0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Jul 6, 2013

MZAHA NA KUCHEKESHA HUDUMISHA UHUSIANO KWA WANANDOA...!

Mzaha na Kuchekesha hudumisha uhusiano kwa wanandoa………!


Kucheka mara kwa mara kutakuondolea msongo wa mawazo na mifadhaiko; pia kutakufanya kulala usingizi mnono na kufurahia maisha yako. Uchekeshaji ni kitu muhimu sana na ndio maana viongozi wakuu, waalimu na washauri nasaha wengi ni wachekeshaji katika mazungumzo yao.


Mara nyingi ninapozungumzia au kujadili kuhusu kucheka, huwa najiuliza, hivi ni ndoa ngapi ambapo wanandoa wake hucheka na vicheko hivyo hutoka kwa wenzao? Nalijua jibu, lakini silipendi, ingawa siwezi kuubadili ukweli. Kama kuna ndoa kumi, basi ni ndoa mbili tu ambapo wanandoa wake hupeana afya kupitia kuchekeshana.

Kwenye ndoa nyingi, utakuta mke au mume amenuna muda wote. Hata mwenzake anapojaribu kumchekesha ili kufanya hali iwe na mwelekeo wa amani na upendo, ni kazi bure. Mke au mume huyu anapokuwa nje na nyumbani kwake, ni mchekaji mzuri sana tena wa vichekesho vya kawaida mno!

Nimebaini kwamba, ndoa inapokuwa na vichekesho yaani mzaha na utani usioumiza, humfanya kila mwanandoa kutamani kuwa nyumbani kwake, humfanya kila mwanandoa kuhisi haja ya ukaribu wa mwenzake. Lakini kubwa zaidi ni kwamba, mwanandoa hujenga afya yake ya akili, mwili na hisia kupitia kicheko.

Mara nyingi nikitazama zile sinema za dhati zilizobuniwa na wataalamu wanaojua Nyanja nyingi za kimaisha, huwa ninaona kicheko kikitumiwa sana kuelezea au kuonesha kama ndoa ni ya amani au vurugu. Kama ndoa ni ya amani, ni wazi utaona wanandoa wakitaniana na kufurahia sana utani. Huu siyo ukweli wa kisinema, bali ndio ukweli halisi.

Ndoa bora huweza kupimwa kwa kiwango cha utani kati ya wanandoa. Hebu jaribu kufikiri kwa hatua, halafu ujiulize, ni ndoa ngapi ngumu unazifahamu (pengine ikiwemo yako). Halafu jiulize, huwa unakuta wanandoa hao wakitaniana mara ngapi, kama imeshatokea ukawa karibu nao? Utapata jibu kirahisi sana. Hujawahi, na kama umewahi, basi ni kwa tukio maalumu au tukio la makusudi la wanandoa hao,kukuonesha wewe kwamba, wanandoa hao wako katika amani. 

Ukweli unaendelea kubaki kwamba,kama wanandoa wanajua kuchekeshana, tena kwa makusudi, vurugu ndogondogo huwa zinafutwa kirahisi sana. Ni lazima zifutwe kwa sababu, hatimaye kila jambo huingizwa kwenye mzaha na kuvurugiwa humo.

Wataalamu wanasema, mahali popote ambapo watu wana dhati sana ya mambo (serious), hapo kuna maumivu mengi. Kuna nyumba ambazo kila jambo linajadiliwa na kuzungumzwa kwa sauti kavu na imara ya dhati – hakuna mzaha hata chembe. Mke na mume wako pamoja tangu asubuhi, lakini hakuna hata mmoja ambaye amemfanya mwenzake akacheka. Kama yupo anayejaribu , atakutana na kizuizi cha, ‘si wakati wa mzaha huu.’

Napenda kukushauri kwamba, hebu kuanzia hivi sasa anza kufanya mzaha mdogomdogo kwa mwenzako, lakini wenye nguvu ya kuchekesha. Kama naye alikuwa hajui utamu wa kuchekesha, ataujulia kwako na huenda naye akaanza kufanya mzaha. Lakini mnaweza kwa pamoja kuamua kuanza kuyageuza maumivu mengi kuwa mzaha na vichekesho. Hili linawezekana.

1 comment:
Andika Maoni Maoni

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi