Hivi karibuni baadhi ya watafiti wa masuala ya mapenzi na uhusiano wamebainisha kwamba bado kitambo kidogo, japokuwa ni polepole ndoa zitaanza kuonekana kama fasheni ya kale na isiyo na umuhimu kwa watu hususani wa kizazi hiki kinachokuja kwa kasi.
Licha ya jamii kushuhudia ndoa zikifungwa kila uchao tena kwa mbwembwe za kila aina, lakini jambo ambalo wengi wetu hatulijui ni kwamba hivi sasa hata hao wanaooana hawajui ni kwa nini wanaoana, na ndiyo maana hata kiwango cha talaka nacho kimepanda sana ukilinganisha na miaka ya zamani.
Kwa nini watafiti hawa wanaamini kwamba kuna siku tena siyo nyingi ndoa zitaonekana kama fasheni ya kale na isiyo na mashiko kwa kizazi hiki?