Kuchagua mwenza: Pale mwanamke anapojikuta anaangukia kulamba GARASA…!
Linapokuja swala la mapenzi, wanawake ndio wanaokabiliwa na changamoto nyingi katika kuchagua mwenza hususan pale wanapokuwa wametokana na wanaume kadhaa ambao wameonyesha nia. Kutoka huko hakumaanishi kukutana kimwili bali hata kule kuwa na mitoko (dates) za mara kwa mara ambapo zote zinaonekana kuzaa matunda, hapo ndipo wanawake hujikuta wakikabiliwa na mtihani mzito wa kuchagua kwamba aolewe na yupi.Nimeshawahi kuwasikia baadhi ya wanawake ambao niko nao karibu wakidai kwamba wanajuta kwa sababu uchaguzi wa wenza waliooana nao haukuwa sahihi kwa sababu ya changamoto wanazokabiliana nazo katika ndoa zao tofauti na matarajio yao.