0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Dec 3, 2009

MCHUNGAJI ALIYEGEUKA MUUAJI-SEHEMU YA MWISHO

Muuaji John Nelson Canning


ILIPOISHIA..........

Ni katika kipindi hicho ambapo ujenzi wakanisa hilo ulipoanza ndipo mauaji ya Gleese na mkewe yalipotokea. Polisi wa upelelezi waliona ni vyema wakaanza upelelezi wao kwa kuangalia vyanzo vyake vya mapato pamoja na matumizi.

ENDELEA KUSOMA HAPA.................

Katika upelelezi wao ndipo walipokuja kugundua kwamba ndani ya wiki moja tangu mchungaji Canning apewe jukumu la kusimamia akaunt za familia ya Gleese ndipo alipolipa deni lake lote la manunuzi ya lile ghala aliloligeuza kuwa kanisa, na baada ya hapo akaanza matumizi makubwa ya fedha kwa kununua nyumba mbili zenye thamani ya dola 83,000, na wakati huo huo alianza upanuzi wa nyumba aliyokuwa akiishi kwa kuifanya kuwa ya kisasa zaidi. Kwa muda mfupi akaunti za familia ya Gleese ilikuwa imekauka ikiwemo akaunti yao nyingine ya akiba iliyokuwa na kiasi cha dola 16,000, zilikuwa zimetoweka kusikojulikana.

Polisi wa upelelezi walipowahoji marafiki wa familia ya Gleese, walidai kwamba wiki moja kabla ya kuuwawa kwao mke wa Gleese bibi Hazel Gleese alianza kumtilia mashaka mchungaji Canning kuhusiana na namna anavyosimamia fedha zao. Bi Hazel aliwaambia majirani zake kwamba anapanga kwenda katika benki jijini New York walipoweka fedha zao ili kuonana na meneja wa benki ili kupata taarifa ya fedha zao kwa mwaka mzima, lakini ikiwa imebaki siku chache kabla ya bi Hazel kwenda benki wakakutwa waameuwawa na hiyo ilitokea baada ya familia hiyo kugundua kwamba mchungaji Canning alikuwa ameghushi sahihi zao na kujiandikia hundi ambapo alikuwa akijilipa yeye mwenyewe.

Polisi wa upelelezi waliamua kuhamishia upelelezi wao katika benki hiyo iliyoko katika jiji la New York ambapo walikwenda na zile taarifa za benki (Bank statements) walizozikuta zimesambaa sakafuni baada ya mauaji yale kutokea. Hata hivyo mapaka kufikia hapo, bado polisi walikuwa hawajpata ushahidi wa kina wa kumfungulia mchungaji Canning mashitaka kuhusiana na mauaji ya ajuza wale.
Msemaji mwingine wa timu hiyo ya upelelezi wa Robert Glick alisema kwamba wanao ushihidi mwingine kutoka kwa raia mwema anaeishi jirani na kanisa la mchungaji Canning ambae alibainisha kwamba siku ile yalipotokea mauaji alimuona mchungaji huyo akienda na kurudi mara kwa mara kwenye shimo la taka lililoko jirani na kanisa hilo ambapo inasemekana kwamba huenda alikuwa antafuta namna ya kuizika miili ya ajuza wale. Askari wa upelelezi walipoenda kuchunguza nyumbani kwa mchungaji huyo walikuta saa ya mkononi ambayo ilikuwa na matone ya damu, damu hiyo ilipochunguzwa aktika maabara ilikuja kugundulika kuwa ilikuwa ni ya Leo Gleese. Mpaka kufikia hapo Polisi wakawa na uhakika kwamba sasa wamembaini muuaji wa Leo na

Hazel Gleese, nae si mwingine bali ni Mchungaji John Nelson Canning.
Siku chache baada ya kuongoza mazishi ya ajuza wale mchungaji Canning alikamatwa na kushitakiwa kwa mauaji ya ajuza wale. Katika kesi hiyo mchungaji Canning alikiri kuwa aliwauwa Leo na mkewe Hazel Gleese kwa kuwapiga kwa kitu kizito na kisha kuwanyonga usiku wa Januari 3, 1995, hiyo ilitokea baada ya kuwa amebanwa na ajuza hao kuhusiana na namna alivyotumia fedha zao huku wakimuonyesha taarifa ya benki inayoonyesha kwamba alijiandikia hundi na kujilipa yeye mwenyewe.

Mnamo Februari 1996 mchungaji John Nelson Canning alipatikana na hatia ya kuhusika na mauaji ya Leo na Hazel Gleese ambapo alihukumiwa kifungo cha maisha jela bila ya uwezekano wa kupata msamaha wa kifungo cha nje (Parole). Mara baada ya kusomwa hukumu hiyo msemaji wa Polisi Phil Ramer aliwaambia wandishi wa habari kwamba hili ni tukio ambalo hatakuja kulisahau katika maisha yake.

Kwa maneno yake mwenyewe alisema “ni vyema watu wakawa waaminifu, ni jambo la kushangaza kukuta mchungaji ambae ameaminiwa na waumini wake kisha anakuja kuwaua baadae kwa sababu ya pesa”

*********************MWISHO*********************

1 comment:
Andika Maoni Maoni
  1. Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti!Saturday, December 05, 2009

    nataka kuwa nchungaji....lol

    wakati mwingine katika maisha yetu ya kila siku tunatenda isivo kwa nini lakini?

    ReplyDelete

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi