0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Nov 16, 2008

NI NINI FAIDA YA KUJIFUNZA MAARIFA HAYA YA UTAMBUZI?


Tukiwalea kiutambuzi, maisha hayatakuwa ni mzigo kwao.
Jumapili ya leo niliamua kushinda nyumbani, nikijaribu kutafakari mada ya kuweka humu kesho jumatatu.

Lakini leo asubuhi nimepokea Sms kadhaa kutoka kwa wasomaji mbalimbali wa Blog hii, pamoja na pongezi, msomaji mmoja alitaka kujua umuhimu wa kujifunza maarifa haya ya utambuzi na nini faida yake.

Na mimi nimeona nimjibu leo leo katika blog hii ili na wasomaji wengine waliokuwa wakijiuliza swali linalofanana na hili wapate kunufaika.

Kujifunza maarifa haya ni muhimu sana kwa ustawi wa maisha yetu, kwani kama ukirejea makala yangu ya nyuma wakati namjibu mdau wa Arusha, aliyetaka kujua maana ya utambuzi, naamini kabisa ina majibu ya kutosha kabisa kujua faida ya kujifunza maarifa haya.
Hata hivyo sio vibaya kama nitaeleza kwamba ni watu gani ambao ni vyema wakajifunza maarifa haya, ingawa mtu yeyote kwa uhitaji wa ustawi wa maisha yake anaweza kujifunza pia hata kama haguswi na sababu nitakazozieleza hapa chini.

Watu ambao ni vyema wakajifunza maarifa haya ni wenye matatizo yafuatayo:

Wale wanaoumwa na wametibiwa katika hospitali mbalimbali lakini hawaoni ugonjwa.

Wale wenye matatizo ya kindoa.

Wale ambao wamekata tamaa na maisha na kuyaona maisha kama mzigo na pengine. wanaamini kama wana laana au mikosi

Wale wanotaka kuacha kunywa pombe, kivuta sigara, au wanataka kuacha kutumia madawa ya kulevya.

Wale ambao siku za nyuma waliwahi kumiliki mali nyingi na sasa wameishiwa na wanajihisi kuchanganyikiwa.

Wale wanoamini kuwa wamelogwa na wamehangaika sana kwa waganga wote maarufu lakini hawajapata nafuu au kutatuliwa matatizo yao.

Wale walioambiwa kuwa wana mapepo au majini lakini hawayataki, na yameshindikana kutolewa.

Wale wanohisi kutengwa na jamii au ndugu.

Wale ambao wamehangaika kila dini au kila dhehebu wakitafuta ufumbuzi wa matatizo yao lakini hawajapata.

Wale wanoogopa watu, kuzungumza mbele ya watu au hata kusimama mbele ya watu.

Wale ambao hawaridhiki na maisha wanayoishi, kazi wanazofanya au hawaelewani na ndugu, majirani au mabosi wao.

Wale ambao wanataka kuwa watu wapya, na kama wanataka kupata chochote wanachohitaji hapa duniani, au kama wanataka kuwa na upendo wa kweli, amani ya kweli, furaha ya kweli, ridhiko la kweli katika maisha yao, hawajachelewa, iwapo wataamua kujifunza maarifa haya watashuhudia mabadiliko makubwa sana katika maisha yao.


Maarifa haya hayahusiani na dini au dhehebu lolote, isipokuwa wakati, mwingine dini inaweza kutumika kama rejea ya kile kinachofundishwa, lakini kimsingi hakuna chembechembe za udini katika elimu hii ya utambuzi

Maarifa haya yanapatikana wapi?

Maarifa haya unaweza kuyapata katika madarasa yaliyoko Kimara Rombo upande wa kulia kama unaelekea Morogoro mji kasoro bahari, lipo jengo limeandikwa "FAJI, Elimu ya Utambuzi inapatikana hapa" Zamani lilikuwa limeandikwa "Familia ya Jitambue"Au unaweza kuwasiliana na wawezeshaji kwa namba za simu zifuatazo:

0713 250701, 0763 627003,0716 795098, 0784 77130, 0755 745952

No comments:
Andika Maoni Maoni

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi