0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Nov 8, 2009

HANDSOME ALIYEITIKISA KENYA-SEHEMU YA MWISHO.....

Simon Matheri Ikere

Mwili wa Simon Matheri baada ya kuuawa

Ndugu wasomaji wa Blog hii, nimekuwa nikipokea ujumbe kupitia simu yangu ya kiganjani kutoka kwa wasomaji wakinishauri kuwa nisiwe nachelewa kuweka muendelezo wa visa na stori ninazoweka humu na pia nisiwe nachelewa ku up date blog hii mara kwa mara.
Naomba nikiri kuwa, hiyo imetokana na mlundikano wa majukumu niliyo nayo kwa sasa, naomba mniwie radhi, na nitajitahidi kuweka mada mbali mbali humu kama kawaida.
Pia ningependa kuweka wazi kuwa hizi kesi au habari za kiuhalifu ninazoweka humu pamoja na ushuhuda sio habari au visa vya kufikirika bali ni habari za kweli kabisa.
Haya, sasa tuendelee ya ile habari ya kule nchini Kenya………

ILIPOISHIA…..
Kitendo cha kuchoma nyumba yake mwenyewe ambayo aliijenga kwa msaada wa baba yake, kilimuuzi sana mzazi huyo na hivyo kumfungulia mashtaka ambapo alifungwa miaka mitano jela.

ENDELEA….

Matheri alitumikia kifungo chake cha maiak mitano katika jela yenye ulinzi mkali ya Kaimiti ambayo hutumika kwa wafungwa sugu wa ujambazi. Katika kipindi ambacho alikuwa jela, huku nyuma familia yake iliishi kwa amani, ambayo hata hivyo ilitoweka mara baada ya Matheri kuachiwa huru kutokana na kumaliza kifungo chake.

Awali wazazi wake walidhani alikuwa amebadilika kitabia kutokana na kutumikia kifungo cha miaka mitanojela, kitu ambacho haikuwa sahihi. Kumbe katika kipindi hicho ambacho alikuwa akitumikia kifungo ndipo alipo alipohitimu na kuwa jambazi sugu.

Baba yake alikiri kwambanaamini mwanaye alifuzu kuwa mwizi na jambazi sugu kwa kufunzwa wakati alipokuwa katika jela ya kamiti, jela amayo hutumika kuwafunga wahalifu sugu. Baada ya kutoka jela, baba yake aliamua kumjengea mwanaye huyo nyumba mpya akiamini kwamba atakuw aamebadilika, lakini hali ilikuwa tofauti, na nyumba hiyo badaye ilikuja kuchomwa moto na na watu wenye hasira kali kutokana na kukerwa na vitendo vyake.

Alipotoka jela tu Matheri alinunua bunduki aina ya AK-47 kutoka kwa wakimbizi wa Somalia na katika hali isiyo ya kawaida, alimtishia kaka yake kwa bunduki hiyo baada ya kutofautiana katika mambo ya kawaida tu. Baada ya mkasa huo, ilibbbidi familia ilifahamishe jeshi la Polisi, ambapo Polisi walianza kumtafuta. Kama vile machale yalimcheza, Matheri alitowerka haraka sana pale nyumbani kwao na akawa anakuja pale mara chache sana tena usiku wa manane.

Pilika zake za ujambazi zilianzia katika wilaya ya Murang’a. Akiwa na washirika wake, Matheri aliendesha ujambazi katika wilaya hiyo, mpaka alipokoswakoswa kuuwawa na Polisi katika msitu mmoja ambapo walikuw awakifuatiliwa na Polisi ambao walikuwa wanatumia mbwa wa kunusa. Katika tukio hilo washirika wake wawili waliuawa nay eye aliponea chupuchupu baada ya kujitumbukiza katika mtowenye maji yaendayo kwa kasina kupotelea kusikojulikana.

Baada ya tukio hili Matheri alihamishia makazi yake katika jiji la Nairobi ambapo pia alikuwa akitoka na kuingia katika miji mikuu ya Afrika Mashariki na kufnya uharamia na kisha kutoweka kutoka mji mmoja hadi mwingineili kuwakwepa Polisi.

Katika kipindi ambacho Matheri aliendesha uharamia katika wilaya ya Murang’a, familia yake nayo haikusalimika. Mara nyingi familia hiyo ilivamiwa na wannchi wenye hasira kali na kuchomewa nyumba ili kulipiza kisasi. Mzee Ikere alidai kwamba kila wakti mtu anapovamiwa na majambazi katika miji ya Nairobi, Mombasa, Kisumu au mji wowote, Familia yake ilikuwa ikipata usumbufu mkubwa, kwani walikuwa wakipata wageni ambao huja kulipiza kisasi kwa kufanya uharibifu mkubwa ikiwa ni pamoja na kuchoma nyumba za familia hiyo.

Ilifikia mahali hata wizi mdogo mdogo wa kuku, jina la mwanye lilihusishwa na wizi huo, kitu ambacho haikuwa kweli. Tukio ambalo Mzee Ikere anasema hatalisahau ni pale aliposhambuliwa kwa mapanga na mikuki na watu wenye hasira kali ikiwa ni katika kulipiza kisasi, kiasi kwamba aliachwa na majeraha huku akivuja damu bila kupata msaada wowote kutoka kwa majirani zake. Ilitokea hata watu wenye magari waliotaka kumpa msada ili kumpeleka hospitalini walikuwa wakitishwa kwamba nao wangeshughulikiwa. Kutokana na usumbufu huo, ilibidi waombe msaada polisi ili familia hiyo ipate msaada wa ulinzi lakini hawakupata msaada huo.

Hadi kufikia mwaka 2007, jina la Simon Matheri Ikere lilikuwa likivuma nchini Kenya kutokana na uhalifu aliokuwa akiundesha yeye na genge lake. Lakini kama waswahili wanvyosema, hakuna marefu yasiyo na ncha. Ilipofika Februari 20, 2007 ukawa ndio mwisho wa mtu huyu.

Kuuawa kwa Matheri kulipokelewa kwa hisia tofauti na jamii ya Wakenya, miongoni mwao zilikuwa ni taasisi za watetezi wa haki za binadamu. Taasisi hizo ziliwashmbulia Polisi kwamba walitumia kauli ya Waziri wa Usalama wa raia, Mheshimiwa Michike vibaya. Taasisi hizo zilipinga waziwazi kuhusu kuuawa kwa Matheri na kuwashutumu Polisi kwamba hawakumtendea haki Matheri kwani alipaswa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria na kuhukumiwa kama mhalifu mwingine yeyote.

Naye mama yek mzaziMatheri, Martha Wanjiru akizungumza mara baada ya kupata taarifa za kuuawa kwa mwanye na Polisi, alisema kwamba, alijua kuwa ipo siku mwanaye huyo angeuawana hatimaye siku hiyo imefika. Mama huyo alikiri kwamba ni takribani mwaka mmoja ulikuwa umepita bila ya kumwona mwanaye.

Huku akionekana kujuta, mama huiyo alisema, “Kama ningejua, mamba ya mwanangu huyu niliyemzaa miaka 30 iliyopita, ingezaa mtoto atakayekuja kuwa muuajina kuniletea usumbufu mkubwa utakaoniumiza moyoni mwangukatika maisha yangu yote, hakika nisingemzaa, lakini hilo ni jambo ambalo siwezi kulifanya.”

Mama huyo anakiri kwamba kuna wakai aliwahi kumsihi mwanaye ajisalimishe mikononi mwa Polisi, kwani hiyo ndiyo njia pekee ambayo ingepelekea kufikishwa kwenye vyombo vya sheria na kuhukumiwa kwa haki, lakini mwanaye hakukubali, badala yake akaendelea na vitendo vyake vya ujambazi.

Naye mkewe Matheri, Bi Felistus Wanjiru akimwelezea mumewe, alisema kwamba Matheri alikuwa ni mpole sana na hakuwa ni mtu wa maneno mengi. Bi Wanjiru alidai kwamba katika kipindi chote alichoishi naye hakujua kwamba mumewe alikuwa ni jambazi sugu aliyekuwa akitafutwa na Polisi.

Hata hivyo hatua inayochukuliwa na Polisi nchini Kenya ya kuwauwa majambazi kama Matheri, imewagawa wakenya katika makundi mawili. Lipo kundi linaloona kama ile ilikuwa ni hatua sahihi ya kukomesha ujambazi nchini humo, na kundi jingine linaona kuwa, hiyo haikuwa ni njia sahihi ya kukomesha ujambazi.

Je, kw Polisi kuendesha mauaji ya namna hii kwa watu wanishukiwa kuwa ni majambazi sugu, hakuliweki Taifa la Kenya katika miongoni mwamnchi zinazokiuka haki za binadamu?
Je, hali hiyo haiwezi kuufanya uhalifu kuwa wa kutisha zaidi, kwani majambazi hawatosita kuuwa wakati wanapofanya uporaji, kwa sababu wanjua hata wao wakipatikana watauawa?

Hayo yote ni miongoni mwa maswali ambayo Wakenya wengi walikuwa wakijiuliza na bado wanjiuliza, na mwenye majibu ya maswali hayo ni serikali yenyewe ya Kenya

****************Mwisho*********************

1 comment:
Andika Maoni Maoni
  1. Ni msisimko na hudhunisho. Nimeipenda na nimeifuatilia mpaka mwisho.

    ReplyDelete

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi