mahali pageni na unagundua kwamba, mahali pale si pageni bali uliwahi kufika kabla. Lakini, kwa akili ya kawaida, unakumbuka kwamba hujwahi kufika hapo. Unaiona sinema mpya lakini unahisi kwamba uliwahi kuiona kabla. Na cha kushangaza ni kwamba unaweza hata kutabiri kitendo kitakachofuata na ikawa kweli, lakini hukumbuki na pengine hujawahi kuiona, kwani ni sinema mpya.

Unakumbana na hali fulani au unafika mahali fulani pageni lakini unagundua kwamba hali ile au mahali pale uliwahi kupaona katika ndoto zako huko nyuma.
Déjà vu pia inaweza ikaonekana katika unusaji, ladha ya chakula, mchanganyiko wa rangi, sauti ya juu au ya chini, kelele au kitu chochote ambacho kinafukua kumbukumbu ya mambo ya zamani.

Mtu mgeni aliye mmbele yako uvaaji wake na namna anavyoongea anaweza kukukumbusha mtu uliyekuwa umekutana naye kabla. Baadhi ya watu wanasema kwamba hali hii ya kufanana inaweza kusababishwa na hali ya ubongo kwa wakati huo.

Watu wanaamini kwamba binadamu baada ya kufa roho yake inaingia katika mwili wa mwingine, wanasema kwamba kwa mujibu wa Déjà vu waliwahi kukumbana na hali kama hiyo zamani. Kunaweza kukawa na sababu na maelezo chungu nzima kuhusu Déjà vu.

Jun 25, 2009

FEDHA ZINAPOGEUZWA MHIMILI MKUU KATIKA MAISHA

Hata uwe na fedha kiasi gani haziwezi kukupa furaha

Kuna imani zisizo sahihi zilizoenea kuhusu pesa ambazo miongoni mwa imani hizo ni zile zinazodai kwamba utajiri hutuongoza kwenye amani ndani ya nafsi zetu, na kutupatia furaha, faraja, heshima na thamani ya nafsi zetu.

Katika tamaduni zinazo abudu majivuno na si maadili, na zinazoheshimu vitu vyenye thamani isiyo ya kudumu, yaani thamani ya nje, ni rahisi kudhani yule mwenye vitu vingi vya kuchezea anaishi vizuri zaidi ya yule mwenye kutafuta maisha ya msingi na ya furaha zaidi.

Bila kujua tunachagua fedha, hiki kifaa cha kuchezea tunachokiona muhimu sana kwa maisha yetu, kuliko maisha ya kiroho, kwa kuamini kwamba fedha ni tiba na ni jibu kwa matatizo yetu yote. Kumbuka, nikisema maisha ya kiroho, sina maana maisha ya kidini. Nina maanisha maisha ya kutambua jambo kubwa kuliko wewe mwenyewe.

Haishangazi kuona harakati za kutafuta vitu visivyo muhimu vya thamani, huwa ndilo jambo tunalolipa umuhimu zaidi. Tunakua tayari kujitoa mhanga katika mengi ili kutafuta fedha (tunakua tayari hata kuhatarisha ama kupoteza roho zetu za thamani kubwa katika kutafuta vitu vya thamani ambavyo tunadhani ni vya muhimu na vyenye thamani hata kushinda roho zetu), lakini badae tunagundua kwamba haikupaswa iwe hivyo.

Tunapogundua kwamba tunafika huko hatupati furaha tunayotarajia, hutufanya tutambue kwamba cha muhimu ni furaha na si fedha kama tulivyodhani.

Imani nyingine siyo sahihi, inatokana na baadhi ya vitabu vya dini, kwamba fedha ndio msingi wa maovu yote duniani (kama vile hakuna kitu chochote cha thamani zaidi ya kuwa maskini wenye kushindwa kujisaidia hata katika matatizo madogo na ya familia yake, acha ya jamii yako).

Kutokana na imani hiyo, baadhi ya watu hujijengea tabia ya kuchukia fedha na kutoa shutuma kubwa kwa fedha.

Hata hivyo tatizo la kweli si fedha, bali ni choyo, ubinafsi na uroho wa fedha (uroho wa fedha unaowafanya watu kutumia njia zozote hata za hatari katika kuipata), ndicho kiini cha maovu yote duniani.

Fedha huandamana na malengo ili iweze kuwa na nguvu kuleta mabadiliko katika maisha ya watu. Wakati kile tunachofanya nacho kinahisia za malengo yaliyopandikizwa na kupewa uhusiano wa lazima na fedha, ndio sababu inayozusha mchakato wa hatari wa kutafuta fedha kiasi kwamba hivi sasa hatua hizo zinaonekana kama malengo yenye sababu na ya muhimu ingawa yanaumiza.

Fedha ambayo kwa kweli ni kitu kilicho huru, haina haja ya kuabudiwa, wala kupotezwa hovyo. Tunachotakiwa ni kuifurahia na kuitumia kwa busara na ni bora ikiwa itatumika kwa malengo muhimu. Ni ukweli ulio wazi kwamba, huwezi kuondoka duniani na fedha uliyoichuma kwenda nayo kwenye maisha baada ya kifo, na kwa ukweli fedha hukupatia uhakika wa usalama usio na ukweli.

Maisha yanaweza kwa kuonekana magumu, na ukweli kwamba kwa jinsi unavyokua kwenye kiwango cha juu ya fedha, ndiyo inavyokua na uwezekano mkubwa kuzama kwenye mambo machafu, yanayokuondolea furaha.

Ni vema tukaepuka kuweka uzito mkubwa kwa fedha, iwezayo kuja na kuondoka, na tukatoa umuhimu katika makuzi ya kiroho, jambo ambalo haliwezi kubadilishwa wala kuchukuliwa na watu wa nje na inakupa ushindi bila kujali kule maisha yanapokupeleka.

Inatakiwa kuwepo sababu Ni wazi hakuna mtu anayeishi huku akifikiria kwamba lengo lake la maisha ni kufikiria ni ace cream au ni peremende ama keki ngapi atakula kabla ya kufikiri. Hivyo ndivyo kuna ulazima wa mtu kukaa chini na kufikiria ni kitu gani kilicho muhimu kwa maisha yake.

Jiulize ikiwa kile unacho kifanya kinakuelekeza kwenye kutimiza lengo la kuwepo kwako duniani au kinakupeleka njia iayo sahihi.

Kumbuka duniani unapoishi hakuna nafasi ya kufanya majaribio ya kuishi kabla hujaingia kwenye maisha halisi ya dunia bali hapa ndio nafasi yako pekee na ya mwisho ya kuishi duniani.

Pengine kitu kinachoweza kukupa uwazi zaidi ni kujiuliza kila siku kabla ya kufumba macho yako na kulala. ‘Ninaishi ili nifanye kazi ama ninafanya kazi ili niweze kuendelea kuishi?’.

Njia nyingine ni kutambua kile unachokiona cha thamani zaidi katika maisha yako na hili unaliweza kwa kujiuliza . ‘Nini ningefanya kama ningepewa taarifa kwamba nina miezi sita tu iliyobakiya kuishi?’ Hii itakusaidia kuepuka makosa yaliyofanywa na watu wenye fedha, watu wa kundi la walionacho walioamini ni lazima wawe wanachama wa vilabu vya walio na fedha ili waweze kuishi.

Kwa vile kitu chochote kikizidi sana hugeuka laana, kuweka usawa ni jambo muhimu. Toa nafasi sawa katika mambo yako ya kidunia na kutafuta fedha na ya kiroho. Narudia tena nikisema kiroho sizungumzii dini, ingawa inaweza kuhusika. Nazungumzia kujua lengo lako maishani na kuifanya dunia kua mahali bora pa kuishi, kwako na wengine wote.

Tunapo weza kuweka uwiano wa utafutaji wetu wa dunia na kiroho, maisha yanakua ya furaha ya kweli na yanakua na udhoefu wa kuridhika tutakaofurahia kuishi ndani yake.

Kwa kufanya hivyo tunajipatia zawadi kubwa kushinda zote ambayo ni amani na utulivu akilini na furaha ya kweli inatotokana na kujua kwamba sababu ya maisha ni kitu fulani hata ikiwa tutamsaidia mtu na kufanya maisha yetu yabadilike bila kujali mchango huo ni wa kinyenyekevu kiasi gani.

Wazo hili hueleweka zaidi kwa kutumia maneno ya Ralph Waldo Emerson aliyewahi kusema ‘maisha ya mtu huwa mazuri zaidi unapojua mwingine ameweza kupumua kwa urahisi zaidi kwa vile yeye anaishi huku ni kufanikiwa.

Nani aliyesema huwezi kuwa na vyote? Ni wazi unaweza. Ukweli ni kwamba, hali asilia ya roho zetu ni ya matumaini kamili, ikiwa imetawaliwa na maana halisi ya furaha ya kweli na kuridhika.

Cha muhimu ni kuweka uwiano mzuri kati ya utafutaji wako wa utajiri wa kidunia na dunia ya kiroho. Kumbuka ya fedha ni huduma na ipo kwa ajili ya kuhudumia na si vinginevyo.

Wakati fedha inapopatikana katika njia za kizamani, (kwa njia za uaminifu na haki) kutumika kama chombo muhimu cha kuondoa tofauti, maisha yanakua ni uzoefu wa kusisimua badala ya kua tatizo linalohitaji kutatuliwa. Na hiyo ndiyo siri kubwa iliyofichwa yakutafuta heshima na matumaini.