0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Oct 30, 2009

HANDSOME ALIYEITIKISA KENYA.

Jiji la Nairobi, Moi Avenue


Siku ya Jumanne ya Februari 20, 2007 ni siku ambayo haitasahauliwea na Wakenya wengi, na hasa Polisi wa nchi hiyo. Ni siku ambayo Polisi zaidi ya 100 wa nchi hiyo kutoka kwenye kitengo maalum cha kupambana na uhalifu walifanikiwa kumuua jambazi mmoja sugu na aliyekuwa akitafutwa kwa udi na uvumba aliyejulikana kwa jina la Simon Matheri Ikerealiyekuwa na umri wa miaka 30.

Akiwa bado ni kijana mmbichi wa umri wa miaka 30, Simon Matheri Ikere alikuwa ni jamabzi hatari aliyekuwa akivuma katika viunga vya jiji la Nairobi kama mzimu kiasi cha Polisi kukiwekea kichwa chake dau la shilingi za Kenya zipatazo 150,000 kwa mtu yeyote ambaye angefanikisha kukamatwa kwake.

Ilikuwa ni majira ya saa nane na nusu za usiku wa Jumatatu kuamkia Jumanne, Polisi zaidi ya 100 waliizingira nyumba ya Simon Matheri Ikere iliyokuwa katika eneo la Athi River takribani kilomita 30 Kusini, Mashariki mwa jiji la Nairobi.

Katika tukio hilo ambalo lilitawaliwa na kurushiana risasi hatimaye ilibidi Polisi wamuombe mtuhumiwa ajisalimishe kwa kutoka nje ya nyumba yake ili kunusuru maisha ya watu wengine waliokuewa ndani ya nyumba ile. Simon aliamua kujisalimisha.

Wakati anatoka nje ya nyumba yake, Polisi walimshambulia kwa risasi na kumuuwa. Polisi walifanikiwa kumuuwJambazi huyo baada ya kupata taarifa kupitia kwa raia mwema, na kwa kutumia satelaiti walifanikiwa kujua mahali alipo kupitia simu yake ya mkononi, baada ya kupata namba yake ya simu kutoka kwa raia huyo mwema.

Msemaji wa Polisi nchini Kenya Gideon Kipunjatialisema kwamba Matheri alikuwa anatuhumiwa kwa mauaji ya watu zaidi ya 18 miongoni mwao wakiwa ni daktari bingwa wa maradhi ya ukimwi {AIDS} Prof. Job Bwayo ambaye aliuawa mwanzoni mwa mwezi huo huo wa Februari pamoja na mfanyakazi wa kimishenari wa Kimarekani aitwae Lois Andersnna binti yake Zelda White.

Mauaji ya Wamarekani hao yalitokea mnamo Januari 2007 katika tukio la kupora gari ambapo inasemekana Matheri na wenzie ndiyo waliohusika. Kipunjati alikiri kwamba Polisi walikuwa na ushahidi wa kina wa kumhusisha na mauaji hayo.

Naye kamanda mkuu wa Polisi wa jiji la Nairobi Njue Njagi akizungumzia tukio hilo alisema, ‘Leo ni siku kubwa kwa upande wa jeshi la Polisi, kwani tumefanikiwa kumuua jambazi sugu aliyekuwa akilisumbua jeshi la Polisi kwa muda mrefu.

Kamanda Njagi aliendelea kusema, ‘Mtu huyu alichukulia kuuwa kama kitu cha kufurahisha [hobby} lakini kwa uwezo wa Mungu leo polisi tumeweza kuzima vitendo vyake.’ Kmanda huyo aliendelea kubainisha kwamba Jeshi la Polisi bado linaendelea kuwasaka majambazi wengine watano ambao ni washirika wakuu wa Matheri.

Polisi wa nchini Kenya wanaamini kwamba Matheri alikuwa akiongoza genge la majambazi ambalo lilikuwa likiendesha uharamia katika miji mikuu ya Afrika Mahsriki, ambapo wakazi wa miji hiyo kwa muda mrefu wamekuwa majeruhi wa vitendo vya ujambazi vilivyokuwa vikiendeshwa na Matheri pamoja na genge lake.

Baada ya kumuuwa Matheri Polisi katika upekuzi walioufanya katika nyumba yake walikuta bunduki aina ya AK-47 pamoja na risasi 26. Hata hivyo upo utata uliojitokeza katika taarifa zilizonukuliwa kutoka pande mbili, yaani upande wa Polisi na mke wa Matheri kwa upande mwingine

Ni utata gani huo, fuatilia kisa hiki kesho…………..

1 comment:
Andika Maoni Maoni

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi