0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Nov 2, 2008

JE NI NINI MALENGO YAKO?

Ni Kitu gani unachotaka kufanya katika maisha yako? Je unaota ndoto gani juu ya maisha yako? Je wewe ni mzuri katika eneo gani? Yaani unacho kipaji gani?
Katika umri wa utoto kila mmoja wetu aliwahi kuigiza kuhusu jambo fulani, wapo waliowahi kuigiza kuwa ni madaktari, madereva, wanasiasa, wasanii waigizaji katika filamu na kadhalika na kadhalika.

Wengi wetu pia tuna ndoto fulani juu ya maisha yetu, ndoto ambazo wakati mwingine huziona kana kwamba ndivyo maisha yetu yatakavyo kuwa huko mbele ya safari.
Hapa ningeomba kutahadharisha kwamba kama ndoto zako zilikuwa hasi na zilikuwa zimejaa maumivu na kukatishwa tamaa au hofu za kushindwa katika kufikia malengo yako hayo, basi ujue kwamba hayo ndiyo mavuno ya aidha ulichokuwa nacho leo au utakachovuna kesho ukubwani.

Mara nyingi inashauriwa na wataalamu wa elimu hii ya utambuzi kuwa ndoto zetu zinatakiwa ziwe ni chanya na za kutupa nafuu.
Kwani ndoto ulizokuwa nazo utotoni au ulizonazo leo inawezekana ikawa ndio matokeo ya shughuli unayofanya leo.

Kama ulikuwa na malengo tofauti na unachokifanya leo, kwa maana ya kwamba unachokifanya leo si kile ulichokuwa umekusudia kuwa ndio malengo yako ya kuwepo hapa duniani basi huajachelewa, unao uwezo wa kuibadilisha hali hiyo kwa jinsi utakavyopenda.
Kimsingi haitakiwi maisha yakuendeshe, bali uyaendeshe, kwani wewe ndio mwenye mamlaka ya kujichagulia maisha uyatakayo na sio maisha yakuchagulie yanavyotaka.

Hebu chunguza mawazo yako ya kina ujue ni kitu gani unachowaza ndani yako, najua sio jambo rahisi sana kutokana na mazoea, lakini ukiamua unaweza kabisa ukajua mawazo yaliyo ndani yako na hapo ndipo utakapo gundua siri kubwa iliyoko katika maisha yako.
Kwa sababu, naamini utagundua kwamba maisha uliyonayo sasa ni matoeo ya kile unachokiwaza na unachokiamini.

Kama ukigundua kuwa mawazo yako yamejaa majuto na maumivu ya matukio ya jana na hofu za kesho, basi yakupasa ubadilishe mfumo wako wa kufikiri, na kuanza kuwaza yale yanayokupa furaha na amani.

Kataa kabisa mawazo ya kukatisha tamaa na jaribu kuwaepuka marafiki wenye mawazo yenye kukatisha tamaa kwani hao ndio maadui wakubwa wa kukukwamisha kufikia malengo yako.
Katika miongoni mwa makala zake kwenye Gazeti la Jitambue, hayati Munga Tehenan, Mtaaluma wa Elimu hii ya utambuzi aliwahi kuandika kuhusiana na nguvu ya mawazo pamoja na subira, aliandika hivi:

“Wakati inawezekana ukawa na hamu ya kuona malengo yako yanatimia mara moja, ukweli ni kwamba hamu yako ya kuleta mabadiliko ya haraka yaweza kukuletea madhara zaidi kuliko faida.

Kwa nini? Kwa sababu unakosa subira na hivyo unafanya mambo yako kinyume na utaratibu wa maumbile. Ukosefu wa subira hutuma ujumbe hasi kwenye mawazo yako ya kina na wakati huohuo unakuwa unafanya mambo kwa kupingana na kanuni ya maumbile. Kwa kufanya hivyo hutumii kile kinachofahamika kama nguvu ya subira. Hii nguvu ya subira yaweza kupatikana kwa hatua mbali mbali zikiongozwa na kufikiri kwako.

Wakati unapokosa subira katika kupata mafanikio, unachofanya ni kuisukuma nafsi yako mbali zaidi kutoka kwenye mafanikio. Wengi wetu hutaka vitu tunavyoamua kuvipata tuvipate hapo hapo, na pale tunapoamua kubadilika ama kuboresha hali zetu, tunataka mabadiliko hayo yatokee mara moja ili mtu aweze kufurahia maisha yetu mapya na kuanza kufurahiya mafanikio.
Lakini sisi ni sehemu ya maumbile na maumbile hayabadili vitu mara moja. Mchakato unaweza kuanza mara moja lakini mabadiliko kamili hayawezi kutokea mara moja.

Kwa vile sisi ni sehemu ya maumbile, ni lazima tufanye kazi kama maumbile yanavyotaka na kwa kufuata taratibu zake.
Linapokuja suala la kufikia malengo yako, mawazo yako ya kina kama yalivyo maumbile yanatakiwa kufanya kazi kwa kupitia mchakato na kukuruhusu kwenda kwa hatua kuelekea kwenye mafanikio ya malengo yako.”

Kwa maelezo hayo tumeona kuwa maisha ni malengo na malengo ndio mafanikio, lakini la msingi tusije tukajiumiza kwa kutaka malengo hayo yatokee mara moja, kuwaza hivyo ni kujiumiza kihisia na kuisababishia miili yetu maumivu na hivyo kuwa mibovu kiafya.

HATUA MUHIMU KATIKA MAKUZI YA MTOTO

Hivi umeshawahi kujiuliza hata siku moja, kwa nini watu wengine ni walevi? Wengine waongeaji sana? Wengine wakimya sana? Wengine waongo sana? Wengine wana tamaa ya ngono kupita kiasi na kadhalika? Lakini pengine una maswali mengi ya namna hii ambayo yanaonyesha jinsi wanadamu wanavyotofautiana.

Kuna hatua 5 muhimu ambazo mtoto lazima afanye mambo ambayo yanastahili kufanyika katika hatua husika. Na iwapo hayatafanyika, hali hizo huhifadhiwa katika mawazo yake ya kina na hivyo kumsababishia matatizo makubwa ukubwani.
Hatua hizo ni kama ifuatavyo:-

Hatua ya kwanza – oral stage: Hatua hii huwahusu watoto wa kuanzia siku moja mpaka miaka miwili. Katika hatua hii ya kwanza, furaha na raha ya mtoto huwa imejificha mdomoni. Utakuta mtoto kila wakati anafurahia kunyonya maziwa ya mama yake, vidole au midoli. Mtoto anatakiwa atumie mdomo wake mpaka ile hamu yake yote iishe. Kama ni kunyonya basi aendelee kufanya hivyo mpaka pale utakapofika wakati mzuri wa kumwachisha ziwa. Kumnyanyasa mtoto wakati ananyonya au kumfanyia vitendo ambavyo si vya kiungwana ikiwa ni pamoja na kumwachisha ziwa mapema, husababisha hamu yake ya kuutumia mdomo ibaki na hivyo kuhifadhiwa kwenye mawazo yake ya kina. Anapokuwa mtu mkubwa hulipa kisasi bila kujua kwa kuutumia mdomo kwa kadri anavyoweza. Hivyo anapokuwa mtu mkubwa anaweza akawa muongo sana, mlevi kupindukia, mvuta sigara sana, muongeaji sana, au mmbeya sana. Kama kuna watu unawafahamu wenye tabia hizi, jaribu kupeleleza kama walinyonyeshwa bila kunyanyaswa au kama hamu yao ya kunyonya iliisha.

Hatua ya pili – anal stage: Hatua hii humhusu mtoto wa miaka miwili au mitatu. Matumizi ya mdomo huwa yamekwisha na raha huhamia sehemu za haja. Katika hatua hii, mtoto hupendelea zaidi kutumia sehemu zake za haja kwa kukojoa au kwenda haja kubwa mara kwa mara. Katika kipindi hiki wazazi wengi hufanya makosa. Mzazi anashauriwa kuwa makini kwa kutoa mafunzo mazuri kwa mtoto wake, kumfundisha jinsi ya kujisaidia au jinsi ya kutumia choo. Kinyume na hivyo ni kumfanya mtoto awe na tabia ya kujifanyisha na hivyo kuwa na hali mbaya ukubwani. Mtoto aliyenyimwa huduma hii akiwa katika hatua hiyo hubakiwa na deni, anapokuwa mkubwa anaweza kupata matatizo ya kiakili. Watoto waliokosa huduma hiyo wanapokuwa wakubwa, mara nyingi huwa mashoga, na wengine huwa waoga kufanya mapenzi, lakini mbaya zaidi ni kukosa kabisa hamu ya mapenzi, wengine huwa wazembe na huwa na tabia fulani fulani ambazo zinahitaji msaada mkubwa wa wengine.

Hatua ya tatu – phallic stage: Hatua hii huwahusu watoto wenye umri wa miaka minne. Ni katika hatua hii ambapo mtoto huanza kutambua jinsia yake na hivyo kuwa karibu na mama yake au baba yake. Mtoto wa kiume hupenda kulala na mama yake na mtoto wa kike pia huwa hivyo hivyo hupenda kulala na baba yake (interest of opposite sex). Mtoto wa kiume humchukia baba yake bila kujua na kumuonea wivu mama yake na kuona kama anamfaidi baba yake jambo ambalo hulitaka liwe kwake, pia mtoto wa kike humchukia baba yake na kumuonea wivu baba yake na kuona kama anamfaidi mama yake jambo ambalo hulitaka liwe kwake. Watoto waliokosa kuwa karibu na wazazi wao wa jinsia tofauti katika hatua hii, wengi hupata matatizo, lakini hulipiza kisasi kwa sababu hawakuwa karibu na jinsia tofauti wanapohitaji kufanya hivyo. Usishangae kumkuta binti akiwa kwenye kundi la wavulana au mvulana akiwa kwenye kundi la wasichana.

Hatua ya nne – latency stage: Hatua hii huwahusu watoto wa miaka sita, minane na wakati mwigine mpaka miaka 12, ambapo mtoto macho yake yote huwa katika michezo ya kawaida na kwenda shule. Hakuna kitu cha ajabu kinachotokea katika hatua hii kati ya jinsia ya kike na ya kiume.

Hatua ya tano - genital stage: Hatua hii huwahusu watoto wa kuanzia miaka 13. katika kipindi hiki vijana wengi huanza kubalehe na kuvunja ungo. Katika hatua hii ndipo mtu hukabiliwa na vitu vingi katika maisha yake yote. Huanza kujishuhulisha na kutafuta maisha yake mwenyewe na ndipo hatua nyingine zote huanza kujirudia tena kama hazikufanywa vizuri katika umri huo. Raha ya mwanadamu yoyote katika kipindi hiki huwa ni mapenzi, lakini hutofautiana kiwango cha kupenda au kutamani kutokana na jinsi alivyolelewa katika hatua nne za mwanzo. Nakuomba sana kila unapokutana na watu waongo, wambeya, wakimya, wapenda ngono kupita kiasi n.k. waulize maisha yao ya utotoni.
This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi