0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Jul 8, 2013

HII NDIYO SABABU YA WANAWAKE WENGI KUIBUA MABOMU...!

Hii ndiyo sababu ya wanawake wengi kuibua mabomu…!

Mnamo mwaka 1973 Dk. Paul MacLean, mtafiti toka taasisi ijulikanayo kama National Instute of Mental Health, alibaini kwamba, ubongo una sehemu tatu zinazoendana na nyakati tatu za mabadiliko ya kimaumbile.

Sehemu ya kwanza inaitwa reptilian. Hii inahusiana na kukutana kimwili kati mwanamke na mwanaume na tabia ya ukatili, hisia za hasira na hofu. Sehemu ya pili ni limbic brain. Hii inahusika na mapenzi, huzuni na wivu. 


Hata matumaini asili yake ni katika sehemu hii. Sehemu hii ndiyo inayodhibiti mapigo ya moyo na joto. Yote haya huathiriwa na kuwepo mahali hapo na mtu tunayempenda. Hamu ya mapenzi huenda moja kwa moja katika sehemu hii. Ni sehemu ambayo ina pupa na inaenda kasi kama umeme.


Ni enao ambalo halitaki kabisa kujishughulisha na mambo ya kutumia akili au tathmini. Sehemu ya tatu ya ubongo inaitwa neo-cortex, ambayo huruhusu matumizi ya mantiki, kutafakari kwa kina, lugha, kufanya mipango, kufikiri na maamuzi ya kina baada ya kufikiri kwa kina.


Katika kitabu chake cha The Emotional Brain, Joseph LeDoux anasema kwamba, sehemu zile mbili za kwanza za ubongo zinathibiti sana ile sehemu ya tatu. Na wala hii sehemu ya tatu haina udhibiti kwa zile sehemu mbili. Na ndiyo maana katika maisha ya kawaida, ‘hisia hudhibiti fikra.’ 


Ingawa fikra zinaweza kuamsha hisia kirahisi, lakini fikra zinapata tabu sana kuziondoa hisia zikishaingia. Hii ina maana sehemu ya pili ambayo ndiyo inayoziamrisha hisia, inaweza kuiburuza sehemu ya tatu kila inapotaka. Limbic ya mwanamke itamwambia, “umempata mwanaume barabara.” Sawa, lakini mwanaume mwenyewe ni mlevi..! 

Limbic itasema, “Nitaishi naye hivyohivyo. Ana sura nzuri mno, ninajisikia vizuri sana ninapokuwa naye….”

Sasa nafikiri unaweza kuona kwamba, hata kama mwanamke anaweza kusema kwamba anamtaka mwanaume mwenye haiba nzuri na mtu mwema si lazima kwamba, ndiye atakayevutiwa naye. Mfano mzuri wa jambo hili ni chakula.


Je huwa tunakula chakula kufuatana na ubora wake kiafya? Hapana…! Wengi wetu tunakula kutokana na utamu na ladha ya chakula! Dona ni bora kuliko ugali wa mahindi yaliyokobolewa kiafya. Lakini asilimia 90 ya Watanzania wanapenda ugali wa mahindi yaliyokobolewa maarufu kama Sembe. 


Hali hii ndiyo inayompata mwanamke anapofanya uchaguzi na kujikuta akimchagua mwanaume anayemfanya kujisikia raha, lakini ambaye si mtu mzuri kwake.


Suluhisho la jambo hili ni nini….?


Wanawake wanaweza kufanya urafiki na wanaume hao wazuri wa sura na wenye sifa ya uburuzaji na valuvalu kwa idadi wanayotaka kama kwa kufanya hivyo watajisikia raha maishani mwao; ili mradi tu urafiki huo usilete maumivu na huzuni ambayo yako juu kuliko furaha yenyewe. 


Kama huzuni ni kubwa kuliko furaha katika mapenzi na mwanaume aliye naye, basi mwanamke hana budi kuachana na limbic brain na kuchagua mwanaume anayemfaa kwa kutumia mantiki.

No comments:
Andika Maoni Maoni

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi