0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Feb 10, 2009

KWA HILI, UCHAWI HAUNA NAFASI

Furaha yote ya ndoa inaweza kuishia hapa.

Tafadhali ningeomba kusisitiza tena kwamba hupaswi kuwa mtumwa wa mwanamke au mwanaume. Leo hii kuna wanawake na wanaume ambao maisha yao ya ndoa yamekuwa ni jela zao wenyewe. Wanaume na wanawake hawa wamekuwa wakiishi kama vile roho zao ni hao wanaume au wanawake.

Bahati mbaya ni kwamba ndugu na jamaa wa wanaume au wanawake hao huwa wanadhani kwamba ndugu zao wamelogwa na wanawake au wanaume hao wanaowageuza watumwa wao. Je unajua kwamba kuna wanaume hapa nchini ambao huwa wanaombwa na wake zao wahame vyumba kwa sababu wake hao wana wageni ambao ni mahawara zao?

Je unajua kwamba kuna wake wa ndoa ambao huwa wanaletewa na wanaume zao mahawara wa wanaume hao kila wakati na kutambulishwa kwao kwamba “Huyu ni hawara yangu” na bado wake hao wakanyamaza na kuendelea kuwaheshimu waume zao? Wapo, tena wengi kuliko unavyoweza kuamini wewe.

Basi kwa taarifa yako hakuna uchawi wala limbwata katika jambo hili, bali kuna utegemezi wa kiakili na hata kimwili. Mwanamke au mwanaume anafikia mahali ambapo anaamini kwamba akiachwa au kuachana na mke au mume aliyenaye hataweza kuishi kwa amani tena, hatamudu kamwe kuishi bila kumuona. Wengine wanaamini kwamba wakiachana na waume au wake hao hawatamudu maisha peke yao. Huu ni utegemezi mbaya kuliko sumu inayouwa haraka.

Kituo cha FAJI kilichoko Kimara kona kinatoa ofa kwa watu wenye matatizo kama haya au wenye ndugu walio kwenye vifungo hivi wafike kwenye kituo chetu kwenye jengo lililoandikwa “ELIMU YA UTAMBUZI INAPATIKANA HAPA” au watupigie simu kwa namba hizi: +255 713 250701, +255 0715 729292 au +255 754 771601 pia wanaweza kutuandikia kupitia anuani ya barua pepe ya blog hii:
kaluse2008@gmail.com ili tuwape msaada na pia kuwaonyesha kwamba huko sio kulogwa.
This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi