Leo nina kisa nataka kuwasimulia.
Bwana mmoja alikuwa amekwenda kazini
kama ilivyo kawaida yake, akiwa ndio anafika kazini akapigiwa simu kujulishwa
kwamba nyumba yake inaungua.
Bwana yule akarudi nyumbani haraka
huku akijaribu kuwasiliana na watu wa zima moto. Alipofika nyumbani akaikuta
nyumba yake ndio inazidi kuteketea kwa moto na hakuna kilichosalimishwa hata
kitu kimoja na askari wa zima moto walikuwa hawajafika katika eneo la tukio.
Basi yule bwana akawa amesimama
akishuhudia nyumba yake ikiteketea asijue la kufanya. Ulikuwa ni msiba mkubwa
sana kwake, kwani ile nyumba ilikuwa ni kubwa na ilimgharimu kiasi kikubwa cha
fedha.