0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Feb 5, 2016

Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake..!



Tafiti nyingi zilizofanywa kwa muda mrefu zinaonyesha kwamba wanawake hutofautiana kabisa kimaumbile na wanaume kiasi kwamba inakuwa kama vile ni viumbe wawili tofauti. Mtaalamu mmoja wa mahusiano ya watu John Gray anamuelezea mwanaume kuwa anatoka sayari ya Mars na mwanamke anatoka kwenye sayari ya Venus, akiwa na maana kwamba hawa ni viumbe wawili tofauti kabisa kimaumbile.

Kimaumbile mwanamke na mwanaume hutofautiana katika kufikiri, hisia, kuyatazama mambo, kupokea taarifa, upendo, utashi na shukurani. Mwanamke hujali sana upendo, yaani kupendwa kuliko ilivyo kwa wanaume. Mwanamke huridhika na yuko tayari kuvumilia ‘yasiyovumilika’ kama anahisi kwamba anapendwa na mwanaume. Ni jambo la kushangaza sana kwamba, mwanamke anapoambaiwa ‘nakupenda’ huwa amepewa zawadi kubwa sana na kujisikia kuwa mshindi katika mahusiano.
Wanawake huwa wanaamini katika kusikilizwa zaidi kuliko kupewa ufumbuzi. Ndio maana wanawake wanapokuwa pamoja wakipeana ushauri na kupeana moyo kuhusu matatizo ya kimahusiano yanayowakabili, hawatafuti ufumbuzi bali kutaka wenzao wawasikilize na kuwa pamoja nao katika madhila yao.
Mwanamke anaposema jambo ambalo linamkera kumwambia mumewe au mpenzi wake, sio kwamba anataka apatiwe suluhisho, la hasha. Anaposema jambo hilo anategemea kusikia mume au rafiki akionesha kusikiliza au kujali na sio ufumbuzi. Kwa bahati mbaya wanaume huwa wanadhani wanawake hao wanatafuta ufumbuzi kwa yale wanayoyaeleza.
Kwa mfano:
Mwanamke anapomwambia mumewe au rafiki yake, “siku hizi naona kazi zimenizidi sana” hategemei kupewa ufumbuzi wa hilo, badala yake anataka kusikia mwanaume aua rafiki yake akichangia katika hisia (Kumbuka mwanamke hujali zaidi hisia). Katika hili kwa bahati mbaya mwanaume atasema, “punguza baadhi ya kazi” au “labda utafute msichana wa kazi” au “na wewe unajiumiza bure, kazi nyingine hazina hata maana…..”
Kwa kuwa mwanaume ni mtu wa ufumbuzi tu atadhani ndicho mkewe anachohitaji, wakati ukweli ni kwamba, mkewe anahitaji kusikilizwa tu- anahitaji mawasiliano. Mwanamke hapa angefurahi kusikia, “pole sana mke wangu, hebu njoo nikukumbatie kidogo….” Angefurahi kwa sababu anachotaka ni kusikilizwa ambapo kwake ndio thamani yake.
Wakati mwanamke anapozungumzia matatizo yenye kumtanza, mwanaume kwa bahati mbaya hudhani kwamba mwanamke huyo anamlaumu yeye au anatafuta ufumbuzi wa matatizo hayo kutoka kwake. Kwa hiyo kwa kadiri mwanamke anavyokuwa na matatizo zaidi ndivyo ambavyo mwanaume anajihisi kulaumiwa. Mwanaume hajui kwamba kimaumbile mwanamke anapozungumzia matatizo au hofu zinazomkabili huwa anataka kusikilizwa zaidi kuliko kutafuta ufumbuzi.
Mwanaume hajui kwamba mwanamke hujisikia ahueni kubwa kusikia tu jibu la ‘ahaa’ au ‘oh, kumbe’ kutoka kwa mwanaume, linatosha kabisa kumpa ahueni mwanamke.

1 comment:
Andika Maoni Maoni
  1. NIMEIPENDA HII MADA..NI KWELI MWANAMKE ANAPENDA SANA KUSIKILIZWA...Ningefurahi kama wengi Wake kwa waume wangesoma hii...

    ReplyDelete

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi