0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Jul 26, 2013

WANAUME WENYE WAKE WAZURI, HUWA NA 'NYUMBA NDOGO' ZISIZOTAZAMIKA KWA SURA AU UMBO.....!

Wanaume wenye wake wazuri, huwa na ‘nyumba ndogo’ zisizotazamika kwa sura au umbo…..!

Kwa mujibu wa utafiti wangu nilioufanyia kwenye eneo langu la kazi na kwa majirani zangu nimebaini kwamba, kati ya wafanyakazi watano niliofuatilia nyendo zao, ni wawili ambao walikuwa na ‘nyumba ndogo’ nzuri na zenye mvuto kuliko wake zao. Watatu walikuwa na ‘nyumba ndogo’ ambazo zinaweza kumpelekea mtu kujiuliza inakuwaje mwanaume huyo kuwa na ‘nyumba ndogo’ hiyo ambayo hata kwa mbali sana haiwezi kulingana na mkewe. Kwa jirani zangu wanne hali haikuwa nzuri, kwani hapa watatu walikuwa na ‘nyumba ndogo’ zilizo kinyume na wake zao kwa sura na umbo.

Watu saba niliowahoji kuhusu jambo hili, watatu walisema kwamba, wana ushahidi kuhusu wanaume wanaowafahamu wenye ‘nyumba ndogo’ zisizotazamika ukilinganisha na wake zao. Wengine wanne walitoa ushahidi wa wanaume wanaowafahamu ambao wana ‘nyumba ndogo’ nzuri sana ukilinganisha na wake zao.


Ni kitu gani kinatokea?


Ni kwamba, kuna ukweli kuwa wanaume wanaweza kuacha wake zao wazuri sana nyumbani na kufuata wanawake wabaya wasiotazamika kwa sura na umbo huko nje. Lakini pia wanaweza kuacha wake zao wabaya kwa sura ndani na kwenda kufuata wanawake wazuri kwa sura na umbo huko nje.

Hii ina maana gani?

Hii ina maana kwamba kuna mkanganyiko kwenye jambo hili. Lakini kwa bahati nzuri mkanganyiko huu kamwe siyo mkubwa na unaoweza kuumiza kichwa cha mtu. 


Binadamu ana kitu kiinachoitwa ukinaifu. Ukinaifu ni hali ya mtu kuchoka kukiona kitu kilekile mara zote. Kwa mfano, mtu anaponunua nguo mpya leo huipenda sana. Lakini baada ya muda fulani, ikiwa bado haijachakaa hujikuta kiwango cha kuipenda kikishuka.

Lakini ni vizuri nikarudi nyuma na kusema kwamba, kwenye suala la mapenzi. Ukinaifu huwapata wanaume kuliko wanawake. Inawezekana sababu ni za kimaumbile na hivyo ni vigumu kusema ni kwa nini inakuwa hivyo.


Kwa sababu ni suala la kimaumbile inakuwa kama lazima kwa mwanaume kupata ukinaifu. Anapopata ukinaifu siyo lazima atoke nje, yaani dawa yake au ufumbuzi siyo kutoka nje ya ndoa, ingawa wanaume wengi hufanya hivyo. Wanapofanya hivyo siyo kwamba, wanajua kwamba, wamepata ukinaifu, hapana. Wao hudhani tu kwamba, wamempenda mwanamke fulani kwa sababu hizi au zile.
Nadharia moja kuhusu ukinaifu ni kwamba, ili ukinaifu ushibishwe ni lazima mtu apate kitu kilicho kinyume na kile ambacho kimempa ukinaifu huo, au kuwa nacho mbali kwa muda fulani. Kwa mfano, kama mwanaume amepata ukinaifu wa umbile la mkewe ambaye ni kimbaumbau, ni lazima kama ataamua kwenda kutafuta mwanamke wa nje, atatafuta mwanamke tipwatipwa.

Kwa mkabala huo, ndiyo pale tunapokuta mwanaume akimfuata mwanamke wa nje mbaya ukilinganisha na mkewe. Labda anaamua kumfuata mwanamke huyo kwa msukumo wa ukinaifu – amekinaishwa na umbo au sura ya mkewe na hivyo angetaka kuona sura ya aina nyingine, ili afute ukinaifu wake. Kinyume cha sura nzuri ni sura mbaya, kwa hiyo atatafuta mwanamke mwenye sura kinyume na ile ya mkewe.
Kuna ukinaifu wa aina nyingi kwenye maisha ya ndoa. Mwanaume anaweza akakinaishwa na mtindo wa nywele wa aina moja wa mkewe. Kama mwanaume huyu hatakuwa mwangalifu, atajikuta akitafuta ‘nyumba ndogo’ yenye mtindo tofauti na mkewe. Inawezekana mkewe anatumia mtindo wa ‘twende kilioni’ kila akisuka nywele zake. Mwanamume anapokwenda kutafuta kilicho kinyume huko nje, anaweza akajikuta amevutiwa na mwanamke mwenye kunyoa na kuchana nywele zake fupi.

Kwa hiyo, inawezekana kabisa mwanaume akatoka nje ya ndoa yake kutafuta kinyume ambacho siyo sura wala umbile. Inawezekana akatoka kwa sababu amekinaishwa na ukimya wa mkewe, hivyo anatafuta kelele. Huyu anaweza kujikuta akiwa na mwanamke wa nje muongeaji na chakaramu sana, ambaye kisura na kiumbile anaweza kuwa sawa na mkewe.

1 comment:
Andika Maoni Maoni
  1. Bonge Bonge la somo ilibidi wengi wangesoma.
    Kazi nzuri kaka. ...

    ReplyDelete

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi