0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Oct 31, 2009

HANDSOME ALIYEITIKISA KENYA-SEHEMU YA PILI

Ilipoishia..............
Baada ya kumuuwa Matheri Polisi katika upekuzi walioufanya katika nyumba yake walikuta bunduki aina ya AK-47 pamoja na risasi 26. Hata hivyo upo utata uliojitokeza katika taarifa zilizonukuliwa kutoka pande mbili, yaani upande wa Polisi na mke wa Matheri kwa upande mwingine.

Endelea kufuatilia kisa hiki hapa chini…………..

Kwani kwa upande wa Polisi walidai kwamba wakati wnmuuwa Matheri alitoka akiwa na bunduki aina ya AK-47 na hivyo kuwalazimisha Polisi kumuuwa ili kujihami, lakini kwa upande wa mkewe, Felister Wanjiru ambaye alikuwa na ujauzito wa miezi saba wakati huo, akihojiwa na kituo cha Luninga cha KTN alidai kuwa mumewe alitoka akiwa hana silaha yoyote, tena alitoka akiwa kifua wazi akiwa amevaa kaptula, maarufu kama Bukta huku akiwa ameweka mikono yake kichwani ili kuwaonesha Polisi kwamba hakuwa na silaha yoyote, lakini kwa mshangao Polisi walimmiminia risasi mumewe na kumuuwa palepale.

Akisimulia zaidi mkasa huo katika kituo hicho cha Luninga, Wanjiru alisema kwamba siku ya tukio alikuwa amelala na mumewe chumbani, mara akasikia michakato ya miguu nje ya nyumba yao, lakini mumewe hakuonekana kwamba alikuwa na wasiwasi, baadae walisikia sauti ya Polisi waliokuwa nje ya nyumba yao wakijitambulisha na kumtaka mumewe atoke nje na ajisalimishe haraka la sivyo wataichoma nyumba moto na kuwauwa wote waliomo ndani.

Mumewealiposikia hivyo alijificha chini ya mvungu wa kitanda ili kuokoa maisha yake. Baada ya kuona kwamba Polisi wanazidi kusisitiza msimamo wao, ilibidi amsihi mumewe ajisalimishe ili kuokoa maisha ya watoto wake, kwani katika nyumba ile walikuwa yeye Wanjiru na mumewe Matheri pamoja na watoto wao 6, huku Wanjiru akiwa akiwa na ujauzito wa miezi 7.

Akizidi kusimulia, Wanjiru alisema kwamba mumewe aliamua kutii amri ya Polisi na kutoka nje huku akiwa amevaa bukta na mikono yake ikiwa nyuma ya kichwa. Alipofika nje aliamriwa apige magoti huku akiwa ameweka mikono yake nyuma ya kichwa na aache kinywa wazi , kitu ambacho alitii.

Ndipo Polisi mmoja alipomsogelea mahali alipo na kutumbukiza mdomo wa Bunduki yake kinywani mwa Matheri na kisha kuifyatua sawia, huku kila mtu akishuhudia. Katika mauaji hayo, Polisi walikiri pia kumuuwa mtu mwingine ambaye inasemekana alikuwa ni mlinzi binafsi wa Matheri {Bodyguard}. Utata wa namna Matheri alivyouawa haukusumbua vichwa vya Wakenya walio wengi, kwani kwao hiyo haikuwa ni hoja, bali cha msingi kwao ilikuwa ni kusherehekea kuuawa kwa Matheri.

Katika kijiji alichozaliwa Matheri kilichopo magharibi mwa jiji la Nairobi vituo vya Luninga nchini Kenya vilikuwa vikionesha wakazi wa kijiji hicho wakishrehekea kwa nyimbo za kuwasifia Polisi kwa ushujaa wao wa kumuuwa mtu ambaye alikuwa ni tishio kwa usalama wao na mali zao.

Hatua ya kluuawa kwa Matheri inasemekana ni katika kutii amri ya waziri wa usalama wa raia nchini Kenya, Mheshimiwa John Michuki ambaye Wakenya walimpa jina la utani la “Kimeendero” au “Crusher” ya kuwaamuru Polisi kuwauwa majambazi pale wanpoonekana kukabiliana na Polisi kwa silaha.

Simon Matheri Ikere kijana mzuri mwenye sura ya mvuto na mpole kupindukia alikuwa ni mtoto wa nane kuzaliwa akiwa ni kitinda mimba wa familia ya Mzee Peter Ikere Gichungu aliyekuwa dereva wa malori nchini humu na mkewe Martha Wanjiru, mama wa kilokole.

Kwa mujibu wa maelezo ya wazazi wake, Simon Matheri Ikere alizaliwa mwaka 1977 na katika kipindi chote cha utoto wake hakuwahi kuonesha tabia ya wizi. Tabia walioijua aliyokuwa nayo tangu utoto wake ni ile ya kuwa na hasira za ziada ambazo hawadhani kama ndio chanzo cha mtoto wao kuwa jambazi sugu.

Baba yake alisema kwamba mwanaye alishindwa kuendelea na masomo ya elimu ya msingi katika shule ya msingi Kihara akiwa darasa la sita. Mzee huyo alikiri kutojua sababu hasa ya mwanaye kuacha shule akiwa darasa la sita ili hali alikuwa na maendeleo mazuri tu shuleni.

Baada ya kumuona mwanye ameacha shule, Mzee huyo akaamua kumpeleka katika eneo la Wangige ambalo ni maarufu kwa shughuli mbalimbali za ufundi, maarufu kama Jua Kali nchini Kenya.

Matheri alipelekwa katika eneo hilo ili akajifunze ufundi wa kuchomea vyuma {Welding}. Baba yake anakiri kwamba huenda katika eneo hilo la Wangige ndipo mwanaye alipojifunza tabia ya uchomaji wa nyumba moto {Arsonist}, ingawa hata hivyo wataalamu wansema tabia hii ni maradhi.

Siku moja miaka saba iliyopita ndipo vitendo hivyo vya uchomaji nyumba moto vilipoanza pamoja na usumbufu mdogo mdogo katika familia. Mzee huyo anakumbuka siku moja likuw ametofautiana naye na kutokana na hasira zake za ziada Matheri aliamua kuchoma nyumba yake mwenyewe na kisha kutoweka.

Kitendo cha kuchoma nyumba yake mwenyewe ambayo aliijenga kwa msaada wa baba yake, kilimuuzi sana mzazi huyo na hivyo kumfungulia mashtaka ambapo alifungwa miaka mitano jela.

Ni nini kitatokea baada ya Matheri kumaliza kifungo chake….Fuatilia kisa hiki kesho

1 comment:
Andika Maoni Maoni
  1. pole kwa kazi nzuri unayoifanya.

    naomba usiwe ukichelewa ku update blog yako

    ReplyDelete

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi