0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Aug 7, 2013

NADHARIA HII, ITAWASHANGAZA HATA WANAWAKE WENYEWE........

 Nadharia hii itawashangaza hata wanawake wenyewe…..!

Mnamo Agost 23, 1973, majambazi wawili wenye silaha aina ya machine gun, walivamia benki moja jijini Stockholm, Sweden. Mmoja kati yao ambaye Alikuwa ametoroka jela siku chache nyuma, Jan-Erik Olsson alitangaza kwamba, “Shughuli imeanza.”

Majambazi hao waliwashikilia mateka watu wanne, wanawake watatu na mwanaume mmoja. Mateka hao walifungwa mabomu miilini na kushikiliwa ndani ya benki hiyo kwa muda wa saa 131, ikiwa na maana kwamba, walishikiliwa kwa siku tano. Mateka hao waliokolewa Agosti 28 na majambazi hao kukamatwa.


Baada ya kuokolewa, mateka wawili walionyesha jambo la kuchangaza na pengine kutisha, kama siyo kuudhi kwa baadhi. Walifanyaje?

MWANAMKE: DALILI ZITAKAZOMFANYA MPENZI MPYA AKUONE WEWE NI KING'ANG'ANIZI....

Mwanamke: Dalili zitakazomfanya mpenzi mpya akuone wewe ni king’ang’anizi…!

Hizi ni miongoni mwa sababu ambazo wanaume wengi huchomoa mapema kwa wapenzi wao wapya kabla uhusiano haujashika kasi. Kuna wakati wanawake hukosea na kuvuka mipaka mwanzoni tu mwa uhusiano. Anamganda mwanaume haraka sana au anaonesha dalili zote za kujipendekeza kupita kiasi. Lakini jambo ambalo wanawake wengi hawalijui ni kwamba, wanaume wako makini sana kuwakwepa wanawake ving’ang’anizi……..


Nitadadavua baadhi ya vijitabia vya wanawake vinavyowafanya wanaume wawaone kama ni ving’ang’anizi…..

SIYO KILA DALILI YA MWANAUME KUPENDA NI YA KWELI....!

Siyo kila dalili ya mwanaume kupenda ni ya kweli…!


Kuna wakati ambapo, wanawake wanajikuta wakikabiliwa na swali la, je, mwanaume huyu ananipenda kweli? Hii hutokea pale anapokutana na mwanaume ambaye, huenda amevutiwa naye. Pengine mwanaume naye anaweza kuonesha kuvutiwa na mwanamke huyo.


Kwa hiyo, mwanamke hujiuliza kama akubali ombi la mwanaume huyo na kukubali kuzungumza naye au kuanzisha naye uhusiano, kama mwanaume atakuwa amezungumza naye kuhusu jambo hilo. ni kweli kwamba, kuna ugumu kwa mwanamke kujua hasa ni kwa namna gani anaweza kujua kwamba, huyo mwanaume amempenda kweli au hapana.



Kuna vitu vingi ambavyo vinaweza kuwa ni dalili ya kumpenda mwanamke, lakini wakati huo huo vinaweza visiwe.


This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi