0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Jul 24, 2014

Uhusiano uliopo kati ya kufikiri kwetu na afya mgogoro...!


http://ip.convio.net/images/content/pagebuilder/11496.jpg

Leo nina kisa nataka kuwasimulia.

Bwana mmoja alikuwa amekwenda kazini kama ilivyo kawaida yake, akiwa ndio anafika kazini akapigiwa simu kujulishwa kwamba nyumba yake inaungua.

Bwana yule akarudi nyumbani haraka huku akijaribu kuwasiliana na watu wa zima moto. Alipofika nyumbani akaikuta nyumba yake ndio inazidi kuteketea kwa moto na hakuna kilichosalimishwa hata kitu kimoja na askari wa zima moto walikuwa hawajafika katika eneo la tukio.

Basi yule bwana akawa amesimama akishuhudia nyumba yake ikiteketea asijue la kufanya. Ulikuwa ni msiba mkubwa sana kwake, kwani ile nyumba ilikuwa ni kubwa na ilimgharimu kiasi kikubwa cha fedha.



Wakati akiwa bado amesimama pale nje akiwa anashuhudia lile tukio, mwanae mmoja wa kiume alimsogelea na kumshika bega, kisha akamwambia ‘usijali nilishaiuza tangu jana!, nilikusikia wewe na mama mkilalamika kuwa hii nyumba ni kubwa sana na mlikuwa hamuihitaji tena, nikakutana na tajiri mmoja mwekezaji toka nje ambaye alikubali kuinunua kwa gharama yoyote’

Ghafla sura ya baba yake ikagubikwa na tabasamu la furaha na kumkumbatia mwanae na kumpongeza kwa kwa uamuzi mzuri alioufanya. Mpaka hapo hakuna kilichobadilika: Nyumba ilikuwa bado inaungua lakini hakuwa mmiliki wa nyumba ile tena, kwa nini ajali, wakati haimuhusu?

Wakati baba akiendelea kumpongeza mwanae huyo, mwanae mwingine mdogo wa kiume aliwasogelea uso wake ukiwa umegubikwa na huzuni, Baba alimwangalia mwanae kwa mshtuko, ‘nini tena?’

 “Ni kweli mwekezaji mmoja alikuwa anataka kuinunua hii nyumba” yule kijana alisema, akimwambia baba yake. “Lakini mkataba wa mauzo ulikuwa bado kusainiwa na pande mbili, kwa hiyo hatuna cha kuuza.”

Baada ya kupata taarifa ile, yule baba aliishiwa na nguvu kabisa, na kukaa chini, mwili wote ulikufa ganzi na hakuwa na la kusema, akabaki kuwaangalia wale wanaye asiamini masikio yake.

Bado hakuna kilichobadilika kwani nyumba bado ilikuwa inaungua. Kilichobadilika ni taarifa tu.

Wakati nyumba yake inaungua aligubikwa na huzuni. Alipopata taarifa kuwa nyumba ilishauzwa kwa mtu mwingine, ingawa bado ilikuwa inaungua alifurahi sana kwa sababu haikuwa yake tena. Zilipokuja taarifa nyingine toka kwa mwanae mdogo kuwa mkataba wa mauzo ulikuwa bado haujasainiwa, baba akataharuki na kurudi kwenye majonzi tena kwa sababu kumbe nyumba bado iko mikononi mwake.

Akiwa bado amegubikwa na simanzi, aliyekuwa mnunuzi wa ile nyumba alifika. “Najua hii ni bahati mbaya sana kwako, kwa nyumba yako kuungua, hata hivyo nilikuwa nahitaji hii ardhi tu, kwa hiyo nitalipa kiasi kile kile cha fedha tulichopatana”

Kusikia hivyo, uso wa yule baba, ukabadilika tena na kugubikwa na furaha kubwa isiyo kifani, kwani nyumba haikuwa mikononi mwake tena, hakuna haja kusikitika.

Naamini mpaka hapo mmeona mwili unavyopata mabadiliko kulingana na jinsi tunavyotafsiri matukio tunatoyapata. Ikiwa tutatafsiri tukio vibaya kwa kuanagalia upande mmoja wa hasi, ni wazi tutapata maumivu ya kihisia.

Kwa mfano wa tukio hili la nyumba kuungua, awali yule mzee alikuwa analalamika kuwa ile nyumba haihitaji tena, kwa kuwa ni kubwa na labda ilikuwa ina muundo wa kizamani, kwa hiyo hakuipenda. Alikuwa anatamani kujenga nyumba mpya ambayo ndiyo aliyokuwa akiihitaji.

Tumejifunza jinsi mawazo yalivyo na nguvu, kwamba kile tunachofikiri ndicho kinachofanyiwa kazi na akili ya kina (Subconscious mind), kwa hiyo, tukio lile ilikuwa ni matokeo ya kile alichokuwa anafikiri. Lakini kwa bahati mbaya matokeo ya fikra zetu hayaji kwa namna tunavyotaka, yanakuja kwa njia ya ajabu mno ambayo mwenye werevu wa kihisia pekee ndiye atakayeweza kung’amua.

Akili ya kina huwa haileti majibu yakiwa yamevaa suti, mara nyingi yanakuwa na sura isiyovutia na yenye kutia kinyaa, usipoigundua, umekwisha. Je ni mara ngapi tunapiga teke yale mambo yanayofanyiwa kazi na akili ya kina na kuja mbele yetu yakiwa na sura kama hii?

Je wewe umejifunza nini juu ya kisa hiki?

Je hofu na maumivu ya kihisia tunayopata ni kutokana na tukio au tafsiri inayokwenda akilini kwetu?

UFAFANUZI ZAIDI:

Kwa ufafanuzi zaidi ni kwamba tunapaswa kujipa majibu chanya pale tunapopata jambo linalotutatiza, kwani hiyo ndiyo njia pekee itakayotufanya tuishi kwa amani.

Kwa mfano iwapo utampigia mpenzi wako simu halafu hapokei na simu yake ikawa inaita mara kadhaa bila kupokelewa, hapo unapaswa kujipa jibu kwamba, "labda atakuwa ameiweka simu kwenye chaji na yeye yuko nje ya hapo nyumbani au ofisini kama ni mfanyakazi."

Kama unadhani atakuta missing call zako na kukupigia lakini asifanye hivyo, basi jipe jibu kwamba, "Labda hana salio" 

Kama ukipiga simu tena ukakuta simu yake iko bize muda wote anaongea na mtu mwingine, jipe jibu kwamba, "Labda anaongea na wazazi wake au bosi wake kama ni mfanyakazi" hata kama ni saa sita usiku hilo jibu linatosha kujifariji na kuepuka msongo wa mawazo!

Kama ukipiga tena ukakuta simu imezimwa, basi jipe jibu kwamba, "Labda simu yake imeisha chaji"

Kama ukipiga simu baadaye ukakuta inaita halafu akapokea lakini akakupa majibu yenye kukera, basi jipe jibu kwamba, "labda amekumbwa na msongo wa mawazo"

Je si mmeona jinsi ilivyo rahisi kuepuka kukerwa na mtu kwa kujipa majibu chanya? 

Dumisha furaha yako kwa kujipa majibu chanya na kuepuka maradhi yatokanayo na kusongeka.....

No comments:
Andika Maoni Maoni

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi